-
1 Samweli 31:8-10Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
8 Siku iliyofuata, Wafilisti walipokuja kuwavua waliouawa vitu walivyokuwa navyo, walimkuta Sauli na wanawe watatu wakiwa wameanguka kwenye Mlima Gilboa.+ 9 Basi wakamkata kichwa na kumvua silaha zake na kutuma ujumbe kotekote katika nchi ya Wafilisti ili habari+ zienezwe katika nyumba za* sanamu zao+ na miongoni mwa watu. 10 Kisha wakaweka silaha zake katika nyumba ya sanamu za Ashtorethi na kuitundika maiti yake kwenye ukuta wa Beth-shani.+
-