Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 10/06 kur. 3-6
  • Ratiba Ya Shule Ya Huduma Ya Kitheokrasi Ya 2007

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ratiba Ya Shule Ya Huduma Ya Kitheokrasi Ya 2007
  • Huduma ya Ufalme—2006
  • Vichwa vidogo
  • Maagizo
  • RATIBA
Huduma ya Ufalme—2006
km 10/06 kur. 3-6

Ratiba Ya Shule Ya Huduma Ya Kitheokrasi Ya 2007

Maagizo

Katika mwaka wa 2007, Shule ya Huduma ya Kitheokrasi itaongozwa kwa kutegemea utaratibu ufuatao.

VICHAPO VITAKAVYOTUMIWA: Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya [bi12], Mnara wa Mlinzi [w], Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi [be], “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa” (Toleo la 1992) [si], na Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko (Toleo la 2004) [rs].

Shule inapaswa kuanza KWA WAKATI kwa wimbo, sala, na utangulizi wa kuwakaribisha wasikilizaji. Kisha fuateni utaratibu ufuatao. Baada ya kila hotuba mwangalizi wa shule atamkaribisha msemaji anayefuata.

SIFA YA USEMI: Dakika 5. Mwangalizi wa shule, mshauri-msaidizi, au mzee mwingine anayestahili atazungumzia sifa moja ya usemi katika kitabu cha Shule ya Huduma. (Katika makutaniko yenye wazee wachache, watumishi wa huduma wanaostahili wanaweza kutumiwa.)

HOTUBA NA. 1: Dakika 10. Hotuba hii inapaswa kutolewa na mzee au mtumishi wa huduma anayestahili, nayo itategemea Mnara wa Mlinzi, Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi, au “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa.” Hotuba hii ya maagizo itolewe kwa dakika kumi. Lengo la kutoa hotuba hii si kuzungumzia tu habari, bali ni kuonyesha jinsi habari hiyo inavyoweza kutumiwa maishani, na kukazia mambo ambayo yatanufaisha kutaniko. Kichwa kilichoonyeshwa ndicho kinachopaswa kutumiwa. Inatarajiwa kwamba ndugu wanaopewa hotuba hii watazingatia wakati ulioonyeshwa. Ndugu anaweza kushauriwa faraghani inapohitajika.

MAMBO MAKUU YA USOMAJI WA BIBLIA: Dakika 10. Mzee, au mtumishi wa huduma, anayestahili, atumie dakika tano za kwanza kuonyesha jinsi habari hiyo inavyohusu hali zenu. Anaweza kuzungumzia sehemu yoyote ya usomaji wa Biblia wa juma hilo. Hapaswi kutoa tu muhtasari wa usomaji wa Biblia. Lengo kuu ni kuwasaidia wasikilizaji waelewe ni kwa nini habari hiyo ni yenye manufaa na jinsi inavyowanufaisha. Msemaji anapaswa kuwa mwangalifu asipite zile dakika zake tano za kwanza. Anapaswa kuhakikisha kwamba anawaachia wasikilizaji dakika tano ili watoe maelezo yao. Wasikilizaji wanapaswa kuombwa watoe maelezo mafupi (yasiyozidi sekunde 30) kuhusu mambo yaliyowapendeza katika usomaji wa Biblia na manufaa yake. Kisha mwangalizi wa shule atawaruhusu wanafunzi watakaotoa hotuba katika shule ya pili au ya tatu waondoke.

HOTUBA NA. 2: Isizidi dakika 4. Hii ni hotuba ya usomaji inayopaswa kutolewa na ndugu. Mwanafunzi anapaswa kusoma habari hiyo bila kutoa utangulizi wala umalizio. Mwangalizi wa shule atajitahidi hasa kuwasaidia wanafunzi wasome kwa njia inayoeleweka, wawe na ufasaha, wakazie maana kwa njia inayofaa, wawe na ubadilifu wa sauti, watue kwa njia inayofaa, na wasome kwa njia ya maongezi ya kawaida.

HOTUBA NA. 3: Dakika 5. Hotuba hii inapaswa kutolewa na akina dada. Wanafunzi wanaopewa mgawo huu watapewa au watajichagulia kikao katika orodha ya vikao iliyo kwenye ukurasa wa 82 wa kitabu cha Shule ya Huduma. Mwanafunzi anapaswa kutumia kichwa kilichoonyeshwa na kuonyesha jinsi habari hiyo inavyoweza kutumiwa katika utumishi wa shambani kwenye eneo lenu. Ikiwa chanzo cha habari hakijaonyeshwa, itambidi mwanafunzi afanye utafiti kuhusu habari hiyo katika vichapo vyetu. Wanafunzi wapya wapewe hotuba zilizo na marejeo. Mwangalizi wa shule ataangalia hasa jinsi mwanafunzi anavyoeleza habari hiyo na jinsi anavyomsaidia mwenye nyumba kuelewa maana ya Maandiko na mambo makuu. Mwangalizi wa shule atampa msaidizi mmoja.

HOTUBA NA. 4: Dakika 5. Mwanafunzi anapaswa kuzungumzia kichwa kilichoonyeshwa. Ikiwa chanzo cha habari hakijaonyeshwa, itambidi mwanafunzi afanye utafiti kuhusu habari hiyo katika vichapo vyetu. Ndugu anapopewa hotuba hii, ataitoa kama hotuba kwa wasikilizaji kwenye Jumba la Ufalme. Dada anapopewa hotuba hii, ataitoa jinsi Hotuba Na. 3 inavyotolewa. Mwangalizi wa shule anaweza kumpa ndugu Hotuba Na. 4 wakati wowote anapoona inafaa kufanya hivyo. Hakikisha kwamba akina ndugu tu ndio wanaopewa hotuba zenye vichwa vilivyo na alama ya nyota.

SHAURI: Dakika 1. Mwangalizi wa shule hatatangaza mapema sifa ya usemi ambayo mwanafunzi anafanyia kazi. Baada ya kila Hotuba Na. 2, Na. 3, na Na. 4, mwangalizi wa shule atatoa maelezo yanayojenga kuhusu jambo linalostahili kusifiwa katika hotuba hiyo. Lengo lake si kutoa pongezi tu, bali ni kuonyesha sababu iliyofanya jambo fulani liwe zuri katika hotuba. Kulingana na uhitaji wa kila mwanafunzi, mashauri mengine yanaweza kutolewa faraghani baada ya mkutano au katika pindi tofauti, ili kumsaidia mwanafunzi afanye maendeleo.

WAKATI: Hotuba wala maelezo ya mshauri hayapaswi kamwe kupita wakati. Wanafunzi wanaotoa Hotuba Na. 2 hadi 4, wanapaswa kukatizwa kwa busara muda wao unapokwisha. Ndugu wanaotoa sifa ya usemi, Hotuba Na. 1, au mambo makuu ya usomaji wa Biblia wakipita wakati, wanapaswa kushauriwa faraghani. Wote wanapaswa kufuata wakati. Programu nzima: Dakika 45, bila kutia ndani wimbo na sala.

FOMU YA MASHAURI: Imo katika kitabu cha shule.

MSHAURI MSAIDIZI: Mbali na mwangalizi wa shule, baraza la wazee linaweza kuchagua mzee mwenye uwezo, ikiwa yupo, awe mshauri msaidizi. Ikiwa kuna wazee kadhaa kutanikoni, kila mwaka, mzee tofauti anayestahili anaweza kupewa mgawo huo. Mshauri msaidizi ana daraka la kuwashauri faraghani akina ndugu wanaotoa Hotuba Na. 1 na mambo makuu ya usomaji wa Biblia, inapohitajiwa. Hahitaji kuwashauri wazee wenzake au watumishi wa huduma kila mara wanapotoa hotuba hizo.

PITIO LA MASWALI NA MAJIBU: Dakika 30. Baada ya kila miezi miwili, mwangalizi wa shule ataongoza pitio la maswali na majibu. Sehemu hiyo itafanywa baada ya sifa ya usemi na mambo makuu ya usomaji wa Biblia kama inavyoonyeshwa juu. Pitio hilo litahusisha habari zilizozungumziwa katika shule miezi miwili iliyotangulia, kutia ndani juma la pitio. Ikiwa kutaniko lenu lina kusanyiko la mzunguko katika juma la pitio, mtafanya pitio (na pia sehemu zile nyingine za juma hilo) juma litakalofuata, nazo sehemu zilizo katika ratiba ya juma hilo linalofuata zitatolewa katika kusanyiko hilo la mzunguko. Ikiwa mwangalizi wa mzunguko anatembelea kutaniko lenu katika juma la pitio, wimbo, sifa ya usemi, na mambo makuu ya usomaji wa Biblia zinapaswa kutolewa kama ilivyoonyeshwa katika ratiba. Hotuba ya maagizo (ambayo itatolewa baada ya sifa ya usemi) inapaswa kuwa ile ya juma litakalofuata. Shule ya Huduma ya Kitheokrasi ya juma litakalofuata itaanza na sifa ya usemi kisha mambo makuu ya usomaji wa Biblia kama ilivyoonyeshwa katika ratiba, na hatimaye pitio la maswali na majibu.

RATIBA

Jan. 1 Usomaji wa Biblia: Isaya 24-28 Wimbo 33

Sifa ya Usemi: Matumizi Yanayofaa ya Habari (be uku. 158 ¶1-3)

Na. 1: Kutayarisha Migawo ya Shule (be uku. 43 ¶1–uku. 44 ¶3)

Na. 2: Isaya 26:1-18

Na. 3: Kwa Nini Ni Kosa Kutoa Mimba? (rs uku. 131-133 ¶3)

Na. 4: Tunawezaje ‘Kumvaa Bwana Yesu Kristo’? (Rom. 13:14)

Jan. 8 Usomaji wa Biblia: Isaya 29-33 Wimbo 42

Sifa ya Usemi: Kuwasaidia Wengine Kuona Faida ya Ujumbe Wetu (be uku. 159 ¶1-4)

Na. 1: Kutayarisha Ukifikiria Kichwa Kikuu na Kikao (be uku. 44 ¶4–uku. 46 ¶2)

Na. 2: Isaya 30:1-14

Na. 3: a Kumjibu Mtu Anayesema: ‘Nina Haki ya Kuamua Mambo Yanayohusu Mwili Wangu Mwenyewe’ (rs uku. 133 ¶4)

Na. 4: Jinsi Tunavyojua Kwamba Yehova Mungu Anawapenda Watoto

Jan. 15 Usomaji wa Biblia: Isaya 34-37 Wimbo 222

Sifa ya Usemi: Kutumia Maneno Yanayofaa (be uku. 160 ¶1-3)

Na. 1: Sitawisha Maoni Kama ya Yesu Kuhusu Yaliyo Sawa na Yaliyo Makosa (w05 1/1 uku. 9-10 ¶11-15)

Na. 2: Isaya 34:1-15

Na. 3: Jinsi ya Kusitawisha Upendo wa Kweli

Na. 4: Adamu na Hawa—Je, Walikuwa Watu Halisi? (rs uku. 25-26)

Jan. 22 Usomaji wa Biblia: Isaya 38-42 Wimbo 61

Sifa ya Usemi: Lugha Inayoeleweka kwa Urahisi (be uku. 161 ¶1-4)

Na. 1: Usivunjwe Moyo na Upinzani (w05 1/1 uku. 15 ¶16-18)

Na. 2: Isaya 38:9-22

Na. 3: b Kumjibu Mtu Anayesema: ‘Dhambi ya Adamu Ilikuwa Mapenzi ya Mungu’ (rs uku. 27 ¶1-2)

Na. 4: Sababu za Kuepuka Kufikiri Kwamba Wengine Wana Nia Mbaya

Jan. 29 Usomaji wa Biblia: Isaya 43-46 Wimbo 113

Sifa ya Usemi: Kutumia Semi Tofauti-Tofauti na Sahihi (be uku. 161 ¶5–uku. 162 ¶4)

Na. 1: Kwa Nini Tunakubali Hukumu za Yehova? (w05 2/1 uku. 23-24 ¶4-9)

Na. 2: Isaya 45:1-14

Na. 3: Kwa Nini Ni Ubatili Kuabudu Mababu? (rs uku. 89 ¶1–uku. 90 ¶3)

Na. 4: c Sababu Inayowafanya Wakristo Waepuke Kujilinganisha kwa Mashindano

Feb. 5 Usomaji wa Biblia: Isaya 47-51 Wimbo 79

Sifa ya Usemi: Maneno Yanayoonyesha Mkazo, Hisia, na Yanayovutia (be uku. 163 ¶1–uku. 164 ¶2)

Na. 1: Neno la Yehova Hutusafisha na Kutusaidia Kuwa Waaminifu (w05 4/15 uku. 11-12 ¶5-11)

Na. 2: Isaya 50:1-11

Na. 3: Sababu Zinazofanya Yehova Mungu Achukie Ibada ya Mababu (rs uku. 90 ¶4–uku. 91 ¶2)

Na. 4: Je, Biblia Inapinga Zoea la Kutoa Zawadi?

Feb. 12 Usomaji wa Biblia: Isaya 52-57 Wimbo 139

Sifa ya Usemi: Usemi Unaopatana na Kanuni za Sarufi (be uku. 164 ¶3–uku. 165 ¶1)

Na. 1: Neno la Yehova Hutupa Ujasiri (w05 4/15 uku. 13 ¶12-14)

Na. 2: Isaya 55:1-13

Na. 3: Kuishi Maisha ya Kujidhabihu Kuna Faida

Na. 4: Wapinga-Kristo Ni Nani? (rs uku. 209-210)

Feb. 19 Usomaji wa Biblia: Isaya 58-62 Wimbo 189

Sifa ya Usemi: Kutumia Muhtasari (be uku. 166 ¶1–uku. 167 ¶2)

Na. 1: Isaya—Kwa Nini Ni Chenye Mafaa (si uku. 123 ¶34-39)

Na. 2: Isaya 60:1-14

Na. 3: Kwa Nini Ni Jambo Linalofaa Kuwa Mtumwa wa Mungu?

Na. 4: d Kuwatambulisha Waasi-Imani (rs uku. 304 ¶1–uku.306 ¶1)

Feb. 26 Usomaji wa Biblia: Isaya 63-66 Wimbo 141

Sifa ya Usemi: Kupanga Mambo Unayotaka Kuzungumzia (be uku. 167 ¶3–uku. 168 ¶2)

Pitio la Maswali na Majibu

Mac. 5 Usomaji wa Biblia: Yeremia 1-4 Wimbo 70

Sifa ya Usemi: Muhtasari Wako Uwe Rahisi (be uku. 168 ¶3–uku. 169 ¶6)

Na. 1: Utangulizi wa Yeremia (si uku. 124 ¶1-5)

Na. 2: Yeremia 3:1-13

Na. 3: Furaha ya Kweli Inategemea Nini?

Na. 4: e Tunapaswa Kuwa na Mtazamo Gani Kuelekea Waasi-Imani? (rs uku. 306 ¶2–uku. 307 ¶2)

Mac. 12 Usomaji wa Biblia: Yeremia 5-7 Wimbo 159

Sifa ya Usemi: Habari Inayofuatana Vizuri (be uku. 170 ¶1–uku. 171 ¶2)

Na. 1: Kutayarisha Hotuba kwa Ajili ya Kutaniko (be uku. 47 ¶1–uku. 49 ¶1)

Na. 2: Yeremia 5:1-14

Na. 3: Kristo Hakujenga Kanisa Juu ya Petro (rs uku. 360 ¶2–uku. 362 ¶3)

Na. 4: Kutumia Jambo Tunalojifunza Kwenye Kutoka 14:11 Katika Siku Zetu

Mac. 19 Usomaji wa Biblia: Yeremia 8-11 Wimbo 182

Sifa ya Usemi: Kutoa Habari kwa Njia Inayofuatana Vizuri (be uku. 171 ¶3–uku. 172 ¶6)

Na. 1: Kutayarisha Hotuba kwa Ajili ya Mkutano wa Utumishi na Hotuba Nyingine (be uku. 49 ¶2–uku. 51 ¶1)

Na. 2: Yeremia 10:1-16

Na. 3: Tunajuaje Kwamba Abrahamu, Ayubu, na Danieli Walikuwa na Imani Katika Ufufuo?

Na. 4: Funguo Ambazo Petro Alitumia Zilikuwa Nini? (rs uku. 362 ¶4–uku. 364 ¶4)

Mac. 26 Usomaji wa Biblia: Yeremia 12-16 Wimbo 205

Sifa ya Usemi: Kutumia Habari Zinazohusika Pekee (be uku. 173 ¶1-4)

Na. 1: Fidia Hutukuza Uadilifu wa Mungu (w05 11/1 uku. 13-14)

Na. 2: Yeremia 12:1-13

Na. 3: “Warithi wa Upapa” Si Wakristo wa Kweli (rs uku. 364 ¶1–uku. 367 ¶3)

Na. 4: Mkristo Anapaswa Kujivunia Nini?

Apr. 2 Usomaji wa Biblia: Yeremia 17-21 Wimbo 30

Sifa ya Usemi: Kutoa Hotuba Bila Kutazama Sana Maandishi (be uku. 174 ¶1–uku. 175 ¶4)

Na. 1: Kutayarisha Hotuba za Watu Wote (be uku. 52 ¶1–uku. 54 ¶1)

Na. 2: Yeremia 20:1-13

Na. 3: Har–Magedoni Itapiganwa Wapi? (rs uku. 84 ¶1–uku. 85 ¶8)

Na. 4: f Tunapaswa Kuonaje Shauri?

Apr. 9 Usomaji wa Biblia: Yeremia 22-24 Wimbo 184

Sifa ya Usemi: Kuepuka Mitego ya Kutoa Hotuba Bila Kutazama Sana Maandishi (be uku. 175 ¶5–uku. 177 ¶1)

Na. 1: Maamuzi ya Msemaji (be uku. 54 ¶2-4; uku. 55, sanduku)

Na. 2: Yeremia 23:1-14

Na. 3: Kwa Nini Kushiriki Katika Huduma Huleta Shangwe?

Na. 4: Ni Nini au Ni Nani Watakaoharibiwa Kwenye Har–Magedoni? (rs uku. 86 ¶1–6)

Apr. 16 Usomaji wa Biblia: Yeremia 25-28 Wimbo 27

Sifa ya Usemi: Wengine Wanapotaka Majibu (be uku. 177 ¶2–uku. 178 ¶2)

Na. 1: Sitawisha Ustadi wa Kufundisha (be uku. 56 ¶1–uku. 57 ¶2)

Na. 2: Yeremia 26:1-15

Na. 3: Ni Nani Watakaookoka Har–Magedoni? (rs uku. 86 ¶7–uku. 87 ¶5)

Na. 4: Udongo Ulilaaniwa Katika Maana Gani? (Mwa. 3:17)

Apr. 23 Usomaji wa Biblia: Yeremia 29-31 Wimbo 148

Sifa ya Usemi: Kutoa Hotuba kwa Njia ya Maongezi (be uku. 179-80)

Na. 1: ‘Pambanua Mambo’ (be uku. 57 ¶3–uku. 58 ¶2)

Na. 2: Yeremia 31:1-14

Na. 3: Kwa Nini Ukuu wa Yehova Hauna Mipaka?

Na. 4: Har–Magedoni—Haionyeshi Mungu Hana Upendo (rs uku. 87 ¶6–uku. 88 ¶1)

Apr. 30 Usomaji wa Biblia: Yeremia 32-34 Wimbo 100

Sifa ya Usemi: Ubora wa Sauti (be uku. 181 ¶1-4)

Pitio la Maswali na Majibu

Mei 7 Usomaji wa Biblia: Yeremia 35-38 Wimbo 165

Sifa ya Usemi: Kupumua Vizuri (be uku. 181 ¶5–uku. 184 ¶1; uku. 182, sanduku)

Na. 1: Watie Moyo Wasikilizaji Wafikiri (be uku. 58 ¶3–uku. 59 ¶3)

Na. 2: Yeremia 36:1-13

Na. 3: Haiwezekani Kutounga Mkono Upande Wowote Katika Har–Magedoni (rs uku. 88 ¶2-5)

Na. 4: Wakristo Wanaweza Kufanya Nini Wanapokuwa na Mashaka?

Mei 14 Usomaji wa Biblia: Yeremia 39-43 Wimbo 56

Sifa ya Usemi: Kutuliza Mkazo wa Misuli (be uku. 184 ¶2–uku. 185 ¶2; uku. 184, sanduku)

Na. 1: Onyesha Jinsi Habari Inavyotumika, Weka Mfano Mzuri (be uku. 60 ¶1–uku. 61 ¶3)

Na. 2: Yeremia 39:1-14

Na. 3: Ni Nani Anayeyachochea Mataifa Kwenye Hali ya Har–Magedoni? (rs uku. 88 ¶6-7)

Na. 4: g Kwa Nini Wakristo Hujitahidi Kuwa na Uchumba Safi?

Mei 21 Usomaji wa Biblia: Yeremia 44-48 Wimbo 122

Sifa ya Usemi: Kupendezwa na Wengine (be uku. 186 ¶1-4)

Na. 1: Jinsi ya Kuboresha Stadi za Mazungumzo (be uku. 62 ¶1–uku. 64 ¶1)

Na. 2: Yeremia 46:1-17

Na. 3: Kujidanganya Kunamaanisha Nini, Nasi Tunawezaje Kujihadhari Tusiathiriwe?

Na. 4: Kumtambulisha Babiloni Mkubwa (rs uku. 28 ¶1-2)

Mei 28 Usomaji wa Biblia: Yeremia 49-50 Wimbo 95

Sifa ya Usemi: Kusikiliza kwa Makini (be uku. 187 ¶1-5)

Na. 1: Jinsi ya Kuendeleza Mazungumzo (be uku. 64 ¶2–uku. 65 ¶4)

Na. 2: Yeremia 49:14-27

Na. 3: Babiloni la Kale Lilijulikana kwa Sababu Gani? (rs uku. 28 ¶3–uku. 30 ¶3)

Na. 4: Kwa Nini Wazazi Wanapaswa Kuwasomea Watoto Wao?

Juni 4 Usomaji wa Biblia: Yeremia 51-52 Wimbo 166

Sifa ya Usemi: Kuwasaidia Wengine Wafanye Maendeleo (be uku. 187 ¶6–uku. 188 ¶3)

Na. 1: Yeremia—Kwa Nini Ni Chenye Mafaa (si uku. 129 ¶36-39)

Na. 2: Yeremia 52:1-16

Na. 3: Ni Upumbavu Kujitegemea Badala ya Kumtegemea Mungu

Na. 4: Kwa Nini Dini Zinazodai Kuwa za Kikristo Ni Sehemu ya Babiloni Mkubwa? (rs uku. 30 ¶4–uku. 31 ¶3)

Juni 11 Usomaji wa Biblia: Maombolezo 1-2 Wimbo 129

Sifa ya Usemi: Kutoa Msaada Unaofaa (be uku. 188 ¶4–uku. 189 ¶4)

Na. 1: Utangulizi wa Maombolezo (si uku. 130-131 ¶1-7)

Na. 2: Maombolezo 2:1-10

Na. 3: Kwa Nini Ni Muhimu Kutoka Katika Babiloni Mkubwa Haraka? (rs uku. 31 ¶4–uku. 32 ¶5)

Na. 4: Kwa Nini Fadhili ya Kweli si Udhaifu?

Juni 18 Usomaji wa Biblia: Maombolezo 3-5 Wimbo 140

Sifa ya Usemi: Kuwaheshimu Wengine (be uku. 190 ¶1-4)

Na. 1: Maombolezo—Kwa Nini Ni Chenye Mafaa (si uku. 132 ¶13-15)

Na. 2: Maombolezo 4:1-13

Na. 3: Kinachomaanishwa na Ubatizo, na Kwa Nini Wanaoamini Hubatizwa (rs p. 307 ¶3-6)

Na. 4: h Kwa Nini Wakristo wa Kweli Hawajihusishi Katika Siasa?

Juni 25 Usomaji wa Biblia: Ezekieli 1-5 Wimbo 1

Sifa ya Usemi: Salamu Zenye Heshima (be uku. 191 ¶1–uku. 192 ¶1)

Pitio la Maswali na Majibu

Julai 2 Usomaji wa Biblia: Ezekieli 6-10 Wimbo 26

Sifa ya Usemi: Kutoa Hotuba kwa Njia ya Heshima (be uku. 192 ¶2–uku. 193 ¶2)

Na. 1: Utangulizi wa Ezekieli (si uku. 132-133 ¶1-6)

Na. 2: Ezekieli 7:1-13

Na. 3: Kinachohitajika Ili Kumkaribia Yehova (Yak. 4:8)

Na. 4: Ubatizo wa Kikristo, Si kwa Kunyunyiza Maji, Wala kwa Watoto wa Wachanga (rs uku. 308 ¶1–uku. 308 ¶6)

Julai 9 Usomaji wa Biblia: Ezekieli 11-14 Wimbo 112

Sifa ya Usemi: Kuzungumza kwa Usadikisho (be uku. 194 ¶1–uku. 195 ¶2)

Na. 1: Usife Moyo Katika Kufanya Yaliyo Mema (w05 6/1 uku. 29-30)

Na. 2: Ezekieli 11:1-13

Na. 3: Je, Ubatizo wa Maji Husafisha Dhambi? (rs uku. 308 ¶7–uku. 309 ¶2)

Na. 4: Tunapaswa Kuelewaje Ufunuo 17:9-11?

Julai 16 Usomaji wa Biblia: Ezekieli 15-17 Wimbo 29

Sifa ya Usemi: Jinsi ya Kuonyesha Usadikisho (be uku. 195 ¶3–uku. 196 ¶4)

Na. 1: Kataa Mawazo Yasiyofaa! (w05 9/15 uku. 26-28)

Na. 2: Ezekieli 16:1-13

Na. 3: Kinachomaanishwa na Kuwa Mwerevu (Met. 13:16)

Na. 4: Ni Nani Wanaobatizwa kwa Roho Takatifu? (rs uku. 309 ¶3–uku. 310 ¶5)

Julai 23 Usomaji wa Biblia: Ezekieli 18-20 Wimbo 193

Sifa ya Usemi: Uwe Mwenye Busara Lakini Thabiti (be uku. 197 ¶1-3)

Na. 1: Kufahamu Maoni ya Anayeuliza Swali (be uku. 66 ¶1–uku. 68 ¶1)

Na. 2: Ezekieli 18:19-29

Na. 3: Ubatizo wa Moto Si Sawa na Ubatizo kwa Roho Takatifu (rs uku. 310 ¶6–uku. 311 ¶4)

Na. 4: Uthibitisho Kwamba Ufalme wa Mungu Ni Halisi

Julai 30 Usomaji wa Biblia: Ezekieli 21-23 Wimbo 35

Sifa ya Usemi: Kutumia Busara Unapohubiri (be uku. 197 ¶4–uku. 198 ¶5)

Na. 1: Jua Jinsi Unavyopaswa Kujibu (be uku. 68 ¶2–uku. 70 ¶3)

Na. 2: Ezekieli 23:1-17

Na. 3: Sababu za Kuichunguza Biblia (rs uku. 33 ¶1–uku. 34 ¶3)

Na. 4: Ni Maoni Gani Yanayofaa Kuhusu Umashuhuri?

Ago. 6 Usomaji wa Biblia: Ezekieli 24-27 Wimbo 37

Sifa ya Usemi: Kusema Maneno Yanayofaa Wakati Unaofaa (be uku. 199 ¶1-4)

Na. 1: Kuandika Barua (be uku. 71-73)

Na. 2: Ezekieli 24:1-14

Na. 3: Musa Alikuwa Mfano Mzuri kwa Wakristo Katika Njia Gani?

Na. 4: Uthibitisho Kutoka Kitabu cha Isaya na Yeremia Kwamba Biblia Iliongozwa na Roho ya Mungu (rs uku. 34 ¶4–uku. 35 ¶3)

Ago. 13 Usomaji wa Biblia: Ezekieli 28-31 Wimbo 123

Sifa ya Usemi: Kutumia Busara Katika Familia na kwa Wengine (be uku. 200 ¶1-4)

Na. 1: Uwe Mwenye Maendeleo (be uku. 74 ¶1–uku. 75 ¶3)

Na. 2: Ezekieli 28:1-16

Na. 3: Kutimia kwa Unabii wa Yesu Kunathibitisha Biblia Iliongozwa na Roho ya Mungu (rs uku. 35 ¶4–uku. 36 ¶1)

Na. 4: Ni Nini Kinachomaanishwa na “Chuki” Katika Maandiko?

Ago. 20 Usomaji wa Biblia: Ezekieli 32-34 Wimbo 215

Sifa ya Usemi: Uwe Mwenye Kujenga na Kutia Moyo (be uku. 202 ¶1–uku. 203 ¶2)

Na. 1: Tumia Zawadi Yako (be uku. 75 ¶4–uku. 77 ¶2)

Na. 2: Ezekieli 34:1-14

Na. 3: Roho ya Mungu Inatusaidiaje?

Na. 4: Biblia Ni Sahihi Kisayansi (rs uku. 36 ¶2–uku. 38 ¶3)

Ago. 27 Usomaji wa Biblia: Ezekieli 35-38 Wimbo 94

Sifa ya Usemi: Kuwa Mwenye Kutia Moyo (be uku. 203 ¶3–uku. 204 ¶1)

Pitio la Maswali na Majibu

Sept. 3 Usomaji wa Biblia: Ezekieli 39-41 Wimbo 194

Sifa ya Usemi: Unapozungumza na Waamini Wenzako (be uku. 204 ¶2–uku. 205 ¶4)

Na. 1: Kwa Nini Ulipende Neno la Mungu? (w05 4/15 uku. 15-16 ¶3-6)

Na. 2: Ezekieli 40:1-15

Na. 3: Je, Wanadamu Wanaweza Kumfurahisha Mungu?

Na. 4: i Kujibu Upinzani Kuhusu Biblia (rs uku. 38 ¶4–uku. 42 ¶2)

Sept. 10 Usomaji wa Biblia: Ezekieli 42-45 Wimbo 77

Sifa ya Usemi: Kurudia Ili Kukazia Mambo (be uku. 206 ¶1-4)

Na. 1: Uzee Unapokuwa “Taji la Uzuri” (w05 1/15 uku. 8-9)

Na. 2: Ezekieli 43:1-12

Na. 3: Kwa Nini Wakristo Hawasherehekei Sikukuu za Kuzaliwa? (rs uku. 282 ¶5–uku. 284 ¶3)

Na. 4: j Tunaweza Kutambuaje “Sauti ya Wageni”? (Yoh. 10:5)

Sept. 17 Usomaji wa Biblia: Ezekieli 46-48 Wimbo 164

Sifa ya Usemi: Kurudia Katika Huduma ya Shambani na Katika Hotuba (be uku. 207 ¶1–uku. 208 ¶4)

Na. 1: Ezekieli—Kwa Nini Ni Chenye Mafaa (si uku. 137 ¶29-33)

Na. 2: Ezekieli 47:1-14

Na. 3: Kwa Nini Wakristo Hujiepusha na Damu? (rs uku. 42 ¶3–uku. 44 ¶2)

Na. 4: k Kwa Nini Urithi wa Kiroho Ndiyo Zawadi Bora Ambayo Wazazi Wanaweza Kuwapa Watoto Wao?

Sept. 24 Usomaji wa Biblia: Danieli 1-3 Wimbo 179

Sifa ya Usemi: Kufafanua Kichwa Kikuu (be uku. 209 ¶1-3)

Na. 1: Utangulizi wa Danieli (si uku. 138-139 ¶1-6)

Na. 2: Danieli 2:1-16

Na. 3: Kwa Nini Namba 144,000 Ni Halisi? (Ufu. 7:4)

Na. 4: Kwa Nini Wakristo wa Kweli Hawakubali Kutiwa Damu Mishipani? (rs uku. 44 ¶3–uku. 45 ¶3)

Okt. 1 Usomaji wa Biblia: Danieli 4-6 Wimbo 14

Sifa ya Usemi: Kutumia Kichwa Kikuu Kinachofaa (be uku. 210 ¶1–uku. 211 ¶1; uku. 211, sanduku)

Na. 1: Ni Wakati Gani Unapokuwa na Haki ya Kuudhika? (w05 8/1 uku. 13-15)

Na. 2: Danieli 4:1-17

Na. 3: Tunaweza Kuigaje Sifa Nzuri za Mefiboshethi?

Na. 4: l Kujibu Madai Kuhusu Kutiwa Damu Mishipani (rs uku. 46 ¶1–uku. 48 ¶1)

Okt. 8 Usomaji wa Biblia: Danieli 7-9 Wimbo 34

Sifa ya Usemi: Kukazia Mambo Makuu (be uku. 212 ¶1–uku. 213 ¶1)

Na. 1: Acha “Neno” la Yehova Likulinde (w05 9/1 uku. 28-31)

Na. 2: Danieli 7:1-12

Na. 3: Inamaanisha Nini Kuzaliwa Mara ya Pili? (rs uku. 145 ¶2–uku. 146 ¶4)

Na. 4: Ni Shangwe Gani za Pekee Hupatikana kwa Kushiriki kwa Ukawaida Katika Huduma ya Shambani?

Okt. 15 Usomaji wa Biblia: Danieli 10-12 Wimbo 210

Sifa ya Usemi: Usitumie Mambo Makuu Mengi Mno (be uku. 213 ¶2–uku. 214 ¶5)

Na. 1: Danieli—Kwa Nini Ni Chenye Mafaa (si uku. 141-142 ¶19-23)

Na. 2: Danieli 11:1-14

Na. 3: Jinsi Unyenyekevu Unavyoweza Kutusaidia Kukabiliana na Kutokuelewana

Na. 4: Kuokolewa Hakutegemei Kuzaliwa Mara ya Pili (rs uku. 146 ¶5–uku. 147 ¶5)

Okt. 22 Usomaji wa Biblia: Hosea 1-7 Wimbo 66

Sifa ya Usemi: Utangulizi Unaoamsha Upendezi (be uku. 215 ¶1–uku. 216 ¶5)

Na. 1: Utangulizi wa Hosea na Kwa Nini Ni Chenye Mafaa (si uku. 143-145 ¶1-8, 14-17)

Na. 2: Hosea 5:1-15

Na. 3: a Kujibu Maoni Kuhusu Kuzaliwa Mara ya Pili (rs uku. 148 ¶1-5)

Na. 4: Njia Ambazo Wakristo wa Kweli Huonyesha Subira

Okt. 29 Usomaji wa Biblia: Hosea 8-14 Wimbo 59

Sifa ya Usemi: Kuvuta Usikivu wa Watu Katika Utumishi wa Shambani (be uku. 217 ¶1-4)

Pitio la Maswali na Majibu

Nov. 5 Usomaji wa Biblia: Yoeli 1-3 Wimbo 166

Sifa ya Usemi: Kutaja Kihususa Habari Unayozungumzia Katika Utangulizi (be uku. 217 ¶5–uku. 219 ¶2)

Na. 1: Utangulizi wa Yoeli na Kwa Nini Ni Chenye Mafaa (si uku. 146-148 ¶1-5, 12-14)

Na. 2: Yoeli 2:1-14

Na. 3: Kinachomaanishwa na Kuwa na “Upendo Mkamilifu” (1 Yoh. 4:18)

Na. 4: Kuungama Mbele ya Padri—Kwa Nini Kunapingana na Maandiko? (rs uku. 347 ¶1–uku. 348 ¶3)

Nov. 12 Usomaji wa Biblia: Amosi 1-9 Wimbo 211

Sifa ya Usemi: Umalizio Mzuri (be uku. 220 ¶1-3)

Na. 1: Utangulizi wa Amosi na Kwa Nini Ni Chenye Mafaa (si uku. 148-150 ¶1-6, 13-17)

Na. 2: Amosi 2:1-16

Na. 3: Kwa Nini Kujifunza Kupitia Mambo Yanayotupata Siyo Njia Bora Zaidi?

Na. 4: Kuungama Dhambi Dhidi ya Mungu na Wanadamu (rs uku. 349 ¶4–uku. 350 ¶3)

Nov. 19 Usomaji wa Biblia: Obadia 1-21–Yona 1-4 Wimbo 220

Sifa ya Usemi: Kumbuka Mambo Haya (be uku. 221 ¶1-5)

Na. 1: Utangulizi wa Obadia na Yona na Kwa Nini Ni Vyenye Mafaa (si uku. 151-153 ¶1-5, 10-14; uku. 153-155 ¶1-4, 9-12)

Na. 2: Yona 1:1-17

Na. 3: Kwa Nini Lazima Paradiso ya Kiroho Itangulie Paradiso ya Kidunia?

Na. 4: b Kwa Nini Dhambi Nzito Zinapaswa Kuungamwa kwa Wazee? (rs uku. 350 ¶4-8)

Nov. 26 Usomaji wa Biblia: Mika 1-7 Wimbo 18

Sifa ya Usemi: Katika Huduma ya Shambani (be uku. 221 ¶6–uku. 222 ¶6)

Na. 1: Utangulizi wa Mika na Kwa Nini Ni Chenye Mafaa (si uku. 155-158 ¶1-8, 16-19)

Na. 2: Mika 2:1-13

Na. 3: Kinachomaanishwa na Kuwa Mwenye Tabia-Pole

Na. 4: Je, Ni Jambo Linalopatana na Akili Kuamini Uumbaji (rs uku. 390 ¶3–uku. 392 ¶2)

Des. 3 Usomaji wa Biblia: Nahumu 1-3–Habakuki 1-3 Wimbo 137

Sifa ya Usemi: Kusema Mambo Yaliyo Sahihi (be uku. 223 ¶1-5)

Na. 1: Utangulizi wa Nahumu na Habakuki na Kwa Nini Ni Vyenye Mafaa (si uku. 158-160 ¶1-7, 11-12; uku. 161-163 ¶1-5, 12-14)

Na. 2: Habakuki 1:1-17

Na. 3: Kuelewa Simulizi la Biblia la Uumbaji (rs uku. 392 ¶3–uku. 394 ¶4)

Na. 4: Kwa Nini Kuishi Milele Hakutachosha?

Des. 10 Usomaji wa Biblia: Sefania 1-3–Hagai 1-2 Wimbo 78

Sifa ya Usemi: ‘Kushika kwa Imara Neno la Uaminifu’ (be uku. 224 ¶1-4)

Na. 1: Utangulizi wa Sefania na Hagai na Kwa Nini Ni Vyenye Mafaa (si uku. 163-166 ¶1-6, 10-12; uku. 166-168 ¶1-7, 13-16)

Na. 2: Sefania 3:1-17

Na. 3: Kwa Nini Kutukuza Msalaba Kunapingana na Maandiko? (rs uku. 214 ¶1–uku. 214 ¶7)

Na. 4: c Hali Nzuri ya Kiroho Inawezaje Kuathiri Ndoa?

Des. 17 Usomaji wa Biblia: Zekaria 1-8 Wimbo 209

Sifa ya Usemi: Kuchunguza Usahihi wa Habari Unayozungumzia (be uku. 225 ¶1-3)

Na. 1: Utangulizi wa Zekaria (si uku. 168-169 ¶1-7)

Na. 2: Zekaria 7:1-14

Na. 3: Maono ya Kugeuka Sura Yametimizwaje?

Na. 4: Je, Umri wa Watu Walioishi Kabla ya Gharika Ulipimwa kwa Miaka Tunayotumia? (rs uku. 396 ¶4–uku. 397 ¶1)

Des. 24 Usomaji wa Biblia: Zekaria 9-14 Wimbo 202

Sifa ya Usemi: Usemi Unaoeleweka (be uku. 226 ¶1–uku. 227 ¶1)

Na. 1: Zekaria—Kwa Nini Ni Chenye Mafaa na Utangulizi wa Malaki na Kwa Nini Ni Chenye Mafaa (si uku. 171-172 ¶23-27; uku. 172-5 ¶1-6, 13-17)

Na. 2: Zekaria 10:1-12

Na. 3: Kwa Nini Mashahidi wa Yehova Husema Kwamba Ufalme wa Mungu Ulisimamishwa Mwaka wa 1914? (rs uku. 397 ¶2–uku. 399 ¶3)

Na. 4: Tunaweza Kujitayarishaje kwa Ajili ya Mnyanyaso?

Des. 31 Usomaji wa Biblia: Malaki 1-4 Wimbo 118

Sifa ya Usemi: Kufafanua Maneno Yasiyoeleweka (be uku. 227 ¶2–uku. 228 ¶1)

Pitio la Maswali na Majibu

[Maelezo ya Chini]

a Kadiri wakati unavyoruhusu, zingatia jinsi ya kuitikia maoni, madai, na upinzani kwa njia inayofaa zaidi eneo lenu.

b Kadiri wakati unavyoruhusu, zingatia jinsi ya kuitikia maoni, madai, na upinzani kwa njia inayofaa zaidi eneo lenu.

c Hotuba hii itolewe na akina ndugu tu.

d Hotuba hii itolewe na akina ndugu tu.

e Hotuba hii itolewe na akina ndugu tu.

f Hotuba hii itolewe na akina ndugu tu.

g Hotuba hii itolewe na akina ndugu tu.

h Hotuba hii itolewe na akina ndugu tu.

i Kadiri wakati unavyoruhusu, zingatia jinsi ya kuitikia maoni, madai, na upinzani kwa njia inayofaa zaidi eneo lenu.

j Hotuba hii itolewe na akina ndugu tu.

k Hotuba hii itolewe na akina ndugu tu.

l Kadiri wakati unavyoruhusu, zingatia jinsi ya kuitikia maoni, madai, na upinzani kwa njia inayofaa zaidi eneo lenu.

a Kadiri wakati unavyoruhusu, zingatia jinsi ya kuitikia maoni, madai, na upinzani kwa njia inayofaa zaidi eneo lenu.

b Hotuba hii itolewe na akina ndugu tu.

c Hotuba hii itolewe na akina ndugu tu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki