Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • Danieli 9:27
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 27 “Na atafanya agano liendelee kufanya kazi kwa ajili ya wengi kwa juma moja; na katika nusu ya juma hilo atamaliza mambo ya zabihu na toleo la zawadi.+

      “Na juu ya bawa la machukizo kutakuwa ule mwenye analeta uharibifu;+ na mupaka wakati wa maangamizi, kile chenye kiliamuliwa kitamwangwa pia juu ya ule mwenye ameharibiwa.”

  • Danieli 11:31
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 31 Na mikono itasimama,* kutoka kwake; na kuchafua patakatifu,+ ile ngome, na kuondoa zabihu ya kuendelea.+

      “Na watasimamisha lile chukizo lenye linaleta uharibifu.+

  • Danieli 12:11
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 11 “Na tangu wakati ile zabihu ya kuendelea+ itakuwa imeondolewa, na lile chukizo lenye linaleta uharibifu litakuwa limesimamishwa,+ kutakuwa siku elfu moja mia mbili makumi kenda (1 290).

  • Marko 13:14-18
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 14 “Hata hivyo, wakati mutaona lile chukizo lenye linaleta uharibifu+ likiwa limesimama mahali halipaswe kuwa (musomaji atumie utambuzi), basi wale wenye kuwa katika Yudea waanze kukimbilia kwenye milima.+ 15 Mutu mwenye kuwa kwenye sehemu ya juu ya nyumba asishuke wala asiingie ndani ili kukamata kitu chochote katika nyumba yake; 16 na mutu mwenye kuwa katika shamba asirudilie vitu vyenye kuwa nyuma ili kukamata nguo yake ya inje. 17 Ole wao wanamuke wenye mimba na wale wenye kunyonyesha watoto katika siku hizo!+ 18 Muendelee kusali kwamba mambo hayo yasifike katika kipindi cha baridi;

  • Luka 21:20
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 20 “Lakini, wakati mutaona Yerusalemu imezungukwa na majeshi yenye kupiga kambi,+ basi mujue kwamba uharibifu wake umekaribia.+

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine