Ratiba ya Mkutano wa Utumishi
Juma Linaloanza Desemba 8
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Pitia kifupi mapendekezo yaliyo kwenye ukurasa wa 8 yanayoonyesha jinsi ya kutoa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Novemba 1 na Amkeni! la Novemba. Waombe wasikilizaji ambao wamekuwa wakitoa magazeti hayo waeleze jinsi ambavyo wamekuwa wakiyatoa. Wamekuwa wakitumia makala, swali, na andiko gani?
Dak. 15: Shule ya Huduma ya Kitheokrasi ya Mwaka wa 2009. Hotuba itolewe na mwangalizi wa shule. Zungumzia mambo ambayo kutaniko lenu linahitaji kuzingatia kutoka katika nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Oktoba 2008. Zungumzia kazi ya mshauri msaidizi. Watie moyo wote wajitahidi sana kutimiza migawo yao, kutoa maelezo wakati wa mambo makuu ya usomaji wa Biblia, na kutumia mapendekezo yanayotolewa kila juma kutoka katika kitabu Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi.
Dak. 20: “Je, Unatumia Kitabu Kutoa Sababu?”a Mnapozungumzia fungu la 4, panga ili painia au mhubiri anayestahili aonyeshe kwa ufupi jinsi ya kutumia kitabu Kutoa Sababu kujibu swali lifuatalo katika huduma ya nyumba kwa nyumba, ‘Kwa nini Mashahidi wa Yehova hawasherehekei Krismasi?’
Juma Linaloanza Desemba 15
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa katika Huduma Yetu ya Ufalme.
Dak. 10: Rudia Mambo Makuu Katika Huduma. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yakitegemea kitabu Shule ya Huduma, ukurasa wa 207. Panga onyesho moja au mawili mafupi ukitumia mapendekezo yaliyo katika kitabu hicho.
Dak. 25: “‘Toa Ushahidi Kamili’—Kwa Kuhubiri Katika Nyumba za Ghorofa Zenye Wapangaji.”b Ishughulikiwe na mwangalizi wa utumishi au mzee mwingine. Onyesha jinsi mnavyoweza kutumia habari hiyo katika eneo lenu.
Juma Linaloanza Desemba 22
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Soma ripoti ya hesabu na taarifa ya shukrani. Taja toleo la vichapo la Januari, na upange ili mzee afanye onyesho la kutoa kichapo hicho.
Dak. 15: Jitayarishe Kutoa Mnara wa Mlinzi la Desemba 1 na Amkeni! la Desemba. Mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Baada ya kutaja kwa ufupi mambo yaliyo katika magazeti hayo, waombe wasikilizaji wataje makala ambazo zinaweza kuwavutia watu katika eneo lenu na kwa nini zitawavutia. Ukitumia baadhi ya makala hizo, waombe wasikilizaji wataje swali ambalo watatumia kuanzisha mazungumzo, kisha wataje andiko ambalo watasoma katika makala kabla ya kutoa magazeti hayo. Malizia kwa onyesho la jinsi ya kutoa kila gazeti, ukitumia mapendekezo yaliyo kwenye ukurasa wa 8 au mapendekezo mengine yanayofaa eneo lenu.
Dak. 20: “Siku ya Pekee ya Kuanzisha Mafunzo ya Biblia.”c Tangaza mwisho-juma mmoja katika mwezi wa Januari ambao kutaniko litajitahidi kuanzisha mafunzo ya Biblia. Pitia mapendekezo yaliyo kwenye fungu la 3 na upange onyesho la pendekezo moja au mawili.
Juma Linaloanza Desemba 29
Funzo la Biblia la Kutaniko:
Shule ya Huduma ya Kitheokrasi:
Usomaji wa Biblia: Ufunuo 15-22
Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
Mkutano wa Utumishi:
Dak. 5: Matangazo ya kwenu.
Dak. 10: Mahitaji ya kwenu.
Dak. 20: “Kazi ya Kuhubiri Inahitaji Uvumilivu.”d Kadiri wakati unavyoruhusu, waombe wasikilizaji waeleze maandiko ambayo hayakunukuliwa.
Juma Linaloanza Januari 5
Funzo la Biblia la Kutaniko:
Shule ya Huduma ya Kitheokrasi:
Usomaji wa Biblia: Mwanzo 1-5
Na. 1: Mwanzo 3:1-15
Na. 2: Kwa Nini Yesu Alikuwa Mwalimu Mkuu? (lr sura ya 1)
Na. 3: Ni Jambo Gani Ambalo Si Ubatili? (1 Kor. 15:58)
Mkutano wa Utumishi:
Dak. 5: Matangazo ya kwenu.
Dak. 10: Iga Mtazamo wa Yesu Kuelekea Huduma. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yakitegemea kitabu ‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu,’ ukurasa wa 84-86, fungu la 16-21.
Dak. 20: “Kusanyiko la Wilaya la Mashahidi wa Yehova la Mwaka wa 2009.”e Ishughulikiwe na mwandishi wa kutaniko. Kabla ya kuzungumzia makala hiyo, soma barua ya mgawo wa kusanyiko la wilaya ya Desemba 15, 2008. Kazia umuhimu wa kuonyesha matunda ya roho nyakati zote.—Gal. 5:22, 23.
[Maelezo ya Chini]
a Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.
b Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.
c Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.
d Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.
e Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.