Je! Wewe Unakumbuka?
Je! wewe umefurahia kusoma matoleo ya hivi majuzi ya Mnara wa Mlinzi? Basi, ona kama unaweza kujibu maswali yanayofuata:
◻ Ni nini kichwa cha uenezaji-evanjeli wa Kibiblia siku hizi?
Kiini cha ujumbe wa mwenezaji-evanjeli leo ni zile habari njema za Ufalme wa Mungu ulio mikononi mwa Mtawala wake mwekwa-rasmi, Yesu Kristo. Hiyo inatia ndani kweli zote alizonena Yesu na ambazo wanafunzi wake waliandika katika kumbukumbu.(Mathayo24:14; 28:19,20)—1/1, ukurasa 4.
◻ Kwa sababu gani inahitajiwa kabisa kuendeleza kuhubiri zile habari njema katika maeneo ambamo tokeo ni dogo au hamna lo lote?
Kupitia Kristo Yesu, Yehova ameamuru kwamba ‘habari njema zihubiriwe katika dunia yote inayokaliwa.’ (Mathayo 24:14, NW) Wakati watu wanapokataa kusikiliza, hiyo inatupa sisi nafasi ya kuonyesha urefu wa kina cha upendo wetu na bidii ya kujitolea Yehova kwa kufanya yanayofaa kwa udumifu. Pia, upendo wetu unatusukuma tuonye jirani zetu juu ya mambo yaliyoko wakati ujao kwa ajili ya aina ya binadamu. (1 Yohana 5:3; 2 Timotheo 4:2) -1/1, ukurasa 26.
◻ Ni manufaa gani ambazo huduma ya wakati wote inaletea wahubiri wengi wa Ufalme?
Inawasaidia kusitawisha kwa ukamili zaidi lile tunda la roho, kuonyesha upendo mwingi zaidi kwa watu, kuwa wenye matokeo zaidi katika huduma, na kumwitibari Yehova kwa kadiri kubwa zaidi. Kwa sababu hiyo, wao wanashangilia kuwa na uhusiano wa karibu zaidi pamoja na Yehova.—1/15, ukurasa 26.
◻ Waandikaji wote wa Biblia walielekeza kwenye mwelekezo na kusudi gani la Mungu wajapokuwa na tofauti za kutokeza habari zao?
Wote walionyesha mambo ambayo Yehova Mungu atatenda kufanya aina ya binadamu iwe yenye furaha, na pia mambo ambayo ni lazima wanadamu mmoja mmoja wafanye ili wapokee kibali cha Mungu.—2/1, ukurasa 7.
◻ Ni nini baadhi ya thawabu na manufaa zinazotokana na kuwa mfuataji haki?
Hali ya kuitibariana na kutumainiana kwa uhakika inasitawishwa, ikiongoza kwenye mielekeo na mahusiano yenye afya. Ufuataji haki unachangia pia dhamiri safi, na unampa mtu amani ya akili, hivi kwamba yeye anaweza kuelekeana na wengine bila hofu ya kuaibika. (Waebrania 9:14; 1 Timotheo 1:19) —2/15, ukurasa 7.
◻ Ni sala za nani ambazo Mungu aliye mweza yote anasikia na kujibu?
Yehova anasikia sala zinazotolewa kumwelekea yeye kupitia mfereji unaofaa, Yesu Kristo; katika njia inayofaa; na kwa mwelekeo unaofaa wa akili na moyo. Mungu anajibu sala kama hizo kulingana na mapenzi yake ya kimungu na kwenye wakati wake uliochaguliwa. —3/15, ukurasa 7.
◻ Ni tukio gani la maana lililotukia katika mwaka wa 20 wa utawala wa Mfalme Artazakse (455 K.W.K.)?
Nehemia alipewa ruhusa arudi akajenge upya Yerusalemu na kuta zao. Amri hii ilikuwa ndio mwanzo wa yale “majuma sabini’’ ya miaka ya unabii wa Danieli, yakielekeza kwenye mtokeo wa Yesu akiwa “Mesiya Kiongozi” katika wakati barabara, katika 29 W.K. (Danieli 9:24, 25; Nehemia 1:1; 2:1-9, NW) —3/15, kurasa 28,29.
◻ Ni njia gani iliyo bora zaidi ya kushughulikia matatizo ya kijamaa?
Ni kwa upendo, kwa maana Biblia inashauri hivi, “Acheni mambo yenu yote yatukie kwa upendo.” Pia, “Upendo hufunika wingi wa dhambi.”(1 Wakorintho 16:14; 1 Petro 4:8, NW) Huu unapasa kuwa upendo wenye kina kirefu ambao una nia ya kuachilia makosa ya kutokamilika ya washiriki wengine wa jamaa ambayo kama sivyo yanaudhi mtu na kukwaruza hisia zake.—4/1, kurasa 6, 7.