-
1 Wafalme 8:27-30Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
27 “Lakini je, kweli Mungu atakaa katika dunia?+ Angalia! Mbingu, ndiyo, mbingu za mbingu, haziwezi kukuenea;+ namna gani basi nyumba hii yenye nimejenga!+ 28 Sasa kaza uangalifu kwenye sala ya mutumishi wako na ombi lake la kuomba rehema, Ee Yehova Mungu wangu, na usikilize kilio cha kuomba musaada na sala yenye mutumishi wako anasali leo mbele yako. 29 Macho yako yafunguliwe kuelekea nyumba hii usiku na muchana, kuelekea mahali kwenye ulisema juu yake, ‘Jina langu litakuwa pale,’+ ili kusikiliza sala yenye mutumishi wako anasali kuelekea mahali hapa.+ 30 Na usikilize ombi la mutumishi wako la kuomba rehema na ombi la watu wako Israeli lenye wanaomba kuelekea mahali hapa, na usikie ukiwa katika makao yako mbinguni;+ ndiyo, usikie na usamehe.+
-