Siku ya Kwanza, 28 Mwezi wa 7
Ule mwenye kuwa katika umoja na ninyi ni mukubwa kuliko ule mwenye kuwa katika umoja na ulimwengu.—1 Yo. 4:4.
Wakati unaogopa, utafakari juu ya mambo yenye Yehova atafanya wakati wenye kuya wakati Shetani hatakuwa tena. Onyesho fulani ku mukusanyiko wa eneo wa 2014, ulionyesha baba fulani mwenye alikuwa nazungumuza na familia yake juu ya namna 2 Timoteo 3:1-5 inaweza kusomwa ikiwa ilikuwa inatabiri namna mambo itakuwa mu Paradiso: “Mu ulimwengu mupya mutakuwa nyakati za furaha. Kwa maana watu watakuwa wenye kupendana, wenye kupenda mambo ya kiroho, wenye kiasi, wanyenyekevu, wenye kumusifu Mungu, wenye kutii wazazi, wenye shukrani, washikamanifu, wenye kupenda sana watu wa familia yao, wenye kupenda makubaliano, wenye kusema mambo ya muzuri juu ya wengine, wenye kujizuia, wapole, wenye kupenda wema, wenye kutumainika, wenye kuwa tayari kusikia, wenye kujishusha, wenye kumupenda Mungu kuliko kupenda raha, wenye wanachochewa na ushikamanifu kwa Mungu; na weye ushikamane na watu wa namna ile.” Unazungumuzaka na watu wa familia yako ao waamini wenzako juu ya namna maisha itakuwa mu ulimwengu mupya? w24.01 6 fu. 13-14
Siku ya Pili, 29 Mwezi wa 7
Nimekukubali.—Lu. 3:22.
Inatia moyo sana kujua kama Yehova anakubali watu wake wakiwa kikundi! Biblia inasema: “Yehova anafurahia watu wake.” (Zb. 149:4) Lakini, wakati fulani kuko Wakristo wenye wanaweza kuvunjika moyo na kujiuliza hivi: ‘Yehova ananikubali na miye?’ Watumishi fulani waaminifu wa Yehova wa zamani walijiuliza pia vile wakati fulani. (1 Sa. 1:6-10; Yob. 29:2, 4; Zb. 51:11) Biblia inaonyesha wazi kama wanadamu wenye hawakamilike wanaweza kukubaliwa na Yehova. Namna gani? Tunapaswa kukubali Yesu Kristo na kubatizwa. (Yoh. 3:16) Kwa kufanya vile tunaonyesha waziwazi kama tumetubu zambi zetu na tumemuahidi Mungu kama tutafanya mapenzi yake. (Mdo. 2:38; 3:19) Yehova anafurahi sana wakati tunafanya ile mambo ili kuwa marafiki wake wa karibu. Wakati tunaendelea kufanya yetu yote ili kuheshimia naziri yetu ya kujitoa kwake, Yehova anatukubali na kutuona kuwa marafiki wake.—Zb. 25:14. w24.03 26 fu. 1-2
Siku ya Tatu, 30 Mwezi wa 7
Hatuwezi kuacha kusema juu ya mambo yenye tumeona na kusikia.—Mdo. 4:20.
Tunaweza pia kuiga wanafunzi wa Yesu kwa kuendelea kuhubiri hata kama wenye mamlaka wanatukataza kufanya vile.Tuko hakika kama Yehova atatusaidia kutimiza utumishi wetu. Kwa hiyo, umuombe Yehova uhodari na hekima na akusaidie ili uvumilie magumu. Wengi kati yetu wako napambana na magumu ya kimwili ao ya kihisia, magumu ya kupoteza mupendwa wao, magumu fulani mu familia, mateso, ao magumu ingine. Na mambo sawa vile, magonjwa ya kuambukiza na vita imefanya ikuwe nguvu kuvumilia magumu mingi kati ya ile. Umufungulie Yehova moyo wako. Umuambie hali yako sawa vile tu unaweza kumuambia rafiki yako wa karibu sana. Ukuwe hakika kama Yehova “atatenda kwa ajili yako. (Zb. 37:3, 5) Kuendelea kusali kutakusaidia “uvumilie chini ya taabu.” (Ro. 12:12) Yehova anajua mambo yenye watumishi wake wako napambana nayo. “Anasikia kilio chao cha kuomba musaada.”—Zb. 145:18, 19. w23.05 5-6 fu. 12-15