-
Matayo 8:24-27Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
24 Sasa angalia! upepo mukali ukatokea katika bahari, mupaka mawimbi yalikuwa yanafunika mashua;* lakini Yesu alikuwa amelala usingizi.+ 25 Wakakuja, wakamuamusha, na kusema: “Bwana, utuokoe, tuko karibu kufa!” 26 Lakini akawaambia: “Sababu gani munaogopa sana,* ninyi wenye imani kidogo?”+ Kisha akasimama na kukemea upepo na bahari, na kukakuwa utulivu mukubwa.+ 27 Basi wanafunzi wakashangaa na kusema: “Huyu ni mutu wa namna gani? Hata upepo na bahari vinamutii.”
-
-
Luka 8:23-25Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
23 Lakini wakati walikuwa katika safari, akalala usingizi. Na zoruba kali yenye upepo mukali ikatokea katika bahari, na mashua* yao ikaanza kujaa maji na kuwa katika hatari.+ 24 Basi wakaenda kumuamusha na kusema: “Mwalimu, Mwalimu, tuko karibu kufa!” Halafu akaamuka, akakemea upepo na muchafuko wa maji, na hivyo vikatulia, na kukakuwa utulivu.+ 25 Kisha akawaambia: “Imani yenu iko wapi?” Lakini walikuwa wameogopa sana, wakashangaa, na kuambiana: “Kwa kweli huyu ni nani? Kwa maana anaamuru hata upepo na maji, na vinamutii.”+
-