Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 8:18
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 18 kumbuka kwamba Yehova Mungu wako ndiye anakupatia nguvu ya kupata utajiri,+ ili atimize agano lake lenye aliapia mababu zako, kama vile leo.+

  • Kumbukumbu la Torati 28:12
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 12 Yehova atakufungulia depo yake ya muzuri, mbingu, ili kupatia inchi yako mvua kwa wakati wake+ na ili kubariki mambo yote yenye unafanya. Utakopesha mataifa mengi, lakini wewe mwenyewe hautahitaji kukopa.+

  • 2 Mambo ya Nyakati 1:11, 12
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 11 Kisha Mungu akaambia Sulemani: “Kwa sababu hii ndiyo tamaa ya moyo wako na haukuomba mali, utajiri, na heshima ao kifo cha* wale wenye wanakuchukia, ao haukuomba maisha ya murefu,* lakini umeomba hekima na ujuzi ili uhukumu watu wangu wenye nimekufanya kuwa mufalme juu yao,+ 12 utapewa hekima na ujuzi; lakini nitakupatia pia mali na utajiri na heshima vyenye hakuna mufalme yeyote mwenye amevipata mbele yako na hakuna mufalme yeyote kisha wewe mwenye atavipata.”+

  • Yobu 42:12
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 12 Basi Yehova akabariki miaka ya mwisho ya maisha ya Yobu kuliko mwanzo,+ na Yobu akakuwa na kondoo elfu kumi na ine (14 000), ngamia elfu sita (6 000), ngombe elfu mbili (2 000) wenye kufungwa wawili-wawili, na punda-dike elfu moja (1 000).+

  • Mezali 10:22
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 22 Baraka ya Yehova ndiyo inamufanya mutu kuwa tajiri,+

      Naye haongeze maumivu* yoyote pamoja nayo.

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine