Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g99 2/22 kur. 3-4
  • Je, Wewe Huizungumzia Dini?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Wewe Huizungumzia Dini?
  • Amkeni!—1999
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Kutovumiliana Huwavunja Wengi moyo
  • Nani Anayependezwa na Dini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
  • Ninaweza Kuipataje Dini ya Kweli?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Sehemu ya 24: Sasa na milele—Mazuri ya Milele ya Dini ya Kweli
    Amkeni!—1990
  • Kuzoea Dini Safi Kwa Ajili Ya Kuokolewa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1999
g99 2/22 kur. 3-4

Je, Wewe Huizungumzia Dini?

“Tafadhali, acha tubadilishe mazungumzo. Kunayo mambo mawili ambayo siyazungumzii kamwe—dini na siasa!”

“Mimi humwachia mke wangu na watoto wangu dini.”

“Sitaki kuizungumzia dini sasa. Nimetoka tu kanisani.”

JE, WEWE husikia maelezo kama hayo kwa ukawaida? Watu fulani hawapendelei kuizungumzia dini kwa sababu wanaiona kuwa jambo la kibinafsi, yaani kati yao na Mungu. Yesu alisema hivi: “Usalipo ingia ndani ya chumba chako cha faragha na, baada ya kufunga mlango wako, sali kwa Baba yako aliye katika siri; ndipo Baba yako atazamaye katika siri atakurudishia wewe.”—Mathayo 6:6.

Kwa upande mwingine, Yesu na wanafunzi wake hawakuona kwamba kila jambo linalohusu dini lapaswa kuwa la kibinafsi. Waliongea kwa uhuru na kusema waziwazi juu ya masuala mengi ya kiroho, na tokeo likawa kwamba mafundisho yao yalienezwa ulimwenguni pote. (Matendo 1:8; Wakolosai 1:23) Bila shaka, si kila mtu aliyetaka kuzungumza nao, na baadhi ya watu waliozungumza nao waliendelea kutilia shaka.

Leo pia, mtazamo wa watu mmoja-mmoja na tamaduni mbalimbali kuelekea kuizungumzia dini hutofautiana. Kwa mfano, katika nchi nyingi za Magharibi, watu wana mwelekeo wa kuhangaikia sana mambo ya kilimwengu—elimu, kazi ya kuajiriwa, michezo, televisheni, kompyuta, na kadhalika. Katika tamaduni nyinginezo, watu wako tayari kuzungumzia imani zao. Na bado, bila kujali hali za watu, kuna mambo fulani yanayotukia katika maisha yao ambayo huwafanya baadhi ya watu ambao hapo mwanzoni hawakupendezwa na dini wachunguze upya uhitaji wao wa kiroho.

Kutovumiliana Huwavunja Wengi moyo

Wale wanaokataa kuizungumzia dini huenda waliona au kuhusika katika mazungumzo yaliyotokeza hasira kali na kugeuka kuwa mabishano makali. “Tofauti za kidini hutokeza ugomvi mwingi zaidi kuliko tofauti za kisiasa,” akasema mhutubu mmoja mwenye kujulikana sana. Pia, Richard M. Johnson, aliyekuwa makamu wa rais wa Marekani, alionelea hivi: “Ushupavu wa kidini hutokeza chuki mbaya sana isiyo na sababu katika akili ya mwanadamu; na, unapokuwa umepotoka, ushupavu huo huamsha hisia kali, zilizo mbaya sana za asili yetu huku kukiwa na kisingizio cha kwamba tunamtumikia Mungu.”

Je, haikushangazi kwamba mafundisho ya Biblia, ambayo yana uwezo wa kuadilisha na kukuza hadhi, yanatumiwa vibaya ili kuendeleza kutovumiliana, kung’ang’ania imani, na chuki? Kwa kweli, si mafundisho ya Biblia yanayowafanya wengi waikatae dini. Badala yake, ni kule kuyapotosha. Kwa mfano, fikiria Ukristo.

Kupitia neno na kielelezo, Mwanzilishi wa Ukristo, Yesu Kristo, alitia moyo kupenda Mungu na kupenda jirani, wala si kutovumiliana na ushupavu. Kristo na wafuasi wake walitumia mbinu za kusababu na kushawishi katika huduma yao. (Mathayo 22:41-46; Matendo 17:2; 19:8) Nao waliwaombea maadui na wanyanyasi wao.— Mathayo 5:44; Matendo 7:59, 60.

Kupitia neno na kielelezo, Mwanzilishi wa Ukristo, Yesu Kristo, alitia moyo kupenda Mungu na kupenda jirani, wala si kutovumiliana na ushupavu. Kristo na wafuasi wake walitumia mbinu za kusababu na kushawishi katika huduma yao. (Mathayo 22:41-46; Matendo 17:2; 19:8) Nao waliwaombea maadui na wanyanyasi wao.—Mathayo 5:44; Matendo 7:59, 60.

Dini ya kweli huelimisha akili na moyo, na huwaunganisha watu. Kwa hiyo, kama tutakavyoona, mazungumzo yenye heshima yanayohusu dini yaweza kuleta matokeo mazuri sana kwa wale wanaotafuta kweli kwa moyo mweupe.

[Sanduku katika ukurasa wa 3]

Yale Ambayo Watu Mashuhuri Wamesema

“Ikiwa Yesu ndiye njia iongozayo kwa Mungu, ni lazima wafuasi wa Yesu washiriki na wengine habari hiyo.”—Ben Johnson, profesa wa somo la kueneza evanjeli katika Seminari ya Theolojia ya Co­lum­bia.

“Yesu aliwafundisha wanafunzi wake kuwapelekea watu gospeli. Hilo Agizo Kuu latuamuru kwenda katika ulimwengu wote. Bwana aliwaamuru wafuasi wake waende kotekote.”—Kenneth S. Hemphill, mkurugenzi wa Southern Baptist Center for Church Growth.

“Isipokuwa tuwe mashahidi, hatuwezi kuwa Wakristo halisi. . . . Kila Mkristo anahitajiwa awe mishonari na shahidi.”—Papa John Paul wa Pili.

Wahubiri wengi sana . . . wanapendezwa zaidi kujenga makutaniko makubwa na miradi ya ujenzi wa makanisa na mgawo wao wa uchungaji unaofuata kuliko vile wanavyopendezwa kuhubiri ujumbe usioridhiana na usiopendeza ulio katika Gospeli.”—Cal Thomas, mtungaji na mwandishi wa safu za gazeti.

“Ni lazima tubishe milango . . . Kama wafanyavyo Mashahidi (wa Yehova) na baadhi ya watu wengine, ni lazima twende na kutangaza Gospeli ya Yesu Kristo.”—Thomas V. Daily, askofu Mkatoliki.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki