-
Mwanzo 8:20, 21Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
20 Kisha Noa akamujengea Yehova mazabahu+ na akakamata wamoja kati ya wanyama wote wenye kuwa safi na wamoja kati ya viumbe vyote vyenye kuruka vyenye kuwa safi+ na akatoa matoleo ya kuteketezwa juu ya ile mazabahu.+ 21 Na Yehova akaanza kusikia harufu ya muzuri.* Kwa hiyo Yehova akasema katika moyo wake: “Sitalaani tena* inchi+ hata kidogo kwa sababu ya mwanadamu, kwa maana muelekeo wa moyo wa mwanadamu ni mubaya kuanzia ujana wake;+ na mimi sitapiga na kuua tena kila kitu chenye uzima kama vile nimefanya.+
-
-
Hesabu 15:2, 3Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
2 “Sema na Waisraeli na uwaambie, ‘Wakati mutaingia mwishowe katika inchi yenye ninawapatia muishi ndani yake,+ 3 na kumutolea Yehova toleo lenye linatolewa kwa njia ya moto kutoka katika mifugo ao kutoka katika kundi—ikuwe toleo la kuteketezwa+ ao zabihu ya kutimiza naziri ya pekee ao toleo la kujipendea+ ao toleo lenye linatolewa wakati wa sikukuu zenu za vipindi,+ ili kumutolea Yehova harufu ya kumupendeza*+—
-