Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w88 2/15 kur. 22-23
  • Kisiwa Thursday Chasikia Zile Habari Njema

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kisiwa Thursday Chasikia Zile Habari Njema
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Vichwa vidogo
  • Habari Njema Zafikia Visiwa Hivi
  • Kundi Lafanyizwa
  • Kufikia Vile Visiwa Vingine
  • Mahali Pazuri pa Kukutania
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
w88 2/15 kur. 22-23

Kisiwa Thursday Chasikia Zile Habari Njema

WAKATI ile ndege inapozunguka kwa kupiga duara, kile tu ambacho sisi tunaweza kuona ni kibumba cha visiwa vyenye maumbo na ukubwa mbalimbali katikati ya bahari ya rangi kijani-buluu. Tunapokaribia kugusa chini, tunaona ile njia ya ndege kukimbilia​—ni kadogo kama nini—​lakini inatusaidia kutusha moyo kama nini!

Sisi tumetua juu ya Kisiwa Horn. Baada ya kisafari cha kutumia basi kwenda kwenye gati, kivukio kidogo kinatupeleka sisi kwenye Kisiwa Thursday, ambapo ndipo mahali pa kati pa Vile Visiwa Torres Strait. Visiwa hivyo vinatandaa kama mawe ya kukanyagia kutoka ile ncha ya kaskazini ya Queensland, Australia, moja kwa moja mpaka kuvuka kwenda Papua New Guinea.

Wakati wa yale majira yenye joto na mvua-mvua (Januari mpaka Mei), kila kitu kinakuwa cha rangi ya kijani na chenye kusitawi sana. Pepo zenye kuzunguka-zunguka kwa nguvu sana zinatokea wakati fulani, zikifanya iwe hatari kutoka kwenye kisiwa kimoja kwenda kwenye kisiwa kingine. Kwa sehemu iliyobaki ya mwaka, kawaida ni kuwa na ukavu na vumbi-vumbi.

Habari Njema Zafikia Visiwa Hivi

Ilikuwa katika 1938 kwamba Lightbearer, kimerikebu cha meta 16 cha Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi, kilisimama kwa muda mfupi kwenye visiwa hivyo kikiwa njiani kuelekea Dutch East Indies (sasa Indonesia). Waliokuwamo walikuwa watu saba wa Mashahidi wa Yehova, wenye hamu nyingi ya kushiriki na wengine ujumbe wa Biblia wa tumaini.

Hata hivyo, bila ya ndugu hao kujua, mmoja wa wamisionari wa Jumuiya ya Wakristo alifika karibu wakati ule ule. Yeye aliambia wanavisiwa wasisikilize Mashahidi hao au kukubali vyo vyote vya vitabu vyao. Lakini wakati akina ndugu walipofika nyumbani kwake na kusema naye, yeye alikubali vitabu vinne. Watu fulani kati ya wanavisiwa hao waliona jambo hilo, kwa hiyo wao wakafikiri: ‘Ikiwa yeye anaweza kuwa navyo, mbona sisi tusiwe navyo?’ Jioni hiyo, wakati wale Mashahidi wengine walipokuwa wakionyesha picha-slaidi, ndugu mmoja aliketi nje akiwa na vibweta vya vitabu. Katika lile giza, kukawa kukitokea-tokea mkono wenye pesa, na sauti yenye kuomba kitabu. Katika muda wa saa moja tu, vitabu 200 viliangushwa kwa njia hiyo! Baadaye, yule mmisionari alijaribu bila fanikio kutumia vitabu ambavyo alikuwa amechukua kama ithibati ya kutoa shtaka dhidi ya Mashahidi.

Kundi Lafanyizwa

Mbegu zile za kwanza za ukweli hazikutiliwa maji kwa wakati mrefu. Msaada wa ziada haukufika katika visiwa hivi vilivyo peke yavyo mpaka miaka ya mwisho-mwisho ya 1950. Wafanya kazi wawili wa wakati wote walitumwa na Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi. Wao walifuatwa na akina Rudd, jamaa moja ya watu watatu, ambayo ilikuja kutumikia mahali ambako uhitaji ulikuwa mkubwa zaidi. Baada ya muda mfupi, kundi dogo lilifanyizwa katika Kisiwa Thursday.

Hizo zilikuwa nyakati zenye magumu, ambazo mahali pa kulala palipatikana kwa shida sana na kulikuwa na upinzani wa kutosha kutoka kwenye serikali na dini zile zenye kuwapo kwa muda mrefu. Mara ya kwanza lile kundi lilikutana katika chumba kidogo kilichokuwa juu ya mahali pale pale palipokuwa na majoko ya mwokaji wa eneo hilo. Ebu wazia tu jinsi mahali hapo palivyokuwa na joto jingi katika visiwa hivyo vya tropiki!

Kwa kung’amua uhitaji wa kuendelea kuwa imara kiroho, Mashahidi wale walipiga moyo konde kuhudhuria mkusanyiko mmoja katika pwani ya Australia bara, kama kilometa 1,300 kutoka huko. Kwa kuwa hawakuwa na nauli ya ndege, wao walitafuta kwa sala njia nyingine ya kwenda kwenye mkusanyiko huo.

Kwanza, akina ndugu walinunua mashua kuu-kuu ya kuvua lulu ambayo haikuwa na injini, kikata-maji, matanga, na nanga. Kwa kutafuta miongoni mwa mashua zilizo katara, mwishowe wao walipata moja inayotumia diseli, yenye injini kubwa ya silinda tano na yenye giaboksi. Kwa kununua hiyo, akina ndugu walifurahi sana kupata matanga, nanga za kutia, na sehemu nyingine nyingi. Hata hivyo, bado hakukuwa na ufito wa kushikilia kikata-maji wala kikata-maji chenyewe hakikuwako.

Ndugu Rudd aliuliza mwenye jahabu (mahali pa kutengenezea mashua) kama yeye angeweza kutazama-tazama eneo lenye kuzunguka mahali hapo. Mwenyewe alisema kwa utani kwamba ikiwa yeye angeweza kupata ufito mahali po pote katika eneo hilo, Mashahidi wangeweza kuuchukua. Mtu huyo mwenye mahali hapo alishangaa wakati ufito ulipopatikana. Akiwa anaenda kutoka nyumba kwa nyumba asubuhi kadha baadaye, Ndugu Rudd aligonga kwa mguu kitu fulani katika nyasi ndefu. Kitu hicho kilikuwa kikata-maji ambacho kingeifaa kabisa mashua yao!

Baada ya kutayarisha chombo kile, lile kundi la watu 25 lilikuwa tayari kwa safari-bahari ya siku saba. Walipokuwa wakiondoka, mchawi wa mahali pale aliweka “laana” juu yao. Usiku mmoja mashua ile ilikwama juu ya mwamba. Akina ndugu walitumia wakati huo kwa faida kukamata kadiri fulani ya samaki. Wakati wa kupwa-kujaa asubuhi, ile mashua ilielea juu ya maji ikaondoka mwambani, ingawa wao walilazimika kupigapiga maji kwa bomba ili yatoke mle ndani katika muda wote uliobaki wa kisafari kile.

Walipofika Townsville, Australia, tajiri mmoja mwenye jahabu alikuja kuwalaki. Inaonekana yeye alikuwa amesoma katika makala moja ya karatasi-habari juu ya jitihada zao kuhudhuria mkusanyiko ule, na yeye alisukumwa na moyo kusaidia. Yeye alisisitiza kutengeneza sehemu zilizoharibika za mashua ile hata ingawa wao hawangeweza kupata pesa za kulipa wala hawangeweza kusaidia kuitengeneza kwa sababu walikuwa kwenye mkusanyiko ule. Baadaye, walitozwa pauni 40 tu (dola 80 za United States) badala ya pauni 500 (dola 1,000 za United States), ambazo wangalitozwa zingalikuwa kiasi nafuu.

Kufikia Vile Visiwa Vingine

Kwa mwelekezo wa Yehova, ujumbe wa Ufalme umefikia pia visiwa vile vya nje-nje. Mathalani, Ndugu Rod Anderson na Allan Webster, ambao walihamia Kisiwa Thursday miaka michache iliyopita, wametumia mashua yao kutoa ushuhuda katika visiwa vingine. Kufikia sasa, kuhubiri kumefanywa katika 12 kati ya vile visiwa 17 vinavyokaliwa.

Mahali Pazuri pa Kukutania

Ingawa hivyo, kwa muda mrefu akina ndugu walishangaa wakijiuliza kama siku moja wangekuwa na Jumba la Ufalme lao wenyewe katika Kisiwa Thursday. Ndipo roho ya Yehova ikawa dhahiri katika kitendo. Katika Septemba 1983, Ndugu Graham Keen, mjenzi stadi, alihamia kisiwani kusaidia kujenga jumba. Hesabu fulani ya makundi ya Australia yalikuwa yameandaa kwa ukarimu vifaa vilivyohitajiwa kwa ujenzi. Vifaa hivyo vilipakiwa ndani ya mabweta fulani na kusafirishwa kwa meli kutoka Cairns, Queensland. Wanavisiwa walishangaa kuona rundiko hilo la vifaa vya kujengea vikiwa katika kisehemu cha ardhi kilichokuwa kitupu hapo kwanza. Ilichukua siku 140 tu za kazi kumaliza jumba lile, pamoja na mahali pa kukaa upande wa nyuma. Walikuwako wahudhuriaji wenye furaha 120 siku ambayo hilo jumba jipya liliwekwa wakfu.

Mashahidi wote walifurahi kama nini kupata hilo Jumba la Ufalme jipya kutumiwa kama mahali pa kati pa ile kazi ya kueneza habari njema katika Visiwa Torres Strait. Kwa msaada wa roho ya Yehova, wao wanafurahi sana kutangaza sifa kwa Yehova Mungu.​—Isaya 42:12.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki