-
Matayo 17:14-17Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
14 Wakati walifika kwenye watu wengi walikuwa,+ mutu fulani akamukaribia Yesu, akamupigia magoti, na kusema: 15 “Bwana, sikilia mwana wangu huruma, kwa sababu iko* na kifafa na ni mugonjwa. Anaanguka mara nyingi ndani ya moto na ndani ya maji.+ 16 Nilimuleta kwa wanafunzi wako, lakini hawakuweza kumuponyesha.” 17 Yesu akajibu na kusema: “Enyi kizazi chenye hakina imani na chenye kupotoka,+ nitaendelea kuwa pamoja na ninyi mupaka wakati gani? Nitawavumilia mupaka wakati gani? Mumulete hapa.”
-
-
Luka 9:38-42Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
38 Na angalia! mutu fulani katikati ya wale watu wengi akaita kwa sauti kubwa, na kusema: “Mwalimu, ninakuomba uangalie mwana wangu, kwa sababu yeye ni mwana wangu mumoja tu.+ 39 Na angalia! roho muovu anazoea kumushika, na mara moja anafanya makelele, na ule roho anamutikisa-tikisa na anatokwa na pofu kwenye kinywa, na hamuache mupaka amuumize. 40 Niliomba wanafunzi wako wamufukuze, lakini hawakuweza.” 41 Yesu akajibu na kusema: “Enyi kizazi chenye hakina imani na chenye kupotoka,+ nitaendelea kuwa pamoja na ninyi na kuwavumilia mupaka wakati gani? Leta mwana wako hapa.”+ 42 Lakini hata wakati alikuwa anakaribia, ule pepo muchafu akamuangusha chini na kumufanya ajigeuze-geuze. Hata hivyo, Yesu akamukemea ule roho muchafu na kumuponyesha ule kijana mwanaume, kisha akamurudishia baba yake.
-