-
1 Mambo ya Nyakati 17:7-10Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
7 “Sasa mwambie hivi mtumishi wangu Daudi: ‘Yehova wa majeshi anasema hivi: “Nilikutoa malishoni, ili usiendelee kuchunga kondoo, uwe kiongozi wa watu wangu Waisraeli.+ 8 Nami nitakuwa pamoja nawe popote utakapoenda,+ nami nitawaangamiza maadui wako wote kutoka mbele yako;+ nami nitakujengea jina kama jina la watu maarufu duniani.+ 9 Nitachagua mahali kwa ajili ya watu wangu Waisraeli na kuwaweka humo, nao wataishi humo na hawatasumbuliwa tena; na watu waovu hawatawakandamiza* tena kama walivyofanya zamani,+ 10 tangu siku nilipowaweka waamuzi juu ya watu wangu Waisraeli.+ Nami nitawashinda maadui wako wote.+ Pia, ninakuambia, ‘Yehova atakujengea nyumba.’*
-
-
1 Mambo ya Nyakati 28:4Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
4 Hata hivyo, Yehova Mungu wa Israeli alinichagua kutoka katika nyumba yote ya baba yangu niwe mfalme wa Israeli milele,+ kwa maana alimchagua Yuda kuwa kiongozi+ na kutoka katika nyumba ya Yuda aliichagua nyumba ya baba yangu,+ na kati ya wana wa baba yangu alinikubali mimi niwe mfalme wa Israeli yote.+
-