Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 12/08 uku. 2
  • Ratiba ya Mkutano wa Utumishi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ratiba ya Mkutano wa Utumishi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Desemba 8
  • Juma Linaloanza Desemba 15
  • Juma Linaloanza Desemba 22
  • Juma Linaloanza Desemba 29
  • Juma Linaloanza Januari 5
Huduma Yetu ya Ufalme—2008
km 12/08 uku. 2

Ratiba ya Mkutano wa Utumishi

Juma Linaloanza Desemba 8

Wimbo 19

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Pitia kifupi mapendekezo yaliyo kwenye ukurasa wa 8 yanayoonyesha jinsi ya kutoa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Novemba 1 na Amkeni! la Novemba. Waombe wasikilizaji ambao wamekuwa wakitoa magazeti hayo waeleze jinsi ambavyo wamekuwa wakiyatoa. Wamekuwa wakitumia makala, swali, na andiko gani?

Dak. 15: Shule ya Huduma ya Kitheokrasi ya Mwaka wa 2009. Hotuba itolewe na mwangalizi wa shule. Zungumzia mambo ambayo kutaniko lenu linahitaji kuzingatia kutoka katika nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Oktoba 2008. Zungumzia kazi ya mshauri msaidizi. Watie moyo wote wajitahidi sana kutimiza migawo yao, kutoa maelezo wakati wa mambo makuu ya usomaji wa Biblia, na kutumia mapendekezo yanayotolewa kila juma kutoka katika kitabu Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi.

Dak. 20: “Je, Unatumia Kitabu Kutoa Sababu?”a Mnapozungumzia fungu la 4, panga ili painia au mhubiri anayestahili aonyeshe kwa ufupi jinsi ya kutumia kitabu Kutoa Sababu kujibu swali lifuatalo katika huduma ya nyumba kwa nyumba, ‘Kwa nini Mashahidi wa Yehova hawasherehekei Krismasi?’

Wimbo 6

Juma Linaloanza Desemba 15

Wimbo 178

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa katika Huduma Yetu ya Ufalme.

Dak. 10: Rudia Mambo Makuu Katika Huduma. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yakitegemea kitabu Shule ya Huduma, ukurasa wa 207. Panga onyesho moja au mawili mafupi ukitumia mapendekezo yaliyo katika kitabu hicho.

Dak. 25: “‘Toa Ushahidi Kamili’—Kwa Kuhubiri Katika Nyumba za Ghorofa Zenye Wapangaji.”b Ishughulikiwe na mwangalizi wa utumishi au mzee mwingine. Onyesha jinsi mnavyoweza kutumia habari hiyo katika eneo lenu.

Wimbo 157

Juma Linaloanza Desemba 22

Wimbo 75

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Soma ripoti ya hesabu na taarifa ya shukrani. Taja toleo la vichapo la Januari, na upange ili mzee afanye onyesho la kutoa kichapo hicho.

Dak. 15: Jitayarishe Kutoa Mnara wa Mlinzi la Desemba 1 na Amkeni! la Desemba. Mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Baada ya kutaja kwa ufupi mambo yaliyo katika magazeti hayo, waombe wasikilizaji wataje makala ambazo zinaweza kuwavutia watu katika eneo lenu na kwa nini zitawavutia. Ukitumia baadhi ya makala hizo, waombe wasikilizaji wataje swali ambalo watatumia kuanzisha mazungumzo, kisha wataje andiko ambalo watasoma katika makala kabla ya kutoa magazeti hayo. Malizia kwa onyesho la jinsi ya kutoa kila gazeti, ukitumia mapendekezo yaliyo kwenye ukurasa wa 8 au mapendekezo mengine yanayofaa eneo lenu.

Dak. 20: “Siku ya Pekee ya Kuanzisha Mafunzo ya Biblia.”c Tangaza mwisho-juma mmoja katika mwezi wa Januari ambao kutaniko litajitahidi kuanzisha mafunzo ya Biblia. Pitia mapendekezo yaliyo kwenye fungu la 3 na upange onyesho la pendekezo moja au mawili.

Wimbo 133

Juma Linaloanza Desemba 29

Wimbo 60

Funzo la Biblia la Kutaniko:

jd sura ya 12 ¶1-10

Shule ya Huduma ya Kitheokrasi:

Usomaji wa Biblia: Ufunuo 15-22

Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi

Mkutano wa Utumishi:

Wimbo 153

Dak. 5: Matangazo ya kwenu.

Dak. 10: Mahitaji ya kwenu.

Dak. 20: “Kazi ya Kuhubiri Inahitaji Uvumilivu.”d Kadiri wakati unavyoruhusu, waombe wasikilizaji waeleze maandiko ambayo hayakunukuliwa.

Wimbo 155

Juma Linaloanza Januari 5

Wimbo 35

Funzo la Biblia la Kutaniko:

jd sura ya 12 ¶11-22

Shule ya Huduma ya Kitheokrasi:

Usomaji wa Biblia: Mwanzo 1-5

Na. 1: Mwanzo 3:1-15

Na. 2: Kwa Nini Yesu Alikuwa Mwalimu Mkuu? (lr sura ya 1)

Na. 3: Ni Jambo Gani Ambalo Si Ubatili? (1 Kor. 15:58)

Mkutano wa Utumishi:

Wimbo 98

Dak. 5: Matangazo ya kwenu.

Dak. 10: Iga Mtazamo wa Yesu Kuelekea Huduma. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yakitegemea kitabu ‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu,’ ukurasa wa 84-86, fungu la 16-21.

Dak. 20: “Kusanyiko la Wilaya la Mashahidi wa Yehova la Mwaka wa 2009.”e Ishughulikiwe na mwandishi wa kutaniko. Kabla ya kuzungumzia makala hiyo, soma barua ya mgawo wa kusanyiko la wilaya ya Desemba 15, 2008. Kazia umuhimu wa kuonyesha matunda ya roho nyakati zote.—Gal. 5:22, 23.

Wimbo 114

[Maelezo ya Chini]

a Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.

b Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.

c Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.

d Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.

e Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki