-
Kutoka 12:3-14Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
3 Liambieni kusanyiko lote la Waisraeli hivi: ‘Siku ya kumi ya mwezi huu, kila mmoja wao anapaswa kuchukua kondoo kwa ajili ya nyumba ya baba yake, kondoo+ mmoja kwa kila nyumba. 4 Lakini ikiwa familia ina watu wachache hivi kwamba hawawezi kummaliza kondoo mmoja, watagawana* na jirani yao wa karibu ndani ya nyumba yao kulingana na idadi ya watu.* Mnapofanya hesabu, kadirieni kiasi cha nyama ya kondoo kitakacholiwa na kila mtu. 5 Kondoo wenu anapaswa kuwa kondoo dume wa mwaka mmoja, asiye na kasoro.+ Mnaweza kuchagua mwanakondoo dume au mwanambuzi. 6 Mtamtunza mpaka siku ya 14 ya mwezi huu,+ na familia zote katika kusanyiko la Israeli zinapaswa kumchinja jioni kabla ya giza kuingia.*+ 7 Watachukua kiasi fulani cha damu na kuinyunyiza kwenye miimo miwili ya mlango na kwenye kizingiti cha juu cha mlango wa nyumba ambamo watamla mnyama huyo.+
8 “‘Ni lazima waile nyama hiyo usiku huo.+ Wanapaswa kuichoma juu ya moto na kuila pamoja na mikate isiyo na chachu+ na mboga chungu za majani.+ 9 Msile sehemu yoyote ya nyama hiyo ikiwa mbichi au ikiwa imechemshwa, yaani, ikiwa imepikwa kwa maji, lakini ichomeni juu ya moto, kichwa chake pamoja na miguu yake na viungo vyake vya ndani. 10 Hampaswi kuhifadhi sehemu yoyote ya nyama hiyo mpaka asubuhi, lakini sehemu yoyote itakayobaki mpaka asubuhi mnapaswa kuiteketeza kwa moto.+ 11 Na hivi ndivyo mnavyopaswa kuila, mkiwa mmejifunga mishipi,* mkiwa na viatu miguuni, na mkiwa na fimbo zenu mkononi; nanyi mnapaswa kuila haraka. Ni Pasaka ya Yehova. 12 Kwa maana nitapita katikati ya nchi ya Misri usiku huo na kumuua kila mzaliwa wa kwanza katika nchi ya Misri, kuanzia mwanadamu mpaka mnyama;+ nami nitatekeleza hukumu dhidi ya miungu yote ya Misri.+ Mimi ni Yehova. 13 Ile damu itakuwa ishara inayoonyesha nyumba mtakazokuwamo; nami nitaiona damu hiyo na kupita juu yenu, na pigo halitawajia na kuwaangamiza ninyi nitakapoipiga nchi ya Misri.+
14 “‘Siku hiyo itakuwa ukumbusho kwenu, nanyi mnapaswa kuisherehekea ikiwa sherehe kwa Yehova katika vizazi vyenu vyote. Kwa kuwa ni sheria ya kudumu, mnapaswa kuisherehekea.
-