Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 28:49, 50
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 49 “Yehova ataleta dhidi yenu taifa la mbali,+ kutoka mwisho wa dunia; litawarukia kama tai,+ taifa ambalo hamtaelewa lugha yake,+ 50 taifa lenye uso mkali ambalo haliwajali wazee wala kuwahurumia vijana.+

  • 2 Wafalme 15:29
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 29 Katika siku za utawala wa Mfalme Peka wa Israeli, Mfalme Tiglath-pileseri+ wa Ashuru alivamia na kuteka Iyoni, Abel-beth-maaka,+ Yanoa, Kedeshi, Hasori, Gileadi,+ na Galilaya,+ nchi yote ya Naftali,+ akawapeleka wakaaji wa maeneo hayo uhamishoni kule Ashuru.+

  • 2 Wafalme 17:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 Katika mwaka wa tisa wa utawala wa Hoshea, mfalme wa Ashuru aliliteka jiji la Samaria.+ Kisha akawapeleka Waisraeli uhamishoni+ kule Ashuru na kuwaweka katika eneo la Hala na Habori kando ya mto Gozani+ na katika majiji ya Wamedi ili waishi humo.+

  • Isaya 7:20
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 20 “Siku hiyo, kwa kutumia wembe uliokodiwa kutoka eneo la ule Mto,* kwa kumtumia mfalme wa Ashuru,+ Yehova atanyoa kichwa na nywele za miguu, nao utafagilia mbali ndevu pia.

  • Isaya 8:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 4 kwa maana kabla mvulana huyo hajajua jinsi ya kuita, ‘Baba yangu!’ na ‘Mama yangu!’ mali za Damasko na nyara za Samaria zitachukuliwa mbele ya mfalme wa Ashuru.”+

  • Isaya 10:5, 6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  5 “Aha! Mwashuru,+

      Fimbo ya kuonyesha hasira yangu,+

      Na gongo lililo mkononi mwao kwa ajili ya shutuma yangu!

       6 Nitamtuma yeye dhidi ya taifa lililoasi imani,+

      Dhidi ya watu walionikasirisha,

      Nitamwamuru achukue nyara nyingi na kupora mali nyingi

      Na kuzikanyaga kama matope barabarani.+

  • Hosea 10:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  6 Itapelekwa Ashuru kama zawadi kwa mfalme mkuu.+

      Waefraimu wataaibishwa,

      Na Waisraeli wataaibika kwa sababu ya ushauri waliofuata.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki