-
2 Samweli 15:2-4Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
2 Absalomu alikuwa anaamuka asubui sana na kusimama pembeni ya barabara yenye inaenda kwenye mulango mukubwa wa muji.+ Kila mara wakati mutu fulani alikuwa na kesi ya hukumu yenye ilipaswa kupelekwa kwa mufalme ili iamuliwe,+ Absalomu alikuwa anamuita na kusema: “Unatoka katika muji gani?” naye alikuwa anasema: “Mutumishi wako anatoka katika kabila moja kati ya makabila ya Israeli.” 3 Absalomu alikuwa anamuambia: “Angalia, malalamiko yako ni ya kweli na ya haki, lakini hakuna mutu kutoka kwa mufalme wa kusikia kesi yako ya hukumu.” 4 Absalomu alikuwa anasema: “Ingekuwa muzuri kama ningewekwa kuwa muamuzi katika inchi! Basi kila mutu mwenye kuwa na kesi ya hukumu ao hukumu angekuja kwangu, na ningehakikisha kwamba anatendewa haki.”
-