Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mwb24 Januari kur. 8-9
  • Januari 29-Februari 4

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Januari 29-Februari 4
  • Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2024
Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2024
mwb24 Januari kur. 8-9

JANUARI 29–FEBRUARI 4

AYUBU 40-42

Wimbo 124 na Sala | Utangulizi (Dak. 1)

HAZINA ZA NENO LA MUNGU

1. Masomo Tunayojifunza Kutokana na Yaliyompata Ayubu

(Dak. 10)

Tambua kwamba Yehova anafahamu mambo mengi kuliko wewe (Ayu 42:​1-3; w10 10/15 3-4 ¶4-6)

Kubali mashauri kutoka kwa Yehova na tengenezo lake kwa utayari (Ayu 42:​5, 6; w17.06 25 ¶12)

Yehova huwathawabisha wale wanaoendelea kuwa washikamanifu kwake licha ya majaribu (Ayu 42:​10-12; Yak 5:11; w22.06 25 ¶17-18)

Ayubu na mke wake wakiwa kwenye kilima kila mmoja akimtazama mwenzake kwa uthamini. Ayubu anaelekeza mkono kuelekea mifugo na nyumba yao.

Yehova alimthawabisha Ayubu kwa kudumisha utimilifu

2. Hazina za Kiroho

(Dak. 10)

  • Ayu 42:7—Marafiki watatu wa Ayubu walikuwa wakimshtumu nani kihalisi, na kujua jambo hilo kunaweza kutusaidiaje kuvumilia tunapodhihakiwa? (it-2 808)

  • Ungependa kushiriki nasi hazina gani kutoka kwenye usomaji wa Biblia wa juma hili?

3. Usomaji wa Biblia

(Dak. 4) Ayu 42:​1-17 (th somo la 11)

BORESHA HUDUMA YAKO

4. Kuanzisha Mazungumzo

(Dak. 3) NYUMBA KWA NYUMBA. Mwenye nyumba ni wa dini ambayo si ya Kikristo. (lmd somo la 5 jambo kuu la 3)

5. Kufanya Wanafunzi

(Dak. 5) lff somo la 13 jambo kuu la 6-7 na Watu Fulani Husema (lmd somo la 11 jambo kuu la 4)

6. Hotuba

(Dak. 4) lmd nyongeza A jambo kuu la 2—Kichwa: Dunia Haitaharibiwa Kamwe. (th somo la 13)

MAISHA YA MKRISTO

Wimbo 108

7. Wasaidie Wengine Wahisi Kwamba Yehova Anawapenda

(Dak. 15) Mazungumzo.

Picha kutoka kwenye video “Tulipata Upendo wa Kikristo Katika Familia ya Yehova.” Mimi na mama yake wakimtembelea dada hospitalini na kumpelekea maua na kadi.

Tunafurahi kumwabudu Mungu ambaye ndiye chanzo cha upendo. (1Yo 4:​8, 16) Upendo wa Yehova unatuvuta kwake na unatuchochea kuendelea kukaa karibu naye. Tukiwa kondoo wa Yehova, sote tunahisi kwamba anatupenda.

Tunamwiga Yehova katika kuonyesha upendo kupitia jinsi tunavyowatendea washiriki wa familia zetu, waabudu wenzetu, na watu wengine. (Ayu 6:14; 1Yo 4:11) Tunapowaonyesha wengine upendo, tunawasaidia kumjua Yehova na kumkaribia. Kinyume na hilo, tukikosa kuwaonyesha wengine upendo, huenda ikawa vigumu kwao kuhisi upendo wa Yehova.

Onyesha VIDEO Tulipata Upendo wa Kikristo Katika Familia ya Yehova. Kisha uwaulize wasikilizaje:

Simulizi la Lei Lei na Mimi limekufundisha nini kuhusu umuhimu wa kuonyesha upendo?

Tunaweza kufanya nini ili kuwasaidia waabudu wenzetu kuhisi upendo wa Yehova?

  • Waone kama kondoo wa Yehova wenye thamani.—Zb 100:3

  • Zungumza nao kwa njia yenye kujenga.—Efe 4:29

  • Watendee kwa njia inayoonyesha unaelewa hisia zao.—Mt 7:​11, 12

8. Funzo la Biblia la Kutaniko

(Dak. 30) bt sura ya 5 ¶1-8, sanduku uk. 39

Umalizio (Dak. 3) | Wimbo 126 na Sala

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki