Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Leo

Alhamisi, Agosti 21

Uvumilivu [hutokeza] hali yenye kukubaliwa; nayo hali yenye kukubaliwa, tumaini.—Rom. 5:4.

Uvumilivu wako hukupatia kibali cha Yehova. Hilo halimaanishi kwamba Yehova anafurahi unapokabili majaribu au matatizo. Wewe ndiye anayekukubali. Uvumilivu wako hutokeza hali yenye kukubaliwa. Baraka bora sana! (Zab. 5:12) Kumbuka kwamba Abrahamu alivumilia majaribu na kufurahia kibali cha Mungu. Yehova alimwona Abrahamu kuwa rafiki Yake na akahesabiwa kuwa mwadilifu. (Mwa. 15:6; Rom. 4:​13, 22) Inaweza kuwa hivyo kwetu pia. Mungu hatoi kibali chake kwa msingi wa kiasi cha kazi tunachofanya katika utumishi wake au mapendeleo tunayofurahia. Anatupatia kibali chake kwa sababu ya kuvumilia kwa uaminifu. Sisi sote tunaweza kuvumilia, licha ya umri, hali, au uwezo wetu. Je, kwa sasa unavumilia kwa uaminifu jaribu fulani? Ikiwa ndivyo, kumbuka kwamba una kibali cha Mungu. Kutambua kwamba tuna kibali cha Mungu kunaweza kuwa na matokeo makubwa sana kwetu. Kunaweza kuimarisha tumaini letu. w23.12 11 ¶13-14

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Ijumaa, Agosti 22

Jithibitishe kuwa mwanamume.—1 Fal. 2:2.

Ni lazima mwanamume Mkristo ajifunze kuwasiliana vizuri. Mwanamume anayewasiliana vizuri anasikiliza na kutambua mawazo na hisia za wengine. (Met. 20:5) Anaweza kutambua mabadiliko ya sauti ya mtu, ishara za uso, na za mwili. Huwezi kujifunza kufanya mambo hayo bila kutumia muda pamoja na watu. Ikiwa una mazoea ya kutumia tu vifaa vya kielektroni ili kuwasiliana, kama vile kutuma barua-pepe na jumbe za simu, uwezo wako wa kuwasiliana ana kwa ana na watu unaweza kupungua. Hivyo, tafuta fursa za kuzungumza na watu wengine ana kwa ana. (2 Yoh. 12) Ni lazima pia mwanamume Mkristo mkomavu awe na uwezo wa kujitegemeza na kuwategemeza watu wa nyumba yake. (1 Tim. 5:8) Ni vizuri kujifunza ustadi utakaokusaidia kupata kazi. (Mdo. 18:​2, 3; 20:34; Efe. 4:28) Fanya kazi kwa bidii na uhakikishe unakamilisha kazi unayoanza. Wengine watatambua hilo na watathamini kazi yako. Hivyo, kuna uwezekano mkubwa zaidi wa kupata kazi na kuidumisha. w23.12 27 ¶12-13

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Jumamosi, Agosti 23

Siku ya Yehova inakuja kama vile mwizi anavyokuja usiku.—1 The. 5:2.

Biblia inapozungumza kuhusu “siku ya Yehova,” inarejelea wakati ambapo Yehova anawaharibu maadui wake na kuwaokoa watu wake. Zamani, pindi fulani, Yehova alileta hukumu juu ya mataifa. (Isa. 13:​1, 6; Eze. 13:5; Sef. 1:8) Katika nyakati zetu, “siku ya Yehova” itaanza wakati ambapo Babiloni Mkubwa atashambuliwa na itakwisha katika vita vya Har–​Magedoni. Ili tuokoke “siku” hiyo, tunahitaji kujitayarisha sasa. Yesu alitufundisha kwamba hatupaswi tu kuwa tayari kwa ajili ya “dhiki kuu” bali pia ‘tuendelee kuwa tayari.’ (Mt. 24:21; Luka 12:40) Katika barua yake ya kwanza iliyoongozwa na roho takatifu ambayo aliwaandikia Wathesalonike, mtume Paulo alitumia mifano kadhaa kuwasaidia Wakristo waendelee kuwa tayari kwa ajili ya siku kuu ya Yehova ya hukumu. Paulo alijua kamba siku ya Yehova haingefika wakati huo. (2 The. 2:​1-3) Ingawa hivyo, aliwahimiza ndugu zake wajitayarishe kwa ajili ya siku hiyo kana kwamba ingekuja kesho, na sisi pia tunahitaji kufuata shauri hilo. w23.06 8 ¶1-2

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki