6Akina ndugu, hata mtu akichukua hatua isiyofaa kabla hajajua, ninyi mlio na sifa za kustahili kiroho jaribuni kumrekebisha upya mtu huyo kwa roho ya upole.+ Lakini kila mmoja wenu aendelee kujiangalia,+ kwa kuwa ninyi pia mnaweza kujaribiwa.+
4Kwa hiyo, mimi mfungwa+ katika Bwana, ninawasihi mtembee kwa kustahili+ mwito mliopokea, 2 kwa unyenyekevu*+ wote na upole, kwa subira,+ mkivumiliana kwa upendo,+
24 Kwa maana mtumwa wa Bwana hahitaji kupigana, bali anahitaji kuwa mpole* kwa wote,+ mwenye uwezo wa kufundisha, anayejizuia anapokosewa,+25 akiwafundisha kwa upole wale wasio na mwelekeo unaofaa.+ Huenda Mungu akawasaidia kutubu* na kupata ujuzi sahihi wa kweli,+
15 Bali mtakaseni Kristo kuwa Bwana katika mioyo yenu, sikuzote mkiwa tayari kujitetea mbele ya kila mtu anayewauliza sababu ya tumaini mlilo nalo, lakini mkifanya hivyo kwa upole+ na heshima kubwa.+