Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Leo

Alhamisi, Oktoba 16

Fungueni njia ya Yehova! Tengenezeni barabara kuu iliyonyooka inayopitia jangwani kwa ajili ya Mungu wetu.—Isa. 40:3.

Safari ngumu kutoka Babiloni kwenda Israeli ingechukua miezi minne hivi, lakini Yehova aliahidi kwamba kizuizi chochote ambacho kingeonekana kuwa kinazuia safari hiyo kingeondolewa. Wayahudi waaminifu walijua kwamba ikiwa wangerudi katika nchi ya Israeli wangepata baraka nyingi kuliko jambo lolote ambalo wangedhabihu. Baraka kuu zaidi ilihusiana na ibada yao. Hakukuwa na hekalu la Yehova katika jiji la Babiloni. Hakukuwa na madhabahu ambayo Waisraeli wangetoa dhabihu zilizotajwa katika Sheria ya Musa, na hakukuwa na mpango wa makuhani ambao wangetoa dhabihu hizo. Isitoshe watumishi wa Yehova walikuwa wachache kwa kulinganishwa na idadi kubwa sana ya watu ambao waliabudu miungu ya uwongo, na ambao hawakumheshimu Yehova na viwango vyake. Basi, maelfu ya Wayahudi waliomwogopa Mungu, walitazamia kwa hamu kurudi katika nchi yao ambako wangerudisha ibada safi. w23.05 14-15 ¶3-4

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Ijumaa, Oktoba 17

Endeleeni kutembea kama watoto wa nuru.—Efe. 5:8.

Tunahitaji msaada wa roho takatifu ya Mungu ili tuweze kuendelea kujiendesha “kama watoto wa nuru.” Kwa nini? Kwa sababu si rahisi kuendelea kuwa safi katika ulimwengu huu uliopotoka kimaadili. (1 The. 4:​3-5, 7, 8) Roho takatifu inaweza kutusaidia kupambana na mawazo ya ulimwengu, kutia ndani falsafa zake na maoni yake yanayopingana na mawazo ya Mungu. Roho takatifu pia inaweza kutusaidia kutokeza “kila namna ya wema na uadilifu.” (Efe. 5:9) Njia moja tunayoweza kupata roho takatifu ni kwa kumwomba Yehova. Yesu alisema kwamba Yehova ‘atawapa roho takatifu wale wanaomwomba.’ (Luka 11:13) Na tunapomsifu Yehova pamoja kwenye mikutano ya Kikristo, tunapokea pia roho takatifu. (Efe. 5:​19, 20) Na roho takatifu ya Mungu itatuchochea tuishi kwa njia inayompendeza Mungu. w24.03 23-24 ¶13-15

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Jumamosi, Oktoba 18

Endeleeni kuomba, nanyi mtapewa; endeleeni kutafuta, nanyi mtapata; endeleeni kupiga hodi, nanyi mtafunguliwa.—Luka 11:9.

Je, unahitaji kuwa mwenye subira zaidi? Ikiwa ndivyo, sali ili uwe mwenye subira zaidi. Subira ni moja kati ya sifa za tunda la roho. (Gal. 5:​22, 23) Basi, tunaweza kusali ili tupate roho takatifu na kumwomba Yehova atusaidie kusitawisha sifa za tunda la roho. Tunapokabili hali inayofanya iwe vigumu kwetu kuwa wenye subira, ‘tunaendelea kuomba’ tupewe roho takatifu ili itusaidie kuwa wenye subira. (Luka 11:13) Pia, tunaweza kumwomba Yehova atusaidie kuona mambo kulingana na maoni yake. Kisha, baada ya kusali, tunapaswa kujitahidi kabisa kuonyesha subira kila siku. Kadiri tunavyosali ili tuwe na subira na kujitahidi kuwa wenye subira, ndivyo sifa hiyo itakavyozidi kutia mizizi katika mioyo yetu na kuwa sehemu ya utu wetu. Kutafakari mifano iliyo katika Biblia kutatusaidia pia. Biblia ina mifano ya watu wengi ambao walikuwa na subira. Tunapotafakari kuhusu masimulizi hayo, tunaweza kujifunza njia za kuonyesha subira. w23.08 22 ¶10-11

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki