-
Danieli 9:27Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
27 “Na atafanya agano liendelee kufanya kazi kwa ajili ya wengi kwa juma moja; na katika nusu ya juma hilo atamaliza mambo ya zabihu na toleo la zawadi.+
“Na juu ya bawa la machukizo kutakuwa ule mwenye analeta uharibifu;+ na mupaka wakati wa maangamizi, kile chenye kiliamuliwa kitamwangwa pia juu ya ule mwenye ameharibiwa.”
-
-
Marko 13:14-18Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
14 “Hata hivyo, wakati mutaona lile chukizo lenye linaleta uharibifu+ likiwa limesimama mahali halipaswe kuwa (musomaji atumie utambuzi), basi wale wenye kuwa katika Yudea waanze kukimbilia kwenye milima.+ 15 Mutu mwenye kuwa kwenye sehemu ya juu ya nyumba asishuke wala asiingie ndani ili kukamata kitu chochote katika nyumba yake; 16 na mutu mwenye kuwa katika shamba asirudilie vitu vyenye kuwa nyuma ili kukamata nguo yake ya inje. 17 Ole wao wanamuke wenye mimba na wale wenye kunyonyesha watoto katika siku hizo!+ 18 Muendelee kusali kwamba mambo hayo yasifike katika kipindi cha baridi;
-