-
Hesabu 21:21-24Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
21 Sasa Israeli akatuma wajumbe kwa Sihoni, mufalme wa Waamori, ili wamuambie:+ 22 “Uturuhusu tupite katika inchi yako. Hatutageuka na kuingia katika shamba ao shamba la mizabibu. Hatutakunywa maji ya kisima chochote. Tutatembea katika Barabara ya Mufalme mupaka wakati tutakuwa tumepita katika eneo lako.”+ 23 Lakini Sihoni hakuruhusu Israeli apitie katika eneo lake. Tofauti na hiyo, Sihoni akakusanya watu wake wote na kuenda kushambulia Israeli katika jangwa na akafika Yahazi na kuanza kupigana na Israeli.+ 24 Lakini Israeli akamushinda kwa upanga+ na akakamata inchi yake+ kuanzia Arnoni+ mupaka Yaboki,+ karibu na Waamoni, kwa sababu muji wa Yazeri+ uko kwenye mupaka wa eneo la Waamoni.+
-