Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Leo

Jumamosi, Agosti 16

Atawapa msingi imara.—1 Pet. 5:10.

Jichunguze kwa unyoofu ili kutambua udhaifu wowote ulio nao, lakini usivunjike moyo. “Bwana ni mwenye fadhili,” na atakusaidia kufanya maendeleo. (1 Pet. 2:3) Mtume Petro anatuhakikishia hivi: “Mungu . . . mwenyewe atamaliza mazoezi yenu. Atafanya muwe imara.” Pindi moja, Petro alihisi kwamba hastahili kuwa pamoja na Mwana wa Mungu. (Luka 5:8) Lakini kwa msaada wa upendo kutoka kwa Yehova na Yesu, Petro aliendelea kuwa mwaminifu akiwa mfuasi wa Kristo. Hivyo, Petro alipata kibali cha “kuingia katika Ufalme wa milele wa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo.” (2 Pet. 1:11) Hiyo ilikuwa baraka iliyoje! Ikiwa utaendelea kuwa mwaminifu kama Petro alivyofanya na kukubali kuzoezwa na Yehova, wewe pia utapata thawabu ya uzima wa milele. ‘Utafikia lengo la imani yako, wokovu wako.’—1 Pet. 1:9. w23.09 31 ¶16-17

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Jumapili, Agosti 17

Mwabuduni Yule aliyeziumba mbingu na dunia.—Ufu. 14:7.

Hema la ibada la kale lilikuwa na ua mmoja—eneo lililo wazi ambalo lilikuwa limezungushiwa wigo au ukingo, mahali ambapo makuhani walitimiza majukumu yao. Madhabahu kubwa ya shaba ya dhabihu za kuteketezwa ilikuwa katika ua pamoja na beseni kubwa la maji la shaba ambalo makuhani walitumia kujitakasa kabla ya kutimiza utumishi wao mtakatifu. (Kut. 30:​17-20; 40:​6-8) Leo, watiwa-mafuta waliobaki duniani ambao ni ndugu za Kristo wanatumikia kwa uaminifu katika ua wa ndani wa hekalu la kiroho duniani. Kuwepo kwa beseni kubwa la maji ni kikumbusho muhimu kwao, na kwa Wakristo wote cha kuendelea kuwa safi kiadili na kiroho. Basi, wale wanaofanyiza “umati mkubwa,” wanamwabudu Yehova wakiwa wapi? Mtume Yohana aliwaona wakiwa “wamesimama mbele ya kiti cha ufalme,” sehemu ambayo inalingana na ua wa nje duniani, ambapo “wanamtolea [Mungu] utumishi mtakatifu mchana na usiku katika hekalu lake.” (Ufu. 7:​9, 13-15) Tunathamini sana pendeleo la kushiriki katika mpango wa ibada safi ya Yehova! w23.10 28 ¶15-16

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Jumatatu, Agosti 18

Kwa sababu ya ahadi ya Mungu, . . . alikuwa mwenye nguvu kwa imani yake.—Rom. 4:20.

Njia moja ambayo Yehova anatupatia nguvu ni kupitia wazee wa kutaniko. (Isa. 32:​1, 2) Basi unapohisi wasiwasi, waeleze wazee wa kutaniko mambo yanayokuhangaisha. Wanapokupatia msaada, usisite kuukubali. Kupitia kwao, Yehova anaweza kukupa nguvu. Tumaini letu linalotegemea Biblia la kupata uzima wa milele—iwe ni katika dunia Paradiso au katika Ufalme wa mbinguni—linaweza pia kutujaza nguvu. (Rom. 4:​3, 18, 19) Tumaini letu linatutia nguvu ili tuendelee kuvumilia majaribu, tuhubiri habari njema, na tutimize migawo mbalimbali kutanikoni. (1 The. 1:3) Tumaini hilohilo lilimtia nguvu mtume Paulo. Alikuwa ‘amekandamizwa,’ ‘kufadhaishwa,’ ‘kuteswa,’ na ‘kuangushwa chini.’ Hata uhai wake ulikuwa hatarini. (2 Kor. 4:​8-10) Paulo alipata nguvu za kuvumilia kwa kukazia fikira tumaini lake. (2 Kor. 4:​16-18) Paulo alikazia fikira tumaini lake la wakati wake ujao la kuishi milele mbinguni. Paulo alitafakari kuhusu tumaini hilo. Na matokeo ni kwamba alihisi “anafanywa upya siku kwa siku.” w23.10 15-16 ¶14-17

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki