Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Leo

Ijumaa, Agosti 22

Jithibitishe kuwa mwanamume.—1 Fal. 2:2.

Ni lazima mwanamume Mkristo ajifunze kuwasiliana vizuri. Mwanamume anayewasiliana vizuri anasikiliza na kutambua mawazo na hisia za wengine. (Met. 20:5) Anaweza kutambua mabadiliko ya sauti ya mtu, ishara za uso, na za mwili. Huwezi kujifunza kufanya mambo hayo bila kutumia muda pamoja na watu. Ikiwa una mazoea ya kutumia tu vifaa vya kielektroni ili kuwasiliana, kama vile kutuma barua-pepe na jumbe za simu, uwezo wako wa kuwasiliana ana kwa ana na watu unaweza kupungua. Hivyo, tafuta fursa za kuzungumza na watu wengine ana kwa ana. (2 Yoh. 12) Ni lazima pia mwanamume Mkristo mkomavu awe na uwezo wa kujitegemeza na kuwategemeza watu wa nyumba yake. (1 Tim. 5:8) Ni vizuri kujifunza ustadi utakaokusaidia kupata kazi. (Mdo. 18:​2, 3; 20:34; Efe. 4:28) Fanya kazi kwa bidii na uhakikishe unakamilisha kazi unayoanza. Wengine watatambua hilo na watathamini kazi yako. Hivyo, kuna uwezekano mkubwa zaidi wa kupata kazi na kuidumisha. w23.12 27 ¶12-13

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Jumamosi, Agosti 23

Siku ya Yehova inakuja kama vile mwizi anavyokuja usiku.—1 The. 5:2.

Biblia inapozungumza kuhusu “siku ya Yehova,” inarejelea wakati ambapo Yehova anawaharibu maadui wake na kuwaokoa watu wake. Zamani, pindi fulani, Yehova alileta hukumu juu ya mataifa. (Isa. 13:​1, 6; Eze. 13:5; Sef. 1:8) Katika nyakati zetu, “siku ya Yehova” itaanza wakati ambapo Babiloni Mkubwa atashambuliwa na itakwisha katika vita vya Har–​Magedoni. Ili tuokoke “siku” hiyo, tunahitaji kujitayarisha sasa. Yesu alitufundisha kwamba hatupaswi tu kuwa tayari kwa ajili ya “dhiki kuu” bali pia ‘tuendelee kuwa tayari.’ (Mt. 24:21; Luka 12:40) Katika barua yake ya kwanza iliyoongozwa na roho takatifu ambayo aliwaandikia Wathesalonike, mtume Paulo alitumia mifano kadhaa kuwasaidia Wakristo waendelee kuwa tayari kwa ajili ya siku kuu ya Yehova ya hukumu. Paulo alijua kamba siku ya Yehova haingefika wakati huo. (2 The. 2:​1-3) Ingawa hivyo, aliwahimiza ndugu zake wajitayarishe kwa ajili ya siku hiyo kana kwamba ingekuja kesho, na sisi pia tunahitaji kufuata shauri hilo. w23.06 8 ¶1-2

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Jumapili, Agosti 24

Ndugu zangu wapendwa, iweni imara, thabiti.—1 Kor. 15:58.

Mwishoni mwa miaka ya 1970, jengo lenye ghorofa 60 lilijengwa hatua kwa hatua huko Tokyo, Japani. Watu walijiuliza jengo hilo lingewezaje kuhimili matetemeko ya ardhi yanayotokea mara kwa mara katika jiji hilo. Siri ilikuwa nini? Mainjinia walikuwa wamebuni jengo hilo liwe imara lakini lenye uwezo wa kunyumbulika ili lihimili mitikisiko ya tetemeko la ardhi. Wakristo ni kama ghorofa hilo refu. Jinsi gani? Mkristo anapaswa kudumisha usawaziko kati ya kuwa imara na kunyumbulika. Anapaswa kuwa imara na thabiti na kuazimia kuendelea kutii sheria na viwango vya Yehova. Anakuwa “tayari kutii” na halegezi msimamo wake. Kwa upande mwingine, anahitaji kuwa mwenye “usawaziko,” au mwenye kunyumbulika, ikiwa hali inaruhusu au hata anapohitajika kufanya hivyo. (Yak. 3:17) Mkristo ambaye amejifunza kuwa na maoni hayo yenye usawaziko ataepuka kushikilia sana maoni yake au kuendekeza mambo yasiyofaa. w23.07 14 ¶1-2

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki