Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 21:22, 23
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 22 “Mtu akitenda dhambi inayostahili hukumu ya kifo, naye ameuawa,+ na mmemtundika mtini,+ 23 maiti yake isibaki mtini usiku kucha.+ Badala yake, mnapaswa kuhakikisha kwamba mnaizika siku hiyohiyo, kwa sababu mtu aliyetundikwa ni kitu kilicholaaniwa na Mungu,+ nanyi hampaswi kuichafua nchi ambayo Yehova Mungu wenu anawapa iwe urithi wenu.+

  • Mathayo 27:57-60
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 57 Sasa kwa kuwa ilikuwa jioni, akaja tajiri mmoja wa Arimathea, aitwaye Yosefu, ambaye pia alikuwa mwanafunzi wa Yesu.+ 58 Mtu huyu alienda kwa Pilato akaomba apewe mwili wa Yesu.+ Naye Pilato akaamuru apewe.+ 59 Yosefu akauchukua mwili huo, akaufunga kwa kitani bora kilicho safi,+ 60 akaulaza katika kaburi lake jipya,*+ alilokuwa amechimba katika mwamba. Kisha akaviringisha jiwe kubwa kwenye mwingilio wa lile kaburi,* akaondoka.

  • Marko 15:43-46
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 43 akaja Yosefu wa Arimathea, mshiriki wa Baraza aliyeheshimiwa, ambaye pia alikuwa akiungojea Ufalme wa Mungu. Akajipa moyo na kwenda kwa Pilato, akaomba apewe mwili wa Yesu.+ 44 Lakini Pilato akataka kujua kama tayari alikuwa amekufa, akamwita yule ofisa wa jeshi, akamuuliza ikiwa Yesu alikuwa amekufa. 45 Baada ya kuhakikisha kutoka kwa huyo ofisa wa jeshi, akamruhusu Yosefu auchukue mwili huo. 46 Baada ya kununua kitani bora, akamshusha na kumfunga kwa kile kitani bora na kumlaza katika kaburi*+ lililokuwa limechimbwa katika mwamba; kisha akaviringisha jiwe kwenye mwingilio wa lile kaburi.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki