Je! Wakumbuka?
Je! wewe umefikiria kwa uangalifu matoleo ya karibuni ya Mnara wa Mlinzi? Ikiwa ndivyo, labda utalipata kuwa jambo lenye kupendeza kukumbuka yafuatayo:
▫ Ni nini ile “ishara inayomaanisha wema” ambayo Yehova huwafanyia wafuasi wa nyayo za Yesu? (Zaburi 86:17)
Ilikuwa ile “shangwe ya roho takatifu” iliyowaimarisha Wakristo wa mapema kuvumilia namna-namna za mnyanyaso zilizowapata. (1 Wathesalonike 1:6) Ni vivyo hivyo leo, na Yehova, aliye Mpaji wa “kila zawadi njema na kila upaji mkamilifu,” hupendezwa kutoa “roho takatifu kwa wale wanaomwomba.” (Yakobo 1:17; Luka 11:13, NW) Kwa hiyo ni shangwe ya roho takatifu inayowafanyia wafuasi wa Yesu “ishara inayomaanisha wema.”—12/15, kurasa 18-19.
▫ Kwa nini ni muhimu kwetu kukubali maoni ya Mungu juu ya kusema uwongo?
Zaburi 5:6 husema kwamba “[a]tawaharibu wasemao uongo.” Ufunuo 21:8 huendelea kusema kwamba mwisho wa waongo ni “kifo cha pili.” (NW) Kwa hiyo, kukubali maoni ya Mungu juu ya kusema uwongo kunatupatia sababu yenye nguvu kusema kweli na kupokea zawadi yake ya uhai.—12/15, ukurasa 23.
▫ Namna ya ibada ya Kisamaria ilitia ndani nini? (Yohana 4:20)
Wasamaria, katika ibada yao yenye kuchanganyika, walikubali Maandiko kuwa tu vile vitabu vitano vya kwanza vya Musa, Pentateuki. Yapata karne ya nne K.W.K. walijenga hekalu juu ya Mlima Gerizimu, kwa kushindana na hekalu la Mungu katika Yerusalemu. Ingawa hekalu la Wasamaria liliharibiwa, hadi leo, wao huwa na mwadhimisho wa Sikukuu ya Kupitwa ya kila mwaka juu ya Gerizimu.—1/1, ukurasa 25.
▫ Je! Wakristo wanahitajiwa kuendeleza hatua dhidi ya uchafuzi au za usafishaji?
Alipokuwa duniani, Yesu hakujaribu kusuluhisha matatizo yote ya kijamii ya siku yake. Wakati Yehova kupitia Ufalme wake wa Kimesiya anapotekeleza kanuni zake zenye uadilifu kwa kiwango cha duniani pote, matatizo ya kimazingira yatasuluhishwa kwa njia yenye kudumu. Kwa hiyo, Mashahidi wa Yehova wana maoni yenye usawaziko. Upendo wa jirani huwasukuma kuonyesha staha kwa ajili ya mali ya wengine, lakini kwa kufaa wao huweka kazi ya kuhubiri ujumbe wa Ufalme kwanza. (Mathayo 6:33)—1/1, ukurasa 31.
▫ Yesu alitumikia akiwa mchukuaji nuru katika njia zipi? (Yohana 8:12)
Yesu alijitoa mwenyewe kuhubiri habari njema za Ufalme wa Mungu. (Luka 4:43; Yohana 18:37) Pia alifunua uwongo mbalimbali wa kidini na hivyo kuandaa uhuru wa kiroho kwa wale waliofungwa katika utumwa wa kidini. (Mathayo 15:3-9) Kwa kutokeza, alithibitika kuwa nuru ya ulimwengu kwa kutoa uhai wake mkamilifu wa kibinadamu kuwa fidia. (Mathayo 20:28; Yohana 3:16)—1/15, kurasa 10-11.
▫ Ni nini baadhi ya sababu kwa nini tunawiwa na Yehova Mungu ujitiisho?
Yehova ni Mwenye Enzi Kuu ya Ulimwengu Wote Mzima, na kwa sababu hiyo tunawiwa naye ujitiisho wetu. Pia, kwa kuwa Yehova ni Mweza Yote, hakuna awezaye kumpinga kwa mafanikio, kwa hiyo hatuwezi kupuuza ujitiisho wetu kwake. Viumbe vyote vyenye akili viliumbwa kutumikia kusudi la Mfanyi wavyo, na hilo laweka wote chini ya wajibu wa kujitiisha wenyewe kwa Mungu katika mambo yote.—2/1, kurasa 10-11.
▫ Ni nini kilichomsaidia Yusufu akinze kufanya uasherati pamoja na mke wa Potifa?
Yusufu alikuwa na kani yenye nguvu iliyotendesha akili yake. Alifikiria sana uhusiano wake pamoja na Yehova na alijua kwamba tendo la uasherati lingalikuwa dhambi si dhidi ya mume wa mwanamke huyo tu, bali kwa umaana zaidi, dhidi ya Mungu.—2/15, ukurasa 21.
▫ Yesu alimaanisha nini aliposema: “Mimi ndimi . . . kweli”? (Yohana 14:6)
Yesu hakuisema na kuifundisha kweli tu; aliishi kulingana nayo na kuifananisha. Hivyo, Ukristo si wazo tu; ni njia ya maisha.—3/1, ukurasa 15.
▫ Zaburi 51 ina somo gani linalofariji?
Zaburi hiyo inatusaidia kung’amua kwamba tukijikwaa katika dhambi lakini tuwe wenye kutubu kwelikweli, Baba yetu wa kimbingu mwenye upendo atasikia kilio chetu cha kupata rehema na atatuokoa kutoka katika hali ya kukata tamaa. Hata hivyo, tunapaswa hasa kuhangaika juu ya suto lolote ambalo limeletwa juu ya jina la Yehova.—3/15, ukurasa 18.
▫ Ni nini kinachofananishwa na ubatizo wa maji?
Ubatizo ni ufananisho wa nje wa wakfu wa mtu kwa Yehova Mungu. Kutumbukizwa chini ya maji huonyesha kwamba wale wanaobatizwa wanakufa kwa habari ya mwendo wa maisha wa kujifikiria wao wenyewe tu. Kuinuliwa kutoka katika majini hufananisha kwamba sasa wao ni hai ili kufanya mapenzi ya Mungu, kuyaweka kwanza maishani mwao. (Mathayo 16:24)—4/1, kurasa 5-6.