-
1 Wafalme 8:14-21Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
14 Kisha mufalme akageuka na kuanza kubariki kutaniko lote la Israeli wakati kutaniko lote la Israeli lilikuwa limesimama.+ 15 Akasema: “Yehova Mungu wa Israeli asifiwe, yeye mwenye kwa kinywa chake mwenyewe alimuahidi baba yangu Daudi, na kwa mukono wake mwenyewe ametimiza, na kusema, 16 ‘Kuanzia siku nilitosha watu wangu Israeli katika Misri, sikuchagua muji katika makabila yote ya Israeli ili kujenga ndani nyumba kusudi jina langu likae ndani,+ lakini nimemuchagua Daudi akuwe juu ya watu wangu Israeli.’ 17 Na ilikuwa tamaa ya moyo wa baba yangu Daudi kujenga nyumba kwa ajili ya jina la Yehova Mungu wa Israeli.+ 18 Lakini Yehova akamuambia baba yangu Daudi, ‘Ilikuwa tamaa ya moyo wako kujenga nyumba kwa ajili ya jina langu, na ulifanya muzuri kutamani jambo hilo katika moyo wako. 19 Hata hivyo, hautajenga nyumba hiyo, lakini mwana wako mwenye utazaa* ndiye atajenga nyumba hiyo kwa ajili ya jina langu.’+ 20 Yehova ametimiza ahadi yenye alitoa, kwa maana nimechukua nafasi ya baba yangu Daudi na ninakaa kwenye kiti cha ufalme cha Israeli, kama vile Yehova aliahidi. Nimejenga pia nyumba kwa ajili ya jina la Yehova Mungu wa Israeli+ 21 na nimetayarisha mahali pale kwa ajili ya lile Sanduku lenye ndani yake muko agano+ lenye Yehova alifanya na mababu zetu wakati alikuwa anawatosha katika inchi ya Misri.”
-