Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Leo

Jumatano, Oktoba 15

Mimi ndiye Alfa na Omega.—Ufu. 1:8.

Herufi alfa ndiyo ya kwanza katika alfabeti ya Kigiriki, na herufi omega ndiyo ya mwisho. Kwa kusema kwamba yeye ndiye “Alfa na Omega,” Yehova anatusaidia kuelewa kwamba anapoanza kufanya jambo fulani, lazima alikamilishe kwa mafanikio. Baada ya kuwaumba Adamu na Hawa, Yehova alisema hivi: “Zaeni, muwe wengi, muijaze dunia na kuitiisha.” (Mwa. 1:28) Wakati huo ni kama Yehova alikuwa akisema “Alfa.” Alieleza waziwazi kusudi lake kwamba wakati utafika ambapo dunia itajaa wazao wa Adamu na Hawa walio wakamilifu na watiifu, ambao wataigeuza dunia kuwa paradiso. Wakati huo ujao, kusudi lake litakapotimia, ni kana kwamba atasema “Omega.” Baada ya kukamilisha uumbaji wa “mbingu na dunia na kila kitu kilichomo,” Yehova alitoa uhakikisho huu. Alitoa uhakikisho kwamba atatimiza kusudi lake kwa ajili ya wanadamu na dunia. Lingetimizwa kikamili mwishoni mwa ile siku ya saba.—Mwa. 2:​1-3. w23.11 5 ¶13-14

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Alhamisi, Oktoba 16

Fungueni njia ya Yehova! Tengenezeni barabara kuu iliyonyooka inayopitia jangwani kwa ajili ya Mungu wetu.—Isa. 40:3.

Safari ngumu kutoka Babiloni kwenda Israeli ingechukua miezi minne hivi, lakini Yehova aliahidi kwamba kizuizi chochote ambacho kingeonekana kuwa kinazuia safari hiyo kingeondolewa. Wayahudi waaminifu walijua kwamba ikiwa wangerudi katika nchi ya Israeli wangepata baraka nyingi kuliko jambo lolote ambalo wangedhabihu. Baraka kuu zaidi ilihusiana na ibada yao. Hakukuwa na hekalu la Yehova katika jiji la Babiloni. Hakukuwa na madhabahu ambayo Waisraeli wangetoa dhabihu zilizotajwa katika Sheria ya Musa, na hakukuwa na mpango wa makuhani ambao wangetoa dhabihu hizo. Isitoshe watumishi wa Yehova walikuwa wachache kwa kulinganishwa na idadi kubwa sana ya watu ambao waliabudu miungu ya uwongo, na ambao hawakumheshimu Yehova na viwango vyake. Basi, maelfu ya Wayahudi waliomwogopa Mungu, walitazamia kwa hamu kurudi katika nchi yao ambako wangerudisha ibada safi. w23.05 14-15 ¶3-4

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Ijumaa, Oktoba 17

Endeleeni kutembea kama watoto wa nuru.—Efe. 5:8.

Tunahitaji msaada wa roho takatifu ya Mungu ili tuweze kuendelea kujiendesha “kama watoto wa nuru.” Kwa nini? Kwa sababu si rahisi kuendelea kuwa safi katika ulimwengu huu uliopotoka kimaadili. (1 The. 4:​3-5, 7, 8) Roho takatifu inaweza kutusaidia kupambana na mawazo ya ulimwengu, kutia ndani falsafa zake na maoni yake yanayopingana na mawazo ya Mungu. Roho takatifu pia inaweza kutusaidia kutokeza “kila namna ya wema na uadilifu.” (Efe. 5:9) Njia moja tunayoweza kupata roho takatifu ni kwa kumwomba Yehova. Yesu alisema kwamba Yehova ‘atawapa roho takatifu wale wanaomwomba.’ (Luka 11:13) Na tunapomsifu Yehova pamoja kwenye mikutano ya Kikristo, tunapokea pia roho takatifu. (Efe. 5:​19, 20) Na roho takatifu ya Mungu itatuchochea tuishi kwa njia inayompendeza Mungu. w24.03 23-24 ¶13-15

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki