-
Luka 22:67-71Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
67 “Kama wewe ndiye Kristo, utuambie.”+ Lakini akasema: “Hata kama ningewaambia, hamungeamini hata kidogo. 68 Zaidi ya hayo, kama ningewauliza, hamungenijibu. 69 Hata hivyo, kuanzia sasa Mwana wa binadamu+ atakaa kwenye mukono wa kuume wenye nguvu wa Mungu.”+ 70 Halafu wote wakamuuliza: “Kwa hiyo, je, wewe ndiye Mwana wa Mungu?” Akawaambia: “Ninyi wenyewe munasema kwamba mimi ndiye.” 71 Wakasema: “Sababu gani tutafute ushahidi zaidi? Kwa maana sisi wenyewe tumejisikilia kutoka katika kinywa chake mwenyewe.”+
-