-
2 Mambo ya Nyakati 28:24, 25Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
24 Zaidi ya hayo, Ahazi alikusanya vyombo vya nyumba ya Mungu wa kweli; akavikata vipandevipande vyombo vya nyumba ya Mungu wa kweli,+ akaifunga milango ya nyumba ya Yehova,+ na kujitengenezea madhabahu katika kila pembe ya Yerusalemu. 25 Na katika majiji yote ya Yuda, alijenga mahali pa juu pa kuifukizia moshi wa dhabihu miungu mingine,+ akamkasirisha Yehova Mungu wa mababu zake.
-