-
2 Samweli 5:6-10Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
6 Mfalme na wanaume wake wakaenda Yerusalemu kuwashambulia Wayebusi+ waliokuwa wakiishi nchini. Walimdhihaki Daudi wakisema: “Hutaingia humu kamwe! Hata vipofu na vilema watakufukuza.” Hivi ndivyo walivyofikiri: ‘Daudi hataingia humu kamwe.’+ 7 Hata hivyo, Daudi akaiteka ngome ya Sayuni, ambayo sasa ni Jiji la Daudi.+ 8 Basi siku hiyo Daudi akasema: “Wale wanaowashambulia Wayebusi wanapaswa kupitia kwenye mfereji wa maji ili wawaue ‘vilema na vipofu,’ wanaomchukia Daudi!”* Ndiyo sababu watu wanasema: “Vipofu na vilema hawataingia nyumbani.” 9 Kisha Daudi akaanza kukaa katika ngome hiyo, nayo ikaitwa* Jiji la Daudi; na Daudi akaanza kujenga pande zote kuanzia kwenye Kilima*+ kuja ndani.+ 10 Kwa hiyo Daudi akawa mkuu zaidi na zaidi,+ na Yehova Mungu wa majeshi alikuwa pamoja naye.+
-