-
Marko 3:1-6Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
3 Yesu akaingia tena katika sinagogi, na mutu mumoja mwenye mukono wenye kukauka* alikuwa pale.+ 2 Kwa hiyo, watu walikuwa wanamuangalia sana waone kama atamuponyesha ule mutu siku ya Sabato, ili wamushitaki. 3 Akamuambia ule mutu mwenye mukono wenye kukauka:* “Simama na ukuje katikati.” 4 Kisha akawaambia: “Je, inaruhusiwa siku ya Sabato kufanya mema ao mabaya, kuokoa uzima* ao kuua?”+ Lakini wakabakia kimya. 5 Kisha kuwaangalia huku na huku kwa kasirani, akiwa amehuzunika sana kwa sababu walikuwa na mioyo migumu,+ akamuambia ule mutu: “Nyoosha mukono wako.” Akaunyoosha, na mukono wake ukapona. 6 Basi Wafarisayo wakaenda inje na mara moja wakaanza kufanya mukutano juu yake pamoja na wafuasi wa chama cha Herode,+ ili kumuua.
-
-
Luka 6:6-11Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
6 Siku ingine ya Sabato+ aliingia katika sinagogi na akaanza kufundisha. Na pale kulikuwa mutu mumoja mwenye mukono wake wa kuume ulikuwa wenye kukauka.*+ 7 Waandishi na Wafarisayo walikuwa sasa wanamuangalia Yesu sana waone kama ataponyesha siku ya Sabato, ili wapate njia fulani ya kumushitaki. 8 Lakini, alijua mawazo yao,+ basi akamuambia ule mutu mwenye mukono wenye kukauka:* “Simama na ukuje katikati.” Na akainuka na kusimama pale. 9 Kisha Yesu akawaambia: “Ninawauliza ninyi, je, inaruhusiwa siku ya Sabato kufanya mambo ya muzuri ao mambo ya mubaya, kuokoa uzima* ao kuuharibu?”+ 10 Kisha kuwaangalia wote huku na huku, akamuambia mutu huyo: “Nyoosha mukono wako.” Akaunyoosha, na mukono wake ukapona. 11 Lakini wakakasirika sana, na wakaanza kuzungumuza kati yao ni jambo gani wangemutendea Yesu.
-