OKTOBA 20-26
MHUBIRI 9-10
Wimbo 30 na Sala | Utangulizi (Dak. 1)
1. Uwe na Mtazamo Unaofaa Kuhusu Majaribu Unayopitia
(Dak. 10)
Tunajua kwamba majaribu si ishara ya kwamba hatuna kibali cha Yehova (Mhu 9:11; w13 8/15 14 ¶20-21)
Hatutarajii mambo yawe mazuri katika mfumo huu wa mambo wa Shetani (Mhu 10:7; w19.09 5 ¶10)
Tunahitaji kutenga wakati ili kufurahia zawadi ambazo Yehova ametupatia, hata ikiwa tunakabili changamoto (Mhu 9:7, 10; w11 10/15 8 ¶1-2)
2. Hazina za Kiroho
(Dak. 10)
Mhu 10:12-14—Mistari hii inatupatia onyo gani kuhusu porojo? (it “Porojo, Uchongezi” ¶4, 8)
Ungependa kushiriki nasi hazina gani kutoka kwenye usomaji wa Biblia wa juma hili?
3. Usomaji wa Biblia
(Dak. 4) Mhu 10:1-20 (th somo la 11)
4. Kuanzisha Mazungumzo
(Dak. 3) MAHUBIRI YA UMMA. Anzisha mazungumzo na mtu anayeonekana kuwa mwenye huzuni. (lmd somo la 3 jambo kuu la 4)
5. Kuanzisha Mazungumzo
(Dak. 4) MAHUBIRI YASIYO RASMI. Zungumzia moja ya “Kweli Tunazopenda Kufundisha” kutoka kwenye nyongeza A ya broshua Wapende Watu na mtu anayekueleza kwamba anahangaishwa na hali ya kiuchumi. (lmd somo la 4 jambo kuu la 4)
6. Kufanya Wanafunzi
Wimbo 47
7. Kupata Utulivu Tunapokabili Msiba
(Dak. 15) Mazungumzo.
Kila siku sisi hukabili majaribu na changamoto. Hata hivyo, baadhi ya majaribu hutukia ghafla, na yanaumiza sana hivi kwamba yanaweza kutulemea kihisia, kimwili, na hata kiroho. Tunawezaje kupata utulivu tunapokabili msiba?
Hata iwe tunakabili jaribu gani, sikuzote Yehova ‘ndiye tegemeo imara la nyakati zetu.’ (Isa 33:6) Ili kumtegemea Yehova, tunahitaji kuwa wenye kiasi na usawaziko. (Met 11:2) Ikiwa tunakabili msiba, huenda tukahitaji kutafuta wakati ili kumtunza mpendwa wetu au sisi wenyewe, kufanya maamuzi yenye hekima, au kutafuta wakati ili tukabiliane na huzuni. (Mhu 4:6)
Kwa kuwa Yehova anatumia waabudu wake ili kuimarishana, tunapaswa pia kuwa tayari kuomba au kukubali msaada. Kumbuka kwamba waabudu wenzako wanakupenda sana, na wako tayari kukutegemeza.
Soma 2 Wakorintho 4:7-9. Kisha waulize wasikilizaji:
Kwa nini tunapaswa kuendelea kujitahidi kudumisha ratiba yetu ya kiroho hata inapokuwa vigumu kwetu kufanya hivyo?
Onyesha VIDEO Yehova Yuko Karibu na Wale Waliovunjika Moyo. Kisha waulize wasikilizaji:
Yehova aliwasaidiaje Ndugu na Dada Septer?
Waabudu wenzao waliwasaidiaje?
Umejifunza jambo gani lingine kutokana na mfano wao?
8. Funzo la Biblia la Kutaniko
(Dak. 30) lfb somo la 28, utangulizi wa sehemu ya 6, na somo la 29