-
2 Wafalme 24:15, 16Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
15 Basi akakamata Yehoyakini+ na kumupeleka katika uhamisho Babiloni;+ akapeleka pia mama ya mufalme, bibi za mufalme, maofisa wa makao ya mufalme, na watu wa kwanza katika inchi, akawakamata kutoka Yerusalemu na kuwapeleka katika uhamisho Babiloni. 16 Mufalme wa Babiloni alikamata pia na kupeleka katika uhamisho Babiloni wapiganaji-vita wote, elfu saba (7 000), na pia mafundi na wenye kufua chuma* elfu moja (1 000), wote walikuwa wanaume wenye nguvu na wenye wamezoezwa kwa ajili ya vita.
-
-
Yeremia 24:1Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
24 Kisha Yehova akanionyesha vitunga mbili vya tini vyenye viliwekwa mbele ya hekalu la Yehova, kisha Mufalme Nebukadneza* wa Babiloni kupeleka katika uhamisho Yekonia*+ mwana wa Yehoyakimu,+ mufalme wa Yuda, pamoja na wakubwa wa Yuda, mafundi, na mafundi wa vyuma;* aliwachukua kutoka Yerusalemu na kuwapeleka Babiloni.+
-