-
2 Mambo ya Nyakati 7:12-14Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
12 Kisha Yehova akamutokea Sulemani+ usiku na kumuambia: “Nimesikia sala yako, na nimechagua mahali hapa kwa ajili yangu ili kuwa nyumba ya zabihu.+ 13 Wakati ninafunga mbingu na hakuna mvua na wakati ninaamuru panzi wakule inchi na kama ninatuma ugonjwa wa kuambukiza kati ya watu wangu, 14 kama watu wangu wenye jina langu limeitwa juu yao+ wanajinyenyekeza+ na kusali na kutafuta uso wangu na wanageuka na kuacha njia zao zenye uovu,+ basi nitasikia kutoka mbinguni na nitasamehe zambi yao na kuponyesha inchi yao.+
-