Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • Matayo 8:24-27
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 24 Sasa angalia! upepo mukali ukatokea katika bahari, mupaka mawimbi yalikuwa yanafunika mashua;* lakini Yesu alikuwa amelala usingizi.+ 25 Wakakuja, wakamuamusha, na kusema: “Bwana, utuokoe, tuko karibu kufa!” 26 Lakini akawaambia: “Sababu gani munaogopa sana,* ninyi wenye imani kidogo?”+ Kisha akasimama na kukemea upepo na bahari, na kukakuwa utulivu mukubwa.+ 27 Basi wanafunzi wakashangaa na kusema: “Huyu ni mutu wa namna gani? Hata upepo na bahari vinamutii.”

  • Luka 8:23-25
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 23 Lakini wakati walikuwa katika safari, akalala usingizi. Na zoruba kali yenye upepo mukali ikatokea katika bahari, na mashua* yao ikaanza kujaa maji na kuwa katika hatari.+ 24 Basi wakaenda kumuamusha na kusema: “Mwalimu, Mwalimu, tuko karibu kufa!” Halafu akaamuka, akakemea upepo na muchafuko wa maji, na hivyo vikatulia, na kukakuwa utulivu.+ 25 Kisha akawaambia: “Imani yenu iko wapi?” Lakini walikuwa wameogopa sana, wakashangaa, na kuambiana: “Kwa kweli huyu ni nani? Kwa maana anaamuru hata upepo na maji, na vinamutii.”+

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine