-
1 Samweli 21:1-6Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
21 Kisha wakati fulani Daudi akafika Nobu+ kwa kuhani Ahimeleki. Ahimeleki akaanza kutetemeka wakati alikutana na Daudi, na akamuambia: “Sababu gani uko peke yako na hakuna mutu pamoja na wewe?”+ 2 Daudi akamujibu kuhani Ahimeleki: “Mufalme aliniagiza nifanye jambo fulani, lakini alisema, ‘Usimujulishe mutu yeyote kuhusu kazi yenye ninakutuma ufanye na kuhusu maagizo yenye nimekupatia.’ Nilisikilizana na vijana wangu tukutane mahali fulani. 3 Sasa kama uko na mikate tano (5), unipatie tu mikate hiyo, ao kitu chochote chenye kitapatikana.” 4 Lakini kuhani akamuambia Daudi: “Kwa sasa hakuna mikate ya kawaida, lakini kuko mikate mitakatifu+—ikiwa tu vijana wako wamejiepusha* na wanamuke.”+ 5 Daudi akamujibu kuhani: “Hakika tumejiepusha na wanamuke kama vile tulifanya mbele wakati nilienda katika mapambano ya kijeshi.+ Kama miili ya vijana hawa ni mitakatifu hata wakati kazi yenye walitumwa wafanye ni ya kawaida, je, haiko mitakatifu zaidi leo?” 6 Kwa hiyo kuhani akamupatia mikate mitakatifu,+ kwa sababu hapakukuwa mikate ingine isipokuwa mikate ya wonyesho, yenye ilikuwa imeondolewa mbele ya Yehova ili mikate mipya iwekwe pa nafasi yake siku hiyo yenye iliondolewa.
-