-
Matayo 17:1-8Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
17 Kisha siku sita (6), Yesu alimuchukua Petro, Yakobo na Yohana ndugu yake na kuwapeleka kwenye mulima murefu wakiwa peke yao.+ 2 Na akageuzwa sura mbele yao; uso wake ukangaa kama jua, na nguo zake za inje zikangaa* kama mwangaza.+ 3 Na angalia! Musa na Eliya wakawatokea, na walikuwa wanazungumuza naye. 4 Kisha Petro akamuambia Yesu: “Bwana, ni muzuri kwetu kuwa hapa. Kama unataka, nitasimamisha mahema tatu (3) hapa, moja yako, moja ya Musa, na moja ya Eliya.” 5 Wakati alikuwa angali anasema, angalia! wingu lenye kungaa likawafunika, na angalia! sauti kutoka katika lile wingu ikasema: “Huyu ni Mwana wangu, mupendwa, mwenye nimekubali.+ Mumusikilize.”+ 6 Wakati wanafunzi walisikia jambo hilo, wakapiga magoti na kuinama mupaka chini, na wakaogopa sana. 7 Basi Yesu akawakaribia, akawagusa na kusema: “Musimame. Musiogope.” 8 Wakati waliinua macho, hawakuona mutu yeyote lakini Yesu peke yake.
-
-
Luka 9:28-36Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
28 Kwa kweli, karibu siku munane (8) kisha kusema maneno hayo, akamuchukua Petro, Yohana, na Yakobo na wakapanda kwenye mulima ili kusali.+ 29 Wakati alikuwa anasali, sura ya uso wake ikabadilika, na nguo zake zikakuwa na weupe wenye kungaa. 30 Na angalia! wanaume wawili walikuwa wanazungumuza naye; walikuwa Musa na Eliya. 31 Hawa walitokea wakiwa na utukufu na wakaanza kuongea juu ya kuondoka kwake, kwenye alikuwa karibu kutimiza kule Yerusalemu.+ 32 Sasa Petro na wale wenye walikuwa pamoja naye walikuwa wamelemewa na usingizi, lakini wakati waliamuka kabisa, wakaona utukufu wake+ na wale wanaume wawili wenye walikuwa wanasimama pamoja naye. 33 Na wakati wale wanaume walikuwa wanaondoka na kuachana naye, Petro akamuambia Yesu: “Mwalimu, ni muzuri kwetu kuwa hapa. Basi, tusimamishe mahema tatu (3), moja yako, moja ya Musa, na moja ya Eliya.” Hakujua kile alikuwa anasema. 34 Lakini wakati alikuwa anasema mambo haya, wingu likatokea na kuanza kuwafunika kwa kivuli. Wakati walikuwa wanafunikwa na wingu, wakaogopa. 35 Kisha sauti+ ikatoka katika lile wingu ikisema: “Huyu ni Mwana wangu mwenye amechaguliwa.+ Mumusikilize.”+ 36 Wakati ile sauti ilikuwa inasema, Yesu akaonekana akiwa peke yake. Lakini wakabakia kimya na siku hizo hawakumuambia mutu jambo lolote kati ya mambo yenye waliona.+
-