6 Basi kama tumo katika dhiki, hiyo ni kwa ajili ya faraja na wokovu+ wenu; au kama tunafarijiwa, hiyo ni kwa ajili ya faraja yenu inayotenda ili kuwafanya mvumilie mateso yaleyale ambayo sisi pia tunateseka.+
17 Hata hivyo, hata ikiwa ninamiminwa kama toleo la kinywaji+ juu ya dhabihu+ na utumishi wa watu wote ambako imani imewaongoza ninyi,+ mimi nafurahi na kushangilia+ pamoja nanyi nyote.
24 Ninashangilia sasa katika mateso yangu kwa ajili yenu,+ nami, kwa upande wangu, ninajazia kinachopungua cha dhiki+ za Kristo katika mwili wangu kwa ajili ya mwili wake, ambao ni kutaniko.+
8 Kwa hiyo, tukiwa na upendo mwororo kwa ajili yenu,+ tulipendezwa vema kuwapa ninyi, si habari njema ya Mungu tu, bali pia nafsi zetu wenyewe,+ kwa sababu ninyi mlikuwa wapendwa+ kwetu.
17 Watiini wale wanaoongoza katikati yenu+ na mnyenyekee,+ kwa maana wanaendelea kuzilinda nafsi zenu kama wale watakaotoa hesabu;+ ili wafanye hivyo kwa shangwe na si kwa kuugua, kwa maana kufanya hivyo kungewadhuru ninyi.+