Ukurasa wa Kichwa/Ukurasa wa Wachapishaji
2009 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova ya
Kina Ripoti ya Mwaka wa Utumishi wa 2008
Kitabu hiki na cha ․․․․․
‘Toa ushahidi kamili kuhusu habari njema.’—MATENDO 20:24.
Mtume Paulo alikuwa amemaliza safari tatu za umishonari na alikuwa amepata majaribu na baraka pia. Sasa alikuwa akielekea Yerusalemu, ambako hakutazamia kukaribishwa kwa uchangamfu, kwa kuwa “vifungo na dhiki” vilikuwa vikimngojea huko. (Mdo. 20:23) Hata hivyo, hakuvunjika moyo. Akiwa Mileto, aliwaambia hivi wazee wa kutaniko la Efeso: “Siifanyi nafsi yangu kuwa kitu chenye thamani sana kwangu, kama tu ningepata kumaliza mwendo wangu na huduma niliyopokea kutoka kwa Bwana Yesu, kutoa ushahidi kamili kuhusu habari njema ya fadhili zisizostahiliwa za Mungu.”—Mdo. 20:24.
Paulo alithamini uhai wake, lakini jambo kuu maishani mwake lilikuwa kufanya mapenzi ya Mungu. Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote wana maoni hayohayo. Ingawa ‘wanachukiwa na mataifa yote’ kama Yesu alivyotabiri, watu wa Mungu wamehubiri habari njema mpaka miisho ya dunia, nao wanahubiri kwa ujasiri katika karibu kila taifa. (Mt. 24:9) Andiko la mwaka wa 2009 na likuchochee kuendelea kutoa ushahidi bila kuacha, na hivyo kuonyesha kwamba unathamini fadhili zisizostahiliwa za Mungu.
[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 2]
Photo Credits: Page 168: Franc Drozg, letter; Photo Archive-Museum of National Liberation Maribor, Slovenia