Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • 2 Samweli 18:15
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 15 Kisha watumishi kumi (10) wenye walibeba silaha za Yoabu wakakuja na kumupiga Absalomu mupaka akakufa.+

  • 2 Samweli 20:1
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 20 Sasa kulikuwa mufanya-fujo fulani mwenye aliitwa Sheba,+ mwana wa Bikri, Mubenyamini. Alipiga baragumu+ na kusema: “Hatuna fungu lolote katika Daudi, na hatuna uriti wowote katika mwana wa Yese.+ Ee Israeli,+ kila mutu aende kwa miungu* yake!”

  • 2 Samweli 20:22
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 22 Mara moja mwanamuke huyo mwenye hekima akaenda kuzungumuza na watu wote, nao wakakata kichwa cha Sheba mwana wa Bikri na kukitupia Yoabu. Basi Yoabu akapiga baragumu, nao wakasambaa kutoka kwenye muji huo, kila mumoja akaenda kwenye nyumba yake;+ na Yoabu akarudia Yerusalemu kwa mufalme.

  • 1 Wafalme 2:22
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 22 Halafu Mufalme Sulemani akamujibu mama yake: “Sababu gani unaomba Abishagi Mushunamu kwa ajili ya Adoniya? Pengine utamuombea pia ufalme,+ kwa maana yeye ni ndugu yangu mukubwa,+ na anaungwa mukono na Abiatari kuhani na Yoabu+ mwana wa Seruya.”+

  • 1 Wafalme 2:24
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 24 Na sasa, kama vile hakika Yehova anaishi, mwenye ameniweka imara kabisa+ na kuniikalisha kwenye kiti cha ufalme cha Daudi baba yangu na kunifanyia nyumba,*+ kama vile aliahidi, Adoniya atauawa+ leo.”

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine