-
1 Timotheo 1:3, 4Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
3 Kama nilivyokutia moyo ubaki Efeso nilipokuwa karibu kwenda Makedonia, sasa ninakutia moyo ufanye vivyo hivyo, ili uwaamuru watu fulani wasifundishe mambo tofauti, 4 wala kusikiliza hadithi za uwongo+ na kuchunguza-chunguza ukoo. Mambo hayo hayaleti manufaa yoyote+ bali hutokeza maswali badala ya kuleta chochote kutoka kwa Mungu kuhusiana na imani.
-
-
1 Timotheo 6:3-5Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
3 Mtu yeyote akifundisha mafundisho tofauti na yanayopingana na fundisho lenye manufaa*+ linalotoka kwa Bwana wetu Yesu Kristo, au mafundisho yasiyopatana na ujitoaji-kimungu,*+ 4 yeye anajivuna kwa kiburi na haelewi chochote.+ Pia, anapenda sana* kubishana na kushindana kuhusu maneno.+ Mambo hayo huleta wivu, mizozo, uchongezi,* na shaka zenye uovu, 5 mabishano ya kawaida kuhusu mambo madogo madogo ya watu waliopotoka kiakili+ na wasiojua kweli, wakifikiri ujitoaji-kimungu* ni njia ya kupata faida.+
-