23 Kisha wakati murefu, mufalme wa Misri akakufa,+ lakini Waisraeli wakaendelea kulia kwa maumivu kwa sababu ya utumwa na kutoa sauti za malalamiko, na kilio chao cha kuomba musaada kikaendelea kupanda mupaka kwa Mungu wa kweli.+
7 Yehova akaongeza kusema: “Kwa kweli nimeona mateso ya watu wangu wenye wako Misri, na nimesikia kilio chao kwa sababu ya wale wenye kuwalazimisha kufanya kazi; ninajua muzuri maumivu yenye wako nayo.+