Ma referanse ya mu Kayé ya renion maisha na kaji ya kuubiri
© 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
5-11 JANVIER
MAFUNDISHO YA LAZIMA YA MU BIBLE | ISAYA 17-20
“Kile kitabapata bale beko natwangaisha”
w18.06 p. 7 par. 16
“Ufalme yangu aina ya mu iyi dunia”
16 Ni kintu kya lazima sana kufanya ile mabadiliko! Bible inasema kama bantu beko sa vile mayi ya mu mutoni ile iko natenka-tenka nju kuko mpepo ya nguvu sana. (Isa. 17:12; 57:20, 21; Ufu. 13:1) Ata kama mambo ya politike iko nafanya bantu ba mingi leo bashikuwe tena mu kimoya na banze kufanshiana mambo ya mubaya, shiye tuko mu kimoya na tuko na amani. Saa Jeova anaona vile bantu ba mu iyi dunia abana mu kimoya, anashikiaka mubaya. Lakini anekalaka na furaa sana saa anaona bantu bake beko mu kimoya.—Soma Sefania 3:17.
w16.04 p. 28 par. 4
Ushiringishe mu mambo ya mu iyi dunia ya bantu bale abana mu kimoya
4 Pengine mu inchi yenu akuna fujo mu mambo ya politike na ile inasaidia kaji ya Jeova iende ku mbele. Lakini vile iyi dunia ya Shetani iko naenda ku mwisho, pengine uku ku mbele bitakuwa nguvu kukatala kuringisha mu mambo ya politike. Dunia italabika kupita nju ishakuyala bantu bale ‘abapendake kusikilizana na bengine,’ na bale beko na ‘bichwa nguvu.’ (2 Ti. 3:3, 4) Mu ma inchi ingine, ba nduku yetu beko nateswa sana nju fujo iritokea mu mambo ya politike pashipo kuwazia. Njo maana, ni muzuri kwanziapo leo kwepuka kuringisha mu mambo ya politike. Kama tunachunga asema kya nguvu kifike mbele, tunezi kwacha imani yetu na kuringisha mu mambo ya politike. Kusema tu bya kweri, bantu ba mu iyi dunia abana mu kimoya. Sasa tunezi kufanya nini nju tushiringishe mu mambo yabo? Tuone mambo 4 ile inezi kutusaidia.
ip-1 p. 198 par. 20
Shauri ile Jeova anapachia mataifa
20 Sasa, kutatokea nini? Isaya anajibu ivi: “Mangaribi kuko kintu kya kongopesha. Mbele busubui bufike akinako tena. Njo kile kitafikia bale beko natuteswa na bale beko natunyanganya bintu byetu.” (Isaya 17:14) Saa bantu beko nafanshia bantu ba Jeova bibaya na kubashushia eshima, iko sa vile beko nabanyanganya bintu byabo. Nju bantu ba Jeova abekalake mu makanisa ya munene-munene ya mu iyi dunia na abapendake kuwamo, njo pale banabasemaka-semaka mubaya na kubateswa. Ata vile, batumishi ba Jeova beko sire asema “busubui” bule mateso yabo itaisha abuna mbari tena.—2 Watesalonike 1:6-9; 1 Petro 5:6-11.
Ma leson ya mu Bible
w06 1/12 p. 11 par. 1
Mawazo ya lazima ya mu kitabu kya Isaya—I
20:2-5—Eske ni bya kweri tu Isaya arianzaka kujunguluka-junguluka miaka 3 pashipo manguo? Pengine Isaya aritoshaka tu nguo yake ya yulu, na ile saa arianzaka kujunguluka-junguluka arikuwa na nguo. Lakini aikwanzake kufunika maungu yake yote.—1 Samweli 19:24.
12-18 JANVIER
MAFUNDISHO YA LAZIMA YA MU BIBLE | ISAYA 21-23
Mambo ile irimufikiaka Shebna inatufundisha nini?
w18.03 p. 25 par. 7-9
Disipline ile Jeova anatupachiaka inaonesha asema anatupenda
7 Nju ya kuyuwa buzuri bwa disipline, tuone bantu bawiri bale Jeova aripachiaka disipline: Shebna, ule ariishi wakati ya Mufalme Hezekia, na Graham, ndugu wa mu inchi moya ivi. Nju Shebna arianzaka kushimamia pengine nyumba ya Ezekia, arikuwa shefu wa yulu sana. (Isa. 22:15) Lakini, arifikiaka kwanza kuripandisha sana, na kuritafutia utukufu. Arifikiaka ata na kujifanshia tuburi ya bei sana, na aritembea mu ma shario ya bei ya yulu sana ile barianzaka kukokota kwa ba sheval!—Isa. 22:16-18.
8 Nju Shebna arijitafutiaka utukufu, Mungu arimutoshaka bushefu na aribupachia Eliakim. (Isa. 22:19-21) Ile irifanshikaka saa Senakeribe, mufalme wa Asiri, arianzaka kupanga kubamba mukini ya Yerusalemu. Kisha mashiku kupita, Senakeribe aritumaka bakubwa ba mu guvernema yake mu Yerusalemu. Bale bakubwa bariendaka na ba soda ba mingi nju ya ku dekurajé Bayahudi na kumongopesha Ezekia nju achirie tu babambe Yerusalemu. (2 Fa. 18:17-25) Ezekia arimutumaka Eliakim aende kusumburia na bale bakubwa, lakini ashikwendaka ye moya. Ariendaka na bantu bengine bawiri. Mu bale bantu murikuwa Shebna. Shebna arikuwaka sekretere ile wakati. Ile inezi kuonesha asema Shebna ashikufungaka kishilani ku roo, lakini arijishushaka na kwichika kaji ile aina na valere ya mingi. Tuone mambo tatu ile mufano yake inatufundisha.
9 Kintu kya kwanza, Shebna aripoteshaka bu shefu bwake. Mufano yake inatuonesha asema muntu wa ‘kuripandisha anangukaka, na muntu wa kujivuna anafikiaka kurikwala.’ (Mez. 16:18) Kama uko na ma kaji mu kutaniko ile inafanyaka pengine bantu banze kukuona-ona sana, eske unafanyaka yako yote nju ushiripandishe mabeka? Eske unakumbukaka asema ni Jeova njo anakupachiaka nguvu na akiri ya kufanya bile byote? (1 Ko. 4:7) Mutume Paulo arianjikaka ivi: ‘Minamianbia mweye bote asema, kila muntu ashanze kuwaza sana nju yake kupita vile inalomba kuwaza; lakini awaze nju ya kukuwa na mawazo ya muzuri.’—Ro. 12:3.
w18.03 p. 25 par. 10
Disipline ile Jeova anatupachiaka inaonesha asema anatupenda
10 Kintu kya piri, kama Jeova arimushauriaka Shebna, pengine ni nju arikuwaka sire asema Shebna atashanjé. (Mez. 3:11, 12) Iyi mufano inezi kusaidia bale bashakupotesha ma kaji fulani mu kutaniko. Kuriko kufunga kishilani ku roo, banezi kwendelea kumutumikia Jehova na roo moya na kukumbuka asema disipline ile Jeova anatupachiaka inaonesha asema anatupenda. Ushisabu asema, kama tunarishusha, Jehova eko sire asema tunezi kushanjé. (Soma 1 Petro 5:6, 7.) Anatumikishaka disipline yake nju ya kutusaidia tushanjé. Kya shiye kufanya, ni kumwacha atusaidie.
w18.03 p. 26 par. 11
Disipline ile Jeova anatupachiaka inaonesha asema anatupenda
11 Kintu kya tatu, bale beko na responsabilité ya kupachiana disipline, sa vile bazazi na bazee mu kutaniko, banezi kufunda mambo ya mingi mu namna Jeova arimutendeaka Shebna. Mambo kani? Disipline ya Jeova inaonesha asema anachukiaka nzambi, lakini inaonesha tena asema anangaikiaka muntu ule arifanya nzambi. Kama weye muzazi ao muzee mu kutaniko unapenda kupachia mukristo mwenzako ao mutoto yako disipline, fwatirisha vile Jeova anafanyaka: Chukia bibaya bya ule muntu, lakini angariako na bizuri byake.—Yuda 22, 23.
Ma leson ya mu Bible
w06 1/12 p. 11 par. 2
Mawazo ya lazima ya mu kitabu kya Isaya—I
21:1—“Dezere ya mutoni munene” ile banataya mu iyi andiko irikuwaka fashi kani? Ata kama Babilone aikukuwaka karibu na mutoni moya ya munene, mu iyi andiko ile fashi ni Babilone. Lakini bariita Babilone vile nju, kila mwaka, mayi ya mu mutoni Efrate na Tigre irianzaka kuyala sana mule, na ile irianza kufanya ile fashi ikuwe tingi-tingi.
19-25 JANVIER
MAFUNDISHO YA LAZIMA YA MU BIBLE | ISAYA 24-27
“Uyu njo Mungu wetu!”
cl p. 15 par. 21
“Angaria! Uyu njo Mungu wetu!”
21 Eske, ushakonaka mutoto saa eko nambia barafiki yake na fieri asema: “Uyu njo baba yangu!”? Ni pamoya na batumishi ba Jeova, banekalaka na fieri nju Jeova ni Mungu wabo. Bible ishakutabiri asema kuko shiku ile baminifu batasemaka ivi: “Angaria! Uyu njo Mungu wetu!” (Isaya 25:8, 9) Kama unayuwa muzuri ma kalité ile Jeova eko nayo, utafikia kuona asema uko na Baba wa muzuri sana kupita ba baba bote.
w24.12 p. 6 par. 14
Mirakle ya mukate
14 Pale Yesu arisemaka tusali nju ya mukate yetu ya kila shiku, aritwambiaka tena tusali nju mapenzi ya Mungu ifanshike ku dunia sa vile iko nafanshika ku mbingu. (Mt. 6:9-11) Saa unashikia ile, ni nini njo inakukuya mu akiri? Bible inaonesha asema, Mungu anapenda mu dunia mukuwe byakurya bya mingi, tena bya butamu. Isaya 25:6-8, inaonesha asema, tutafuraiya byakurya bya mingi ile saa ufalme ya Jeova itanza kutawala dunia. Zaburi 72:16 inasema ivi: “Kutakuwa byakurya bya mingi sana ku dunia; na ku nchongo ya mirima byakurya bitayala sana.” Eske, na weye unapenda ile wakati ifike ata leo nju upike byakurya bile unapendaka ao nju ufunde namna ya kupika byakurya bile auyapikaka? Kutoshako ile, utafuraiya mantunda ya michi yako ya ma raisin ile uripanda. (Isa. 65:21, 22) Unawaza asema utakuwa we moya nju ya kufuraiya bile byote? Apana! Tutakuwa ba mingi sana.
w25.01 p. 28-29 par. 11-12
Bizuri bile tunapata nju Jeova anatupenda
11 Waza vile maisha yako itakuwa pa dunia mu paradi. Akutakuwa malari na lufu. (Isa. 25:8; 33:24) Jeova atafanshia kila muntu mambo ile eko nayo lazima. Utapenda kuyuwa sana nini? Ba nyama ao ba ndeke? Utapenda kufunda ku desiné, ao kupika gidar? Kusema tu bya kweri, tutakuwa na lazima ya bantu bale banayuwa ku desiné, kuyenga na bale banayuwa kurima. Tena, tutakuwa na lazima ya bantu ba kufanya ma kaji ingine ya kwachana-achana sa vile kupika byakurya, kutengeneza bintu, na bantu ba kufanya ma jardin ya muzuri. (Isa. 35:1; 65:21) Nju utaishi milele, utakuwa na saa ya mingi ya kufunda byote bile unapenda.
12 Tutafurai sana kupokelea bale batafufuka! (Mdo. 24:15) Waza tena vile utakuwa na furaa ya mingi sana ya kufunda nju ya Jeova saa utanza kwangaria bintu bya mingi bile ariumbaka. (Zb. 104:24; Isa. 11:9) Na furaa ile itapita byote, ni ya kumutumikia Jeova na konsianse ya muzuri! Eske utechika kupusa ile ma baraka yote nju tu ya ‘kufurahia kufanya nzambi mu minite kiloko’? Apana! (Ebr. 11:25) Tutechika kufanya byote bile Jeova analomba nju tu tupate ile ma baraka. Kumbuka asema, atutendeleaka kuchunga paradi milele! Shiku ni moya tu, itafika! Tutapata ile ma baraka yote nju Jeova anatupenda sana na aritutoweya mutoto yake!
Ma leson ya mu Bible
w15 15/12 p. 17 par. 1-3
Bible Tafsiri ya Ulimwengu Mupya ya mu anglais ile baritosha mu 2013
Nju ya nini bashakwanjika ma shapitre ya mingi sa vile bananjikaka ma poeme? Barianjikaka bipande bya mingi bya mu Bible sa vile bananjikaka ma poeme. Mu ma luga ya mingi leo, bananjikaka ma poeme mu ile banaita rime, ni kusema, ma letre ya ku mwisho ya ma fraze ile ishakufwatana, ile iko na son moya. Lakini, mu kiebré aina vile. Bo bananjikaka ivi: Banaoneshaka buzuri na bubaya bwa kintu ao bwa mambo moya ivi. Tena, banaoneshaka kintu na contraire yakyo. Njo pale, rime mu ma poeme ya kiebré aina mu ma letre ya ku mwisho ya ma fraze ile ishakufwatana, lakini iko mu namna mawazo ishakupangana muzuri.
Mu ma tradiksion ya nzamani ya Bible Tafsiri ya Ulimwengu Mupya, barianjikaka kitabu kya Yobu na kya Zaburi mu ma mistari-mistari ile banaita vers nju ya kuonesha asema, ni vile njo barianjikaka ku mwanzo nju ya kusaidia muntu aimbe bile bashakwanjika ao afanye resitasion. Ile namna ya kwanjika inasaidia muntu aone mawazo ya munene na aibambe mu akiri. Mu Tafsiri ya Ulimwengu Mupya ya mu anglais ile iritoka mu 2013, mu Mezali, Wimbo wa Sulemani na mu ma shapitre ingine ya mingi ya mu bitabu bya ba profete bashakupanga mianjiko mu mistari-mistari nju ya kuonesha asema bariianjikaka sa vile bananjikaka ma poeme na nju ya kusaidia muntu aone buzuri na bubaya bwa kintu ao bwa mambo moya ivi, na ayuwe kintu na contraire yakyo. Kwa mufano, mu Isaya 24:2, kila mustari inaonesha kintu na contraire yakyo. Na vile inafwatana, inasaidia kukazia asema akuna muntu ule anezi kukimbia ukumu ya Mungu. Ule arianjika ile andiko ashikupenda tu kurudiria-rudiria bintu, lakini aripenda tena kukazia message ya Mungu.
Mu kiebré, binekalaka nguvu kwachanisha poeme na ile banaita prose. Njo pale, kila tradiksion ya Bible inezi kukuwa na namna yake ya kwanjika na ya kupanga ma versé. Batradiktere njo banangariaka ni ma versé kani njo banezi kwanjika mu mistari-mistari ao mu ma vers. Ma versé ingine banayanjikaka mu prose, lakini inafananaka kiloko na poeme, na mu ile ma versé banatumikisha maneno ya mufano, ao banaonesha buzuri na bubaya bwa kintu ao bwa mambo moya ivi, nju ya kukazia mawazo fulani.
26 JANVIER–1 FÉVRIER
MAFUNDISHO YA LAZIMA YA MU BIBLE | ISAYA 28-29
Umutukuze Jeova na milomo yako pamoya na roo yako
ip-1 p. 299 par. 23
Isaya anatabiri ‘bya kushangaisha’ bile Jeova atafanya
23 Bakubwa ba kanisa ya Bayaudi banasema kama banayuwa sana mambo ya Jeova, lakini bashakumwacha. Beko nafundisha mawazo ya bongo nju ya bibaya na bizuri, kisha beko na defandre bile beko nasema. Kwa lakini, bitendo byabo bibaya binaonesha asema abana batumishi ba Mungu ba bya kweri. Njo pale, bantu ba mingi banafwata bitendo byabo na banamwacha Mungu. Jeova atatumikisha “mambo ya kushangaisha,” ao ‘bya kushangaisha’ nju ya kubaripisha. Ye moya anasema ivi: “Aba bantu bananichofeaka tu mu kusema na bananieshimiaka tu na milomo yabo, lakini roo yabo iko mbari na miye; na kuniongopa kwabo kunashimamia pa bile bantu beko nabafundisha. Njo pale, miye njo mitafanshia tena aba bantu mambo ya kushangaisha, bya kushangaisha na bya kushangaisha; na akiri ya bantu babo ba akiri itapotea, na ekima ya bale bantu ba ekima bataifuchika.” (Isaya 29:13, 14) Ekima na akiri ile bantu ba Yuda banasemaka kama beko nayo, yote itapotea saa Jeova ataongoza mambo mu namna ile itafanya Babilone itoshe ibada yabo ya bongo. Mambo ya vile iritokeaka tena mu siekle ya kwanza, ile saa bakubwa ba kanisa ya Bayaudi baripotosha taifa. Na bya vile bitafikiaka makanisa ya leo.—Matayo 15:8, 9; Waroma 11:8.
w21.05 p. 9 par. 7
Akuna kintu kile kinezi kukwaza muntu muzuri
7 Yesu ariwekaka peupe bongo bwa bakubwa ba ma kanisa ya mu wakati yake. Kwa mufano, arioneshaka vile bafarisayo barianzaka kukazia sana kunawa ku mikono kuliko kuchunga bazazi. (Mt. 15:1-11) Pengine mambo ile Yesu arisemaka irishangaishaka sana banafunzi bake. Njo pale, barimulizaka ivi: “Eske unayuwa asema bile urisema birikwaza bafarisayo?” Yesu aribajibu ivi: ‘Mumea yote ile Baba yangu wa ku mbingu ashikupanda bataitosha. Mubache. Ni ba biongozi bipofu. Njo pale, kama kipofu anaongoza kipofu, bote bawiri batangukia mu njimu.’ (Mt. 15:12-14) Yesu ashikwachake kusema kweri ata kama bakubwa ba makanisha abakufuraiaka bile arisemaka.
w24.06 p. 10 par. 8
Endelea kukuwa mukeni wa Jeova milele!
8 Muntu ule ‘anasemaka kweri mu roo yake’ anafwataka ma kanuni ya Jeova saa eko pa bantu na ata saa ile eko pa ye moya. (Isa. 29:13) Ashikalake mudanganyifu. Muntu ule eko mudanganyifu anawazaka asema ma kanuni ingine ya Jeova aina ya lazima. (Yak. 1:5-8) Pengine anezi kukatala kufwata bile Jeova anasema nju ya mambo moya ivi ile ye anaona asema aina ya lazima. Kisha kama anaona asema mambo ile eko nafanya aimuletee kintu kibaya, anezi kukatala tena kufwata ma kanuni ingine ya Mungu. Na ile itafanya ibada yake ikuwe ya bongo. (Muh. 8:11) Lakini, tunapenda kukuwa baminifu mu mambo yote.
Ma leson ya mu Bible
it “Ariel” par. 1; it “Ariel” Nim. 3
Ariel
(Ariel) [Fashi ya kumutolea Mungu ma sakrifise; ao, simba wa Mungu].
3. Njina ya mufano ile baripachiaka Yerusalemu mu Isaya 29:1, 2, 7. Tample ya Jeova irikuwaka mu Yerusalemu. Mu ile tample murikuwaka fashi ya kutoa ma sakrifise. Njo pale Yerusalemu irikuwa fashi ya kumutolea Mungu ma sakrifise. Tena, ile fashi irikuwa santre ya ibada safi ya Jeova. Lakini, mambo ile iko mu Isaya 29:1-4 iko naongopesha nju inaonesha asema mu 607 M.Y.A. basoda ba Babilone batalabisha Yerusalemu. Pale sasa, Yerusalemu itakuwa “fashi ya kutoa ma sakrifise,” ni kusema, Yerusalemu bataichoma, mutayala damu na maiti ya bantu bale batakufwa. Ma rezon ile inafanya bile byote bifike iko mu versé 9 tii na mu 16. Lakini, Isaya 29:7, 8 inaonesha asema mataifa ile itapenda kwalabisha Yerusalemu, aitaweza.
2-8 FÉVRIER
MAFUNDISHO YA LAZIMA YA MU BIBLE | ISAYA 30-32
Fuchama mu mabawa ya Jeova
w01 15/11 p. 16 par. 7
Tunezi kukimbiria kwa Jeova
7 Nju tunezi kukimbiria kwa Jeova, iyi maneno inatupachiaka nguvu: “Atakufunika na manyonya yake, na utakimbiria mu mabawa yake. Uaminifu yake itakuwa ngao ya munene na kibumbashi kya kuprotejé.” (Zaburi 91:4) Mungu anatuprotejaka sa vile ndeke anafunikaka batoto yake mu mabawa. (Isaya 31:5) Jeova ‘anatufunika na manyonya yake.’ Vile tunayuwa, “manyonya” ya ndeke njo mabawa yake. Ndeke anatumikishaka ile mabawa yake nju ya kufunika batoto yake kama kuko danger. Sa vile batoto ba ndeke, na shiye tuko mu manyonya ya mufano ya Jeova nju tushakukimbiria mu organizasion yake.—Rutu 2:12; Zaburi 5:1, 11.
w24.01 p. 24 par. 13
Jeova atakusaidia mu magumu
13 Mambo ile tunapashwa kufanya. Kumbuka asema muntu ni bantu. Kama uko tu pa we moya na aupendake kuwa na bengine, unezi kwanza kuwaza sana nju yako na nju ya magumu ile uko nayo. Na kuwaza sana vile, kunaweza kukusuma ubebe ma desizion ya mubaya. (Mez. 18:1) Saa moya ivi, kila muntu anapendaka kuwa pa ye moya, sirtu kama eko na magumu ya nguvu. Lakini, kama unarikaria pa we moya wakati mulefu, ile itaonesha asema aubebe na valere njia ile Jeova eko natumikisha nju ya kukusaidia. Njo pale, ata kama uko napita mu bya nguvu bya je, acha bantu ba mu famiye yako, barafiki yako na bazee bakusaidie. Ubaone sa vile njia ile Jeova eko natumikisha nju ya kukusaidia.—Mez. 17:17; Isa. 32:1, 2.
w23.10 p. 17 par. 19
Namna kani Jeova ‘atakupachia nguvu?’
19 Unezi kufanya nini nju tumaini yako ikuwe nguvu? Kwa mufano, kama uko na tumaini ya kuishi milele ku dunia, soma na uwaze sana nju ya mandiko ya mu Bible ile inaonesha vile paradi itakuwa. (Isa. 25:8; 32:16-18) Waza vile maisha itakuwa mu dunia ya sasa. Waza uko mule! Unaona nani? Unashikia sauti kani? Unarishikia je? Nju ufikie kuwaza muzuri nju ya vile maisha itakuwa mu dunia ya sasa, angaria mu bitabu byetu ma foto ile inaonesha vile paradi itakuwa. Ao angaria ma chansons originales sa vile Dunia Mupya Yenye Kuja, Iko Karibu Sana, ao Wazia ile Siku. Kama tunaendelea kuwaza sana nju ya tumaini ile tuko nayo ya kwingia mu dunia ya sasa, magumu ile tuko nayo leo tutaiona sa vile ‘ni ya mashiku kiloko tu na aina nguvu kuivumilia.’ (2 Ko. 4:17) Jeova atakupachia nguvu kupitia tumaini ile ashakukupachia.
Ma leson ya mu Bible
it “Mukate” par. 6
Mukate
Maana ya mufano. Mu Bible, terme “mukate,” iko na maana mingi ya mufano. Kwa mufano, Yoshua na Caleb bariambiaka batoto ya Israel asema bantu ba mu Kanaani barikuwa sa vile ‘mukate ku mancho yabo.’ Pengine ile inapenda kuonesha asema bitakuwa teketeke sana nju ya kubawina na ile itapachia nguvu batoto ya Israel. (Hes. 14:9) Zaburi 80:5 inasema ivi nju ya Jeova, Muchungaji wa batoto ya Israel: “Uribakurisha machozi yabo sa mukate.” Iko saa iyi maneno inapenda kuonesha uzuni ile Jeova arishikia nju bantu bake barimukosea. Tena, Isaya 30:20 inasema kama Jeova analetea bantu bake “mateso sa mukate na magumu sa mayi.” Pengine ile inapenda tu kuonesha sitwasion ile bantu bake batajikutamo saa ba enemi batajunguluka mukini, na ile itakuwa kwabo sa vile mukate na mayi.
9-15 FÉVRIER
MAFUNDISHO YA LAZIMA YA MU BIBLE | ISAYA 33-35
“Yeye njo anafanyaka utulizane”
w24.01 p. 22 par.7-8
Jeova atakusaidia mu magumu
7 Magumu. Saa tuko mu magumu ya nguvu, tunezi kurishikia, kuwaza ao kufanya mambo vile atufanyake uku kote. Saa moya unezi kushikia makari sana, saa ingine uzuni sana, na kurishikia bimoya ivi tu. Da Ana, ule turitaya ku mwanzo, arikuwa na ma santima ya kwachana-achana kisha lufu lwa bwana yake. Anasema ivi: “Ile saa mirianza kushikia sa vile minaishiwa, mirianzaka kuwaza tu nju ya mateso yangu. Tena, mirianzaka kushikia makari sana nju bwana yangu ariniacha.” Na kuongezeapo pa ile, da Ana arijishikia sa eko ye moya na birimufanya mubaya sana nju aripashwa kwanza sasa kubeba ma desizion nju ya mambo ile bwana yake Luis arianzaka kushimamia muzuri sana. Saa moya ivi, arijishikiaka sa vile eko mu mpepo ya nguvu sana mu kachi-kachi ya mutoni ya munene. Sasa, Jeova anatusaidiaka je saa tuko mu bya nguvu?
8 Vile Jeova anatusaidiaka. Anatwambia asema, atatusaidia nju tutulizane. (Soma Isaya 33:6.) Saa kuko mpepo ya mingi pa mayi, bato inezi kwanza kwenda uku na uku. Sasa nju ya kusaidia ile bato, kunekalaka bintu bimoya ivi ku ma ngambo yote ya bato bile bishakushuka tii na mu mayi, bile binasaidiaka bato ishitenke-tenke sana. Ile inafanyaka voyage ipite muzuri. Lakini bintu bya mingi bile binasaidiaka bato ishende uku na uku, binatumikaka muzuri kama bato iko natembea. Njo pamoya na Jeova, atatusaidia tushitenke-tenke ao tutulizane kama atuchoke na kama tunabakia baminifu mu magumu.
w21.02 p. 29 par. 10-11
Namna ya kuchunga furaa mu magumu
10 Kya kufanya: Umulombe Jeova ekima. Nju ya kuvumilia magumu pashipo kupotesha furaa, umulombe Jeova akupachie ekima nju ubebe ma desizion ya muzuri. (Soma Yakobo 1:5.) Tunapashwa kufanya nini kama tunaona asema Jeova anakawia kujibia sala yetu? Yakobo anasema kama tunapashwa ‘kwendelea kumulomba’ Mungu. Ata tunamulomba Jeova ekima mala ngapi, ye ashituchokake na ashitatompola. Kama tunamulomba Jeova atupachie ekima ile itatusaidia tuvumilie magumu, atatupachia ayo na roo moya. (Zb. 25:12, 13) Anaonaka magumu yetu, binamulumaka ku roo saa tuko nateswa, na anapendaka sana kutusaidia. Auone asema ile inatuletea furaa! Sasa, Jeova anatupachiaka ekima je?
11 Jeova anatupachiaka ekima kupitia Sauti yake. (Mez. 2:6) Nju tupate ile ekima, tunapashwa kufunda Sauti yake na bitabu byetu bile biko nasemea Bible. Lakini, kutoshako kongeza konesanse, tunapashwa kufanya kintu kingine. Tunapashwa kutumikisha mambo ile tuko nafunda. Yakobo arianjikaka ivi: “Mushikuwe tu ba kushikia sauti . . . Lakini, mukuwe tena bale beko naitumikisha.” (Yak. 1:22) Kama tunatumikisha mashauri ya Mungu, tutakuwa bantu ba amani, bantu bale beko na mawazo ya muzuri, na tutakuwa bantu bale beko na roo ya buluma. (Yak. 3:17) Ile yote, itatusaidia tuvumilie magumu pashipo kupotesha furaa yetu.
ip-1 p. 352-355 par. 21-22
“Na akuna muntu ata moya atasema: ‘Niko malari.’”
21 Profesi ya Isaya iko nafanshika na leo. Leo, batumishi ba Jeova bashakupona kiroo. Abana tena mu butumwa bwa mafundisho ya bongo sa vile ame aikufwake, ba mungu ba tatu mu mungu moya, na moto ya mateso. Mafundisho ile beko napata, inabasaidiaka bashikuwe na bitendo bibaya na buyuwe namna ya kubeba ma desizion ya muzuri. Na kupitia lufu lwa Yesu, beko safi ku mancho ya Mungu na beko na konsianse ya muzuri. (Wakolosai 1:13, 14; 1 Petro 2:24; 1 Yohana 4:10) Kupona kwabo kwa kiroo kunabasaidiaka bakuwe na santé ya muzuri. Kwa mufano, nju banaepuka kufanya busharati na kufuta tumbako, ile inabasaidia bashipate ma malari sa vile sida ao kansere.—1 Wakorinto 6:18; 2 Wakorinto 7:1.
22 Tena, mambo ile iko mu Isaya 33:24 itafanshika kisha Armagedon, mu dunia ya sasa. Saa ufalme ya Jeova itanza kutawala dunia, bantu bote batakuwa na santé ya muzuri kimwili na kiroo. (Ufunuo 21:3, 4) Kisha kutosha iyi dunia ya Shetani, mu dunia mutafanshika ma mirakle ya mingi sa ile Yesu arifanyaka pale arikuwaka pa dunia. Ba bifopu bataona, ba biziwi batashikia na ba bilema batatembea! (Isaya 35:5, 6) Bale bote batapita bajima ku Armagedon, batakuwa na kaji ya munene sana ya kugeuza iyi dunia ikuwe paradi.
Ma leson ya mu Bible
w23.05 p. 15 par. 8
Endelea kutembea mu “njia ya butakatifu”
8 Bengine banezi kusema ivi: ‘Bile byote ni bya bien. Lakini, mambo ile irifikiaka Bayaudi nzamani, eske inatwangaria shiye leo?’ Ndiyo, nju mu namna ya mufano, tuko natembea mu “njia ya butakatifu.” Ata kama tuko na tumaini ya kuishi ku mbingu ao apa pa dunia, shiye bote tunapashwa kubakia mu “njia ya butakatifu” nju itatusaidia twendelee kumwabudu Jeova sasa na mu mashiku ya ku mbele, saa ufalme yake itafanya dunia ikuwe ya muzuri sana. (Yoh. 10:16) Kwanzia 1919 K.Y.K., ma milion ya banaume, banamuke, na batoto banatoka mu Babilone mukubwa, ni kusema, makanisa yote ya bongo. Bashakwanza kutembea mu njia ya mufano, na weye uko mu ile njia. Bantu barianza kutembea mu ile njia kushakupita miaka 100 ivi, lakini, ile njia barikuwa bashakwanzaka kuitengeneza nzamani sana.
16-22 FÉVRIER
MAFUNDISHO YA LAZIMA YA MU BIBLE | ISAYA 36-37
Bile urishikia bishikongopeshe
it “Ezekia” Nim. 1 par. 14
Ezekia
Senakeribe arishinda kubamba Yerusalemu. Vile Ezekia ariwazia, Senakeribe aridesidé kuya kubamba Yerusalemu. Wakati basoda barikuwa bashakujunguluka mukini ya Lakishi, Senakeribe aritumaka basoda bake bengine nju baambie bantu ba mu Yerusalemu barilete tu lwabo kwasho kupikana. Rabshaké (ile aina njina yake ya kizarikio, lakini ni titre ya busoda), arianzaka kusema muzuri sana kiebré na ye njo arishimamiaka kile kinkunji kya bantu bale Senakeribe aritumaka. Arimushushiaka eshima Ezekia na arimuchokozaka Jeova. Arisemaka na kiburi asema Jeova ashitaweza kusové Yerusalemu sa vile ba mungu ba ma inchi ingine nabo abakuwezake kusové ma inchi yabo mu mikono ya mufalme wa Asiri.—2Fa 18:13-35; 2Ny 32:9-15; Isa 36:2-20.
ip-1 p. 387 par. 10
Imani ya mufalme inaripa
10 Tena, Rabshaké anaambia Bayaudi asema basoda babo ba mu Yerusalemu beko tu bule. Kisha, anasema ivi na kiburi: “Mitakupachia ba sheval 2 000, na tutaona kama utapata bantu ba kupandapo.” (Isaya 36:8) Eske, kya lazima ni kukuwa na basoda bale banayuwa kupanda pa ba sheval? Apana, nju wokovu ya Yuda aishimamie pa kukuwa na basoda ba mingi. Mezali 21:31 inasema ivi: “Sheval banamutayarishaka nju ya shiku ya nvita, lakini Jeova njo anekalaka na sové.” Kisha Rabshaké arisemaka kama basoda ya Asiri njo beko na baraka ya Jeova, apana Bayaudi. Selon yeye, kama abakukuwa na baraka ya Jeova, abakufya kubamba mikini ingine ya mingi vile mu Yuda.—Isaya 36:9, 10.
ip-1 p. 388 par. 13-14
Imani ya mufalme inaripa
13 Mu kusema kwake, Rabashaké anatosha tena kintu kingine. Anambia Bayaudi asema bashimwaminie Ezekia ata kama anasema Jeova njo atabasové. Anakumbusha Bayaudi asema ba mungu ba Samari abakufanya kintu nju basoda ya Asiri barifikia kubamba ma kabila 10. Ashikwishia pale, aribauliza ivi: ‘Ba mungu ba Amat na Arpad beko wapi? Ba mungu ba Sefarvaim beko wapi? Eske, bariwezaka kusové Samari mu mikono yangu?’—Isaya 36:18-20.
14 Lakini, kintu kimoya kile Rabshaké ashikuona ni kya kusema, Samari barialabisha nju irimwacha Jeova. Yerusalemu yo irikuwa ikingari mu mikono ya Jeova kupitia mufalme Ezekia. Ba mungu ba bongo ba mu Samari abakukuwa na nguvu ya kusové ile ma kabila 10. (2 Wafalme 17:7, 17, 18) Lakini, wakati Ezekia arianza kutawala, Yerusalemu iriacha kwabudu ba mungu ba bongo. Irianza sasa kumutumikia Jeova. Bantu batatu bale Ezekia aritumaka nju bakutane na Rabshaké abakujiangaishake ata nju ya kumujibu Rabshaké. Isaya 36:21 inaonesha asema baribakia kimya na abakumujibu ata kintu kimoya, nju mufalme aribambiaka bashimujibu. Eliakim, Shebna na Yoa barienda kwa mufalme Ezekia nju ya kumupachia rapor ya bile Rabshaké arisema.—Isaya 36:22.
Ma leson ya mu Bible
it “Kroshé” par. 4
Kroshé
Jeova arimwambia ivi mufalme Senakeribe wa Asiri: “Mitaweka kroshé yangu ku mpua yako na nkamba yangu pa kachi-kachi ya milomo yako, na mitakurudisha mu njia ile urikuyiya.” (2Fa 19:28; Isa 37:29) Jeova arifanya Senakeribe aache Yerusalemu na arudie ku mukini ya Ninive, na kule batoto yake banaume barimuwaka. (2Fa 19:32-37; Isa 37:33-38) Pale Jeova arisema kama ataweka nkamba mu kinywa kya baadui, aripenda kuonyesha asema atanza kubaongoza bote sa vile banaongozaka sheval na nkamba.—Isa 30:28.
23 FÉVRIER–1 MARS
MAFUNDISHO YA LAZIMA YA MU BIBLE | ISAYA 38-40
“Sa vile muchungaji, atachunga muzuri kinkunji kyake”
w23.02 p. 2-3 par. 3-4
Mambo ile Bible inatufundisha nju ya mwenye nayo
3 Soma Isaya 40:8. Tangu nzamani, Bible ishakupachia bantu ba mingi mashauri ya muzuri ile iko nabaongoza mu maisha. Ile iriwezekana je? Ile ni ulizo ya muzuri nju barianjikaka mbele Mandiko pa bintu bile binezi kwalabika mbio. Njo pale leo, atuna ata dokima moya ya ile mandiko ya ku mwanzo-mwanzo. Lakini, Jeova ariongoza bantu fulani bafanye ma kopi ya ile mandiko takatifu. Ata kama bale barifanya ile ma kopi abakukuwa bakamilifu, barifanya yabo yote nju ya kukuwa bangalifu sana. Kwa mufano, muntu moya, arisemaka ivi nju ya mandiko ya kiebré: “Mu bitabu byote bya nzamani sana, akuna kitabu sa Bible kile barianjikaka muzuri kwashipo kushanjé mawazo ile iko ndani.” Njo pale, ata kama barianjikaka Bible nzamani pa bintu bile binezi kwalabika mbio, na ata kama bale barifanyaka ma kopi ya Bible abakukuwa bakamilifu, tuko sire asema mambo yote ile iko mu Bible ile tuko nayo leo, ni mawazo ya Jeova, mwenye Bible.
4 Jeova njo anatupachia “kado yote ya muzuri na ya kukamilika.” (Yak. 1:17) Mu ma kado ya muzuri sana ile Jeova ashakutupachia, muko na Bible. Vile tu tunayuwaka, kama muntu anatupachia kado, ile inaonesha asema anatupenda na anayuwa bintu bile tuko nabyo lazima. Ni pamoya na Jeova, ule aritupachia Biblia. Kama tunangaria muzuri kado ya Bible ile aritupachia, tutayuwa mambo ya mingi nju yake. Tutaona tena asema anatuyuwa muzuri na anayuwa muzuri sana bintu bile tuko nayo lazima. Mu iyi abari, tutaona vile Bible inaonesha waji asema Jeova eko na iyi ma kalité tatu: Ekima, aki, na mapendo. Tuone mbele vile Bible inaonesha waji asema Mungu eko na ekima.
cl p. 70 par. 7
Nguvu ya kuprotejé—‘Kwa Mungu njo tutakimbiria’
7 Pale Jeova anajikomparé na muchungaji, anapenda kutufanya tukuwe sire asema atatuprotejé. (Ezekieli 34:11-16) Mu shapitre 2 murikuwa andiko ya Isaya 40:11 ile inasema ivi nju ya Jeova: “Sa vile muchungaji, atachunga muzuri kinkunji kyake. Atatumikisha mukono yake nju ya kuweka batoto ba nkondolo fashi moya na atababeba mu kilari kyake.” Mutoto ya nkondolo arikuwa nafika je mu kilari kya muchungaji, mu mufuko ya nguo yake? Ule nkondolo arikuwa namuchofea polepole muchungaji, na arikuwa napika-pika na kichwa kyake mukulu ya muchungaji nju amwangarieko. Ile saa muchungaji ariona vile, aripasha kukunjama, kumunyangula polepole na kumuweka mu kilari kyake. Ile mufano inaonesha muzuri vile muchungaji wetu mukubwa anapendaka kutuprotejé!
w18.01 p. 8 par. 4-6
‘Anamupachiaka nguvu muntu ule ashakuchoka’
4 Soma Isaya 40:26. Akuna muntu ata moya ule anaweza kubalula ma nyota yote ile iko mu mbingu. Bantu ba sianse banasema kama galaksi yetu, ile banaita voie lactée, inezi kuwa na ma nyota 400 miliare. Lakini kya kushangaisha, Jeova ashakupachia kila nyota njina ao sinye fulani. Ile inatufundisha nini? Kama Jeova anangaikiaka biumbe byake bile abina na bujima, waza sasa vile anakuonaka weye ule uko namutumikia nju unamupenda! (Zb. 19:1, 3, 14) Baba yetu Jeova anakuyuwa inje na ndani. Shi ata Bible inaonesha kama ‘na ma nywele ya ku bichwa byetu, anaibalulaka yote!’ (Mt. 10:30) Na muntu moya, mu bale barianjikaka Zaburi, anatwambia ivi: “Jeova anayuwa bile biko nafikia bantu bale abana na nkosa.” (Zb. 37:18) Anayuwa mateso ile uko napata, na anaweza kukupachia nguvu ya kuvumilia.
5 Soma Isaya 40:28. Nguvu yote inatoka kwa Jeova. Kwa mufano, waza mbele nju ya nguvu ile yuwa iko nayo. Muntu moya wa sianse, ule njina yake ni David Bodanis, arisemaka ivi: “Bwingi bwa nguvu ile yuwa inatoshaka mu segonde moya iko pamoya na bwingi bwa nguvu ile ma mamilire ya ma bombe atomike inatoshaka.” Mutu mwingine wa sianse arisema kama “bwingi bwa nguvu ile yuwa inatoshaka mu segonde moya, inezi kupachia bantu courant mu miaka 200 000”! Tuko sire asema Jeova, ule anapachiaka yuwa nguvu, atatupachia nguvu ile tuko nayo lazima nju ya kuvumilia mateso yote.
6 Soma Isaya 40:29. Kumutumikia Jeova kunaletaka furaa ya mingi. Yesu ariambiaka banafunzi bake ivi: “Mubebe muchi yangu ya kubebea bujito.” Na aribambiaka tena ivi: “Mutapata kitulizo. Nju muchi yangu ya kubebea bujito aina bujito, na bujito bwangu buko bupepelo.” (Mt. 11:28-30) Iyi mambo ni ya bya kweri! Saa moya, tunezi kushikia muchoko sana saa tuko nenda ku mikutano ao mu maubiri. Lakini tunarishikiaka je saa tunarudia? Tunapataka nguvu na ile inatusaidiaka tukuwe tayari nju ya kuvumilia magumu ya maisha. Auone asema muchi ya Yesu ya kubebea bujito aina ata bujito?
Ma leson ya mu Bible
ip-1 p. 400 par. 7
“Tuliza bantu bangu”
7 Ile profesi aikutimizikaka tu paka mu siekle ya 6 M.Y.A. wakati ya kurudishwa. Iritimizika na mu siekle ya 1 K.Y.K. Yohana mubatizaji njo arikuwa sauti ya muntu ule eko nalalamika mu dezer, vile Isaya 40:3 inaonesha. (Luka 3:1-6) Roo takatifu irimusaidia Yohana aone kama ile mambo inamwangaria na yeye. (Yohana 1:19-23) Kwanzia mu mwaka ya 29 K.Y.K., Yohana aritayarishia Yesu Kristo njia. Mambo ile Yohana arianza kutangaza, irisaidia bantu banze kumuchunga Masiya ule barilakaka. Lakini na bo, baripasha kumushikia na kumufwata. (Luka 1:13-17, 76) Kupitia Yesu, Jeova aripasha kufanya bantu bale baritubu batoke mu butumwa bwa nzambi na lufu. Ile inawezekana tu kupitia ufalme yake. (Yohana 1:29; 8:32) Maneno ya Isaya iritimizika mu kipimo kinene ile saa bantu ba mu Israel ya kiroo, bale baribakiaka, baritoka mu Babilone mukubwa mu 1919 na baribarudisha mu ibada safi.