-
1 Wafalme 8:37-40Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
37 “Kama njaa inatokea katika inchi,+ ao ugonjwa wa kuambukiza, ugonjwa wenye kukausha mimea, kuvu,+ nzige wenye kupatikana kwa wingi, ao nzige wenye kula sana;* ao kama adui yao anawazunguka kwa ajili ya vita katika muji wowote wa inchi* ao kama kunatokea aina ingine yoyote ya pigo ao ya ugonjwa,+ 38 sala yoyote, ombi lolote la kuomba rehema+ lenye linaweza kutolewa na mutu yeyote ao na watu wako wote Israeli (kwa maana kila mumoja anajua pigo la moyo wake mwenyewe)+ wakati wananyoosha mikono yao kuelekea nyumba hii, 39 basi usikie kule mbinguni, makao yako,+ na usamehe+ na utende; na upatie zawabu kila mumoja kulingana na njia zake zote,+ kwa maana unajua moyo wake (wewe peke yako unajua kwa kweli moyo wa kila mwanadamu),+ 40 ili wakuogope sikuzote zenye wanaishi katika inchi yenye ulipatia mababu zetu.
-