Ufahamu Katika Habari
Papa Atatiza Watu Juu ya Siasa
● Agizo la Papa John Paul wa Pili hivi karibuni kwamba viongozi wa kidini ulimwenguni pote waache utendaji wa kisiasa limetokeza mvurugo fulani, Kasisi Myesuiti mwanabunge wa U.S. Robert Drinan amesema kwamba hatatafuta kuchaguliwa katika cheo hicho. Kwa upande mwingine, mtawa wa kike Carolyn Farrell, meya wa Dubuque, lowa, alisema kwamba hataacha, kwa kuwa wanawake “hawajapata kuwa katika cheo cha viongozi wa kidini.”
Hali, wakati uo huo, papa alikuwa akisihi washiriki wa kanisa Waafrika washiriki katika siasa: “Jambo la maana la Mkristo kukazania ni lile la maisha ya kisiasa,” aliambia wasikilizaji wengi katika Nairobi, Kenya. “Katika taifa raia wana haki na wajibu wa kushiriki katika maisha ya kisiasa.” Papa aliongeza kwamba “lingekuwa kosa kuwaza kwamba Mkristo mmoja mmoja hapaswi kujiingiza katika sehemu hizo za maisha.”
Ikitoa maelezo juu ya kanuni inayoelekea kupingana kati ya agizo la papa kwa viongozi wa kidini na utendaji wake wa kisiasa katika Poland na katika kanisa, makala ya mhariri ya gazeti New York Times ilisema hivi: “Inaonekana kuwa si siasa ambazo Papa anataka makasisi waache, bali kuchaguliwa katika vyeo.” Kwa sababu ya tangazo la Yesu kwamba wanafunzi wake “si wa ulimwengu; kama mimi pia nisivyo wa ulimwengu,” je! twaweza kumwazia akisema mambo hayo yenye kupingana?—Yohana 17:14; 18:36, Catholic Douay Version.
Mungu Yuko Upande wa Nani?
● Hivi karibuni, gazeti Brazil Herald lilitoa maelezo juu ya namna timu ya mpira ya Atletico kutoka Belo Horizonte ilivyosherehekea kwa kelele ushindi wao juu ya timu ya Fluminense kutoka Rio de Janeiro. Walakini gazeti Herald lilisema kwamba wanne wa timu ya Atletico, “ambao waliongolewa wakawa Waprotestanti hivi karibuni, walijitenga, wakifungua Biblia na kumshukuru Bwana kuwasaidia washinde Fluminense.”
Je! ni jambo la akili kumwuliza au kumshukuru Mungu kwa ajili ya ushindi kama huo? Ni ombi la nani linalopaswa kutimizwa wakati watu wanyofu pande zote mbili wanapotoa sala wapate ushindi? Likiona jambo hilo hatua hilo, gazeti Brazil Herald lilipeleka ulizo hilo hatua moja zaidi: “Hiyo inatokeza ulizo linaloulizwa mara nyingi na watu ambao hawajalevywa sana na uzalendo wakati wa vita: Kwa nini Bwana anaonea upande ule mwingine—katika habari hii, kuonea timu ya Fluminense kutoka Rio, hata aunge mkono upande mmoja wa timu ya Atletico? Pengine watu hao watawa wa wanazidisha sana kupendezwa kwa Bwana na matokeo ya mchezo wa mpira—pengine vita kati ya mataifa.”
Hakika Mungu hawezi kuwa na daraka la kushinda au kushindwa kwa upande mmoja katika michezo au vita vya kumwaga damu vinavyopiganwa na wanadini kati yao wenyewe. Jibu wanalopewa watu hao wanaotoa sala ya kutaka msaada wa Mungu upande wao ni kama lile alilolipa taifa la Israeli lenye kuasi: “Nanyi mkunjuapo mikono yenu, nitaficha macho yangu nisiwaone; naam, mwombapo maombi mengi, sitasikia; mikono yenu imejaa damu.” Mahali pa kuunga mkono upande fulani katika vita vya watu, Wakristo wa kweli wataendelea kutokuwamo, wakitoa sala kwa ajili ya ufalme wa Mungu peke yake.—Isa. 1:15, 16; 2:4; Mt. 6:9, 10.