-
Mwanzo 39:7, 8Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
7 Kisha mambo hayo, bibi ya bwana wake akaanza kumuangalia na kumutamani sana Yosefu na kusema: “Lala na mimi.” 8 Lakini akakataa na kumuambia bibi ya bwana wake: “Angalia, bwana wangu haangaikie kile ninafanya katika nyumba hii, na ameweka vitu vyake vyote katika mikono yangu.
-
-
Kumbukumbu la Torati 13:6-8Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
6 “Kama ndugu yako, mutoto mwanaume wa mama yako, ao mutoto wako mwanaume ao mutoto wako mwanamuke ao bibi yako mwenye unapenda ao rafiki yako wa karibu sana* anajaribu kukushawishi kwa uficho, na kusema, ‘Tuende na tutumikie miungu mingine,’+ miungu yenye wewe wala mababu zako hawakujua, 7 kati ya miungu ya vikundi vya watu vyenye kuwazunguka pande zote, ikuwe karibu na ninyi ao mbali na ninyi, kuanzia mwisho mumoja wa inchi mupaka mwisho mwingine wa inchi, 8 haupaswe kukubali ushawishi wake wala kumusikiliza,+ wala usimusikitikie wala kumusikilia huruma wala kumulinda;
-