-
Matayo 21:7-9Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
7 Wakaleta huyo punda na mwana-punda wake, kisha wakaweka juu yao nguo zao za inje, na kukaa juu yake.+ 8 Wengi kati ya wale watu wakatandika nguo zao za inje katika barabara,+ na wengine walikuwa wanakata matawi ya miti na kuyatandika katika barabara. 9 Zaidi ya hilo, watu wengi wenye walikuwa mbele yake na wale wenye walikuwa wanamufuata wakaendelea kusema kwa sauti kubwa: “Okoa, tunaomba, Mwana wa Daudi!+ Amebarikiwa ule mwenye anakuja katika jina la Yehova!*+ Umuokoe, tunaomba, wewe mwenye kuwa kwenye nafasi za juu!”+
-
-
Marko 11:7-10Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
7 Wakamupelekea Yesu ule mwana-punda,+ wakaweka nguo zao za inje juu yake, na Yesu akakaa juu yake.+ 8 Pia, wengi wakatandika nguo zao za inje katika barabara, lakini wengine wakakata matawi yenye majani katika mashamba.+ 9 Na watu wenye walikuwa mbele na wale wenye walikuwa wanafuata nyuma wakaendelea kusema kwa sauti kubwa: “Umuokoe, tunaomba!+ Amebarikiwa ule mwenye anakuja katika jina la Yehova!*+ 10 Ubarikiwe Ufalme wenye unakuja wa baba yetu Daudi!+ Umuokoe, tunaomba, wewe mwenye kuwa kwenye nafasi za juu!”
-
-
Luka 19:37, 38Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
37 Wakati tu alikaribia barabara yenye kushuka kutoka kwenye Mulima wa Mizeituni, kundi lote la wanafunzi likaanza kushangilia na kumusifu Mungu kwa sauti kubwa kwa sababu ya matendo yote yenye nguvu yenye walikuwa wameona, 38 na kusema: “Amebarikiwa Ule mwenye anakuja akiwa Mufalme katika jina la Yehova!* Amani mbinguni, na utukufu kwenye nafasi za juu!”+
-