-
Matayo 15:15-20Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
15 Petro akamuambia: “Utufasirie mufano huo.” 16 Basi akasema: “Je, ninyi pia bado hamuelewe?+ 17 Hamujue kama kitu chochote chenye kinaingia katika kinywa kinapita ndani ya tumbo na kisha kinatoka na kuingia katika choo?* 18 Lakini, mambo yenye yanatoka katika kinywa yanatoka katika moyo, na mambo hayo ndiyo yanamuchafua mutu.+ 19 Kwa mufano, mawazo mabaya:+ mauaji, uzinifu, uasherati,* wizi, ushahidi wa uongo, na maneno ya kumutukana Mungu, yanatoka katika moyo. 20 Hayo ndiyo mambo yenye yanamuchafua mutu; lakini kula bila kunawa mikono* hakumuchafue mutu.”
-