-
Hesabu 28:26-31Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
26 “‘Siku ya matunda ya kwanza yenye kukomaa,+ wakati munamutolea Yehova toleo la nafaka mupya,+ mutafanya mukusanyiko mutakatifu katika sikukuu yenu ya majuma.+ Hamupaswe kufanya kazi yoyote ya nguvu.+ 27 Mutatoa kuwa toleo la kuteketezwa kwa ajili ya harufu ya kumupendeza* Yehova: ngombe-dume wawili wadogo, kondoo-dume mumoja, na wana-kondoo dume saba (7) kila mumoja wa mwaka mumoja,+ 28 na toleo lao la nafaka la unga muzuri wenye kuchanganywa na mafuta, sehemu tatu za kumi (3/10) kwa ajili ya kila ngombe-dume, na sehemu mbili za kumi (2/10) kwa ajili ya ule kondoo-dume mumoja, 29 sehemu moja ya kumi (1/10) kwa ajili ya kila mwana-kondoo dume kati ya wale wana-kondoo dume saba (7), 30 na pia mwana-mbuzi mumoja ili kufunika zambi kwa ajili yenu.+ 31 Mutatoa vitu hivyo zaidi ya toleo la kuteketezwa lenye linatolewa kwa ukawaida na toleo lake la nafaka. Watakuwa wanyama wenye hawana kasoro,+ pamoja na matoleo yao ya kinywaji.
-