Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Karibu
Hii ni chombo ya kukusaidia kutafuta habari mu vichapo vya Mashahidi wa Yehova mu luga mbalimbali.
Kama unapenda kuchukua kichapo fulani, tafazali fungua jw.org.
  • Leo

Siku ya Tano, 12 Mwezi wa 9

Tamasha ya ulimwengu huu inabadilika.​—1 Ko. 7:31.

Ujiendeshe mu njia yenye itafanya wengine waone kama uko mutu mwenye usawaziko. Ujiulize hivi: ‘Watu wananionaka kuwa mutu mwenye usawaziko, mwenye kujipatanisha na hali, na mwenye kuachilia mambo kwa kupenda? Ao wananionaka kuwa mutu mugumu, mukali, ao wa kichwa nguvu? Ao nasikilizaka wengine na kufuata mawazo yao kama ni lazima?’ Kama tunaendelea kuwa na usawaziko, tutaonyesha kama tuko namuiga Yehova na Yesu. Tunapaswa kuwa na usawaziko wakati hali inabadilika mu maisha yetu. Ile mabadiliko inaweza kufanya tupate magumu yenye hatuyawaziaka hata kidogo. Kwa mufano tunaweza kugonjwa sana bila kutazamia, ao mabadiliko ya kiuchumi ao ya serikali yenye haitazamiwe fasi kwenye tunaishi, inaweza kufanya maisha yetu ikuwe nguvu sana. (Muh. 9:11) Inaweza pia kuwa nguvu kwetu wakati tengenezo inabadilisha mugao wetu wa utumishi. Hata hali ibadilike namna gani, unaweza kujipatanisha nayo kwa kufanya hii mambo ine: (1) Ukubali mabadiliko, (2) ufikirie mambo ya sasa hapana ya zamani, (3) ujikaze kuona mambo ya muzuri mu maisha yako na (4) usaidie wengine. w23.07 21-22 fu. 7-8

Tuchunguze Maandiko Kila Siku—2025

Siku ya Posho, 13 Mwezi wa 9

Wewe ni mutu mwenye samani sana.​—Da. 9:23.

Wakati nabii Danieli alikuwa angali kijana, Wababiloni walimufunga na kumupeleka mu muji wao wenye ulikuwa mbali na Yerusalemu. Lakini, Danieli alishangaza wale wenye walimufunga. Waliona “kile chenye [kinaonekana] kwa macho,” ni kusema, waliona kama Danieli “hakukuwa na kasoro yoyote, alikuwa na sura ya muzuri,” na kama alitoka mu familia yenye kuheshimiwa. (1 Sa. 16:7) Njo maana, Wababiloni walimuzoeza ili aanze kutumika mu nyumba ya Kifalme. (Da. 1:3, 4, 6) Yehova alimupenda Danieli juu alichagua kuwa mushikamanifu kwake. Kwa kweli, inawezekana Danieli alikuwa tu na miaka 20 hivi wakati Yehova alimuona kuwa mwenye haki, sawa vile Noa na Yobu, wanaume wenye walimutumikia kwa uaminifu kwa miaka mingi. (Mwa. 5:32; 6:9, 10; Yob. 42:16, 17; Eze. 14:14) Na Yehova aliendelea kumupenda Danieli mu maisha yake yote yenye ilikuwa ya murefu na ya maana.​—Da. 10:11, 19. w23.08 2 fu. 1-2

Tuchunguze Maandiko Kila Siku—2025

Siku ya Yenga, 14 Mwezi wa 9

Elewa kwa ukamili upana na urefu na urefu kuenda juu na urefu kuenda chini.​—Efe. 3:18.

Wakati unataka kuamua ikiwa utauza nyumba fulani ao hapana. Itakuwa lazima uchunguze kila sehemu ya nyumba yenye unapenda kuuza. Hapana kupitia video lakini kwa kufika mahali kwenye kuko ile nyumba. Tunaweza pia kufanya vile wakati tuko nasoma na kujifunza Biblia. Kama unaisoma mbiombio pengine utajifunza tu kweli za musingi, ni kusema “mambo ya musingi ya maneno matakatifu ya Mungu.” (Ebr. 5:12) Kuliko kufanya vile, sawa vile mutu anaweza kufanya kuhusu nyumba, ingia “ndani” ili uchunguze mambo yote ya maana. Njia ya muzuri ya kujifunza Biblia ni kuona namna sehemu zake mbalimbali zinapatana. Usitafute tu kujua ni kweli gani unaamini, lakini pia juu ya nini unaziamini. Ili kuelewa Neno ya Mungu kwa undani kabisa, unapaswa kujifunza mafundisho mazito ya Biblia. Mutume Paulo alitia moyo ndugu na dada zake wajifunze Neno ya Mungu kwa uangalifu ili waweze “kuelewa kwa ukamili upana na urefu na urefu kuenda juu na urefu kuenda chini” wa kweli. Na ile ingefanya wafikie kuwa “na mizizi na kufanywa imara” katika imani yao. (Efe. 3:14-19) Siye pia tunapaswa kufanya vile. w23.10 18 fu. 1-3

Tuchunguze Maandiko Kila Siku—2025
Karibu
Hii ni chombo ya kukusaidia kutafuta habari mu vichapo vya Mashahidi wa Yehova mu luga mbalimbali.
Kama unapenda kuchukua kichapo fulani, tafazali fungua jw.org.
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine