Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Isaya 61:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  7 Badala ya aibu mtakuwa na fungu mara mbili,

      Na badala ya fedheha watapiga vigelegele kwa shangwe kwa sababu ya fungu lao.

      Naam, watamiliki fungu mara mbili katika nchi yao.+

      Watakuwa na shangwe milele.+

  • Yeremia 30:10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 “Nawe, mtumishi wangu Yakobo, usiogope,” asema Yehova,

      “Wala usihofu, Ee Israeli.+

      Kwa maana nitakuokoa kutoka mbali

      Na uzao wako kutoka katika nchi waliyopelekwa utekwani.+

      Yakobo atarudi na kuwa na utulivu bila usumbufu,

      Na hakuna yeyote atakayewaogopesha.”+

  • Yeremia 33:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 Nami nitawarudisha mateka wa Yuda na mateka wa Israeli,+ nami nitawajenga kama nilivyofanya mwanzoni.+

  • Yeremia 33:9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 9 Naye atakuwa kwangu jina la furaha, sifa, na uzuri mbele ya mataifa yote ya dunia yatakayosikia kuhusu wema wote nitakaowapa.+ Nao wataogopa na kutetemeka+ kwa sababu ya wema na amani ninayompa.’”+

  • Ezekieli 39:25
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 25 “Kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Nitawarudisha watu wa Yakobo waliotekwa+ na kuwaonyesha rehema watu wote wa nyumba ya Israeli;+ nami nitalitetea jina langu takatifu kwa bidii.*+

  • Ezekieli 39:27
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 27 Nitakapowarudisha kutoka katika mataifa na kuwakusanya pamoja kutoka katika nchi za maadui wao,+ mimi pia nitajitakasa miongoni mwao mbele ya macho ya mataifa mengi.’+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki